Ndugu zangu. Nawaomba wale wote mnaoweza kumtetea Ndugu Ponda dhidi ya mashitaka anayokabiliwa nayo, basi aende kule kotini akawasiliane na wakili wa utetezi ili apewe nafasi hiyo. Vinginevyo tukikaa tu na kuendelea kumtetea kupitia JF ambako hakuna kesi dhidi ya Ponda, tutasababisha mtu huyu afungwe kwa kukosekana ushahidi wa kumtetea, halafu ndio tutaendelea kulalamika zaidi kwamba kaonewa. Haya shime, katoeni ushahidi Mahakamani utakaomsaidia ku counter hoja zilizowasilishwa hapo Mahakamani dhidi ya mtu huyu. Kumtetea Ponda humu JF hakumsaidii kabisa kwa sasa, ni sawa na kupiga kelele tu, halafu mwisho wa siku akapigwa mvua hivi hivi kwa uzembe wenu wenye ushahidi wa kumuokoa.