Serikali yapitisha mabadiliko ya katiba Simba, uwekezaji sasa njia nyeupe

Serikali yapitisha mabadiliko ya katiba Simba, uwekezaji sasa njia nyeupe

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) imeidhinisha rasmi marekebisho ya Katiba ya klabu ya Simba baada ya kukamilika kwa mchakato wa kisheria uliokuwa chini ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Michezo.

1771420748772.png

Ikumbukwe Februari 16, 2026, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda alimuagiza Msajili wa Vyama vya Michezo kuhakikisha kuwa mchakato wa marekebisho ya Katiba ya Simba unapatiwa majibu kabla ya mwezi kumalizika.

Soma > Makonda ampa msajili siku 12 kumaliza utata Simba

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Februari 18, 2026, Msajili wa Vyama vya Michezo nchini, Abel Ngilangwa, amesema marekebisho hayo yamefanyika kwa kuzingatia Sheria na Kanuni zote zinazosimamia vyama vya michezo nchini.

“Napenda kuufahamisha umma kuwa mchakato wa uchambuzi, tathmini na uidhinishaji wa marekebisho ya Katiba ya Klabu ya Simba umekamilika kwa mujibu wa Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa Sura ya 49 na kanuni zake,” amesema Ngilungwa

Ngilangwa ameongeza kuwa Katiba hiyo iliyorekebishwa iliwasilishwa kwa mujibu wa Kanuni ya 11 ya Kanuni za Msajili wa Vyama vya Michezo T.S Na. 441 ya mwaka 1999 kwa ajili ya kupitiwa na kuidhinishwa.

1771420995405.png
Aidha ameeleza kuwa Msajili alitekeleza wajibu wake kwa mujibu wa Kanuni ya 11(3)(a) ya Kanuni za Msajili wa Vyama vya Michezo T.S Na. 441 ya mwaka 1999, inayomtaka kuhakikisha marekebisho yoyote ya katiba hayaathiri usalama, hayavurugi amani miongoni mwa wanachama au jamii kwa ujumla, wala kuathiri maendeleo ya chama.


1771489377095.png

1771489419438.png

1771489432685.png

1771489444177.png
 
Serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) imeidhinisha rasmi marekebisho ya Katiba ya klabu ya Simba baada ya kukamilika kwa mchakato wa kisheria uliokuwa chini ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Michezo.


Ikumbukwe Februari 16, 2026, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda alimuagiza Msajili wa Vyama vya Michezo kuhakikisha kuwa mchakato wa marekebisho ya Katiba ya Simba unapatiwa majibu kabla ya mwezi kumalizika.

Soma > Makonda ampa msajili siku 12 kumaliza utata Simba

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Februari 18, 2026, Msajili wa Vyama vya Michezo nchini, Abel Ngilangwa, amesema marekebisho hayo yamefanyika kwa kuzingatia Sheria na Kanuni zote zinazosimamia vyama vya michezo nchini.

“Napenda kuufahamisha umma kuwa mchakato wa uchambuzi, tathmini na uidhinishaji wa marekebisho ya Katiba ya Klabu ya Simba umekamilika kwa mujibu wa Sheria ya Baraza la Michezo la Taifa Sura ya 49 na kanuni zake,” amesema Ngilungwa

Ngilangwa ameongeza kuwa Katiba hiyo iliyorekebishwa iliwasilishwa kwa mujibu wa Kanuni ya 11 ya Kanuni za Msajili wa Vyama vya Michezo T.S Na. 441 ya mwaka 1999 kwa ajili ya kupitiwa na kuidhinishwa.

Aidha ameeleza kuwa Msajili alitekeleza wajibu wake kwa mujibu wa Kanuni ya 11(3)(a) ya Kanuni za Msajili wa Vyama vya Michezo T.S Na. 441 ya mwaka 1999, inayomtaka kuhakikisha marekebisho yoyote ya katiba hayaathiri usalama, hayavurugi amani miongoni mwa wanachama au jamii kwa ujumla, wala kuathiri maendeleo ya chama.

Mbona kwenye mkutano wa wanachama hayo marekebisho yalisomwa tuu na Mangungu na hayakupitishwa kwa kuyapigia kura?
Ina maana serikali haina taarifa za kikao hicho cha wanachama?
Dah hii nchi kila kitu shida.
 
Mmh!Hapa kuna tatizo na hapo mbeleni kuna mnyukano mwingine utakuja kuibuka tu kwanini siku zote msajili alishindwa kuipitisha mpaka aagizwe na waziri?
 
Kwa jambo hili huyo msajili hastahili kuendelea kukaa ofisini.

Maana anaonekana anafanya mambo kwa maelekezo sio kwa utashi wa taaluma yake.

Kumbe jambo lilikuwa linawezekana ila danadana zikawa nyingi.
 
Mbona kwenye mkutano wa wanachama hayo marekebisho yalisomwa tuu na Mangungu na hayakupitishwa kwa kuyapigia kura?
Ina maana serikali haina taarifa za kikao hicho cha wanachama?
Dah hii nchi kila kitu shida.
Marekebisho yalijadiliwa na kupitishwa, katika ule mkutano kuna watu walipangwa kuzuia mabadiliko kilichotokea kuna mtu alisoma maazimio ya wanachama 250 ambayo yalibariki maelekezo ya mwanasheria mkuu na watu wakapigia makofi yakawa yamepitishwa.
Wale watu waliopangwa walisubiri Mangungu alete ajenda ili wafanye fujo lakini Mangungu kwa kutambua mabadiliko yameshapitishwa akafunga mkutano.
Tatizo la Simba watu wako kwa ajili ya maslahi binafsi na sio maslahi ya Simba na hicho ndio chanzo cha mgogoro.
 
Back
Top Bottom