Makange
Member
- Jul 27, 2007
- 27
- 1
Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Stephen Wasira, akizungumza na waandishi wa habari alipotoa ripoti ya uchunguzi na maamuzi ya serikali kuhusu wakazi wa eneo la Tabata Dampo lililovunjwa mwezi uliopita.Serikali imeamua kuwalipa wamiliki wa nyumba 80 zilizovunjwa kila mmoja sh milioni 20 na viwanja bure.Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Kandoro.Akisoma Tamko la Serikali jijini Dar es Salaam jana kufuatia matokeo ya Tume Maalumu ya Kuchunguza Ubomoaji wa Nyumba hizo,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Stephen Wassira, alisema uamuzi huo wa serikali unatokana na kubaini kwamba ubomoaji huo haukuzingatia uamuzi wa Baraza la Ardhi.
Akifafanua kuhusu hilo, Wassira alitaja taratibu hizo ambazo zilipaswa kuzingatiwa kwamba ni kufikisha dhamira hiyo ya ubomoaji kwanza katika vikao vya juu vya timu ya menejimenti na vikao vya Baraza la Madiwani.Wassira aliongeza kwamba, taratibu nyingine zilizokiukwa, ni wananchi kutoshirikishwa katika azma ya ubomoaji huo kitu ambacho ni kinyume cha misingi na kanuni za utawala bora huku kukiwa na harufu ya rushwa.
Source: http://haki-hakingowi.blogspot.com/2008/04/serikali-yamwaga-sh1.html
Akifafanua kuhusu hilo, Wassira alitaja taratibu hizo ambazo zilipaswa kuzingatiwa kwamba ni kufikisha dhamira hiyo ya ubomoaji kwanza katika vikao vya juu vya timu ya menejimenti na vikao vya Baraza la Madiwani.Wassira aliongeza kwamba, taratibu nyingine zilizokiukwa, ni wananchi kutoshirikishwa katika azma ya ubomoaji huo kitu ambacho ni kinyume cha misingi na kanuni za utawala bora huku kukiwa na harufu ya rushwa.
Source: http://haki-hakingowi.blogspot.com/2008/04/serikali-yamwaga-sh1.html