Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
SERIKALI inapoteza Sh bilioni 33 kila mwezi kutokana na uchanganyaji wa mafuta ya taa na dizeli unaofanywa na madereva wa malori ya mizigo nchini.
Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Chama cha Wamiliki wa Malori ya Kusafirishia Mizigo (TATOA), Zacharia Poppe wakati akizungumza katika Kamati ya Bunge ya Miundombinu.
Alisema kiwango cha mafuta ya taa kinachochanganywa katika mafuta ya dizeli ni kikubwa na kinapunguza kiwango cha mafuta hayo kuingizwa nchini.
Mafuta ya taa hayana kodi, na kutokana na kutumika kuchanganywa katika dizeli kunasababisha kupotea kwa fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika kwa miradi mingine ya maendeleo, alisema Poppe.
Alisema hivi karibuni malori 88 ya dizeli yaliyokuwa yakitokea Tanzania yalikamatwa nchini Burundi kutokana na kuchanganywa na mafuta ya taa, hali ambayo imefikia hatua ya kuiomba serikali kutoza kodi kwa mafuta ya taa au kuuzwa kwa bei kubwa ili kupunguza vitendo hivyo.
Jambo la ajabu pindi dereva anapokamatwa akiwa amechanganya mafuta ya taa kwenye dizeli yeye hakamatwi ila lawama zinamwangukia mmiliki wa gari, kwa nini asishtakiwe kwa kuwa yeye ndio mwizi? Alihoji Poppe.
Alisema endapo biashara ya dizeli itaanguka ni hasara pia kwa serikali kwa kuwa itakosa mapato huku vipuri vya magari vikiharibika ovyo.
Kuhusu ajali za barabarani, Mkurugenzi wa Mipango kutoka wakala wa ujenzi wa barabara Tanroads, Johnson Rwiza alisema ipo haja kwa mamlaka zinazohusika kuwachunguza na kuwachuja madereva mienendo na tabia zao kabla ya kupewa leseni hali ambayo inaweza kupunguza ajali.
Akichangia mada kuhusu ajali, Mbunge wa Rorya, Philemon Sarungi alisema ipo haja kwa mamlaka zinazohusika kuwapima akili madereva kabla ya kupatiwa leseni ili kujua ukamilifu wa afya zao.
Alishauri kazi hiyo iende pamoja na kuwashirikisha madaktari ili kuwapima ugonjwa wa kisukari, akili, shinikizo la damu na kwa wale ambao akili zao sio nzuri, wafanyiwe mtihani baada ya miaka mitatu kwa ajili kupimwa zaidi. annet
Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Chama cha Wamiliki wa Malori ya Kusafirishia Mizigo (TATOA), Zacharia Poppe wakati akizungumza katika Kamati ya Bunge ya Miundombinu.
Alisema kiwango cha mafuta ya taa kinachochanganywa katika mafuta ya dizeli ni kikubwa na kinapunguza kiwango cha mafuta hayo kuingizwa nchini.
Mafuta ya taa hayana kodi, na kutokana na kutumika kuchanganywa katika dizeli kunasababisha kupotea kwa fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika kwa miradi mingine ya maendeleo, alisema Poppe.
Alisema hivi karibuni malori 88 ya dizeli yaliyokuwa yakitokea Tanzania yalikamatwa nchini Burundi kutokana na kuchanganywa na mafuta ya taa, hali ambayo imefikia hatua ya kuiomba serikali kutoza kodi kwa mafuta ya taa au kuuzwa kwa bei kubwa ili kupunguza vitendo hivyo.
Jambo la ajabu pindi dereva anapokamatwa akiwa amechanganya mafuta ya taa kwenye dizeli yeye hakamatwi ila lawama zinamwangukia mmiliki wa gari, kwa nini asishtakiwe kwa kuwa yeye ndio mwizi? Alihoji Poppe.
Alisema endapo biashara ya dizeli itaanguka ni hasara pia kwa serikali kwa kuwa itakosa mapato huku vipuri vya magari vikiharibika ovyo.
Kuhusu ajali za barabarani, Mkurugenzi wa Mipango kutoka wakala wa ujenzi wa barabara Tanroads, Johnson Rwiza alisema ipo haja kwa mamlaka zinazohusika kuwachunguza na kuwachuja madereva mienendo na tabia zao kabla ya kupewa leseni hali ambayo inaweza kupunguza ajali.
Akichangia mada kuhusu ajali, Mbunge wa Rorya, Philemon Sarungi alisema ipo haja kwa mamlaka zinazohusika kuwapima akili madereva kabla ya kupatiwa leseni ili kujua ukamilifu wa afya zao.
Alishauri kazi hiyo iende pamoja na kuwashirikisha madaktari ili kuwapima ugonjwa wa kisukari, akili, shinikizo la damu na kwa wale ambao akili zao sio nzuri, wafanyiwe mtihani baada ya miaka mitatu kwa ajili kupimwa zaidi. annet