Serikali ya wanyonge inapozidi kuwakandamizi wanyonge! Baada ya NHIF, Mamlaka za Maji nazo zapandisha tozo

Kingjr2

JF-Expert Member
Sep 8, 2018
644
1,271
Natumai wale watumiaji wanufaika na huduma za maji kutoka Mamlaka za maji wamepata ujumbe unaowataarifu mabadiliko ya tuzo ya huduma hizo

Sina ugomvi na mabadiliko hayo ila najiuliza maswali yafuatayo:

1. Taarifa ya mabadiliko imetolewa jana ikisema tuzo hizo zitaanzia tarehe mosi desemba 2019, kwanini wamezitumia kwenye units zilizosomwa kabla ya tarehe moja desemba? Ki utaratibu si ilitakiwa matumizi ya kuanzia tarehe moja Desemba ndio yahusike na tuzo hizo mpya?

2. Ni sababu zipi/maboresho yapi yamepelekea mabadiliko ya tuzo hizo hasa huku kwetu Morogoro tunapopata huduma ya maji kwa mbinde kwa baadhi ya mitaa?

3. Tumeelezwa mabadiliko hayo ni kwa mujibu wa sheria, hivi hawa watunga sheria hizi ndio sheria za kumsaidia mnyonge?

4. Ni lini serikali hii inayojinadi kuwa serikali ya wanyonge itaacha kuwanyonga hawa wanyonge?

Tumeona NHIF na vifurushi vyao si rafiki kwa wanyonge, sasa Mamlaka za maji nazo tozo zake si rafiki kwa wanyonge! Sasa hawa wanyonge wanaponea wapi?

5. Hivi raia wanaoshangalia pale serikali inaposifiwa kwamba inawajali wanyonge, huwa wanaona nini? Ni wapi serikali imewapa wanyonge kipaumbele?

Ni kwenye afya? Sina hakika! Kwenye Maji? Nisaidieni! Labda kwenye Elimu! Tujiulize, shule zetu zinakidhi vigezo? Watoto wa wakubwa wanasoma na wakwetu madarasa hayo hayo?

Sasa ni wapi wanyonge wanapopewa nafuu! Labda wenzangu mnisaidie!

Screenshot_20191204-021119~2.jpeg
 
Mmmh, kufa hatufi ila cha moto ni kwa wote.

Hii ndo awamu ya 5 serikali ya wanyonge (mf. majumbani Tsh. 1.600/- ongezeko ni Tsh. 530/-) hilo ni ongezeko kubwa mno, ukilinganisha na huduma itolewayo na hiyo idara. (Maji kukatika mara kwa mara)

Shirika linataka litoe giwio na kusifu kupitia kwa mnyonge, mnyonge anaishia kulalamika tu hana namna ya kupinga hata kwa maandamo ambayo ni haki yake haruhusiwi ila maandamo ya kusifia ruksa.

Raia nchi nyingine ongezeko la mkate au mafuta tu utawaona wanavyoandamana kupinga ongezeko lo lote lile. Anyway tutafika wanapopataka wao na sio sisi tunapopataka!
 
Mmh! Tshs 1600 - 1070 = 530/=. Ongezeko hili ni 49.5%. Ni ongezeko kubwa mno kwa walaji.
 
Serikali inayojali wanyonge, ni kauli ya kisiasa iliyojaa unafiki, hasa awamu hii.
 
Kwa taarifa za kuaminika hapo bado sana tena ndo mwanzo tu!!!Bado kuna tozo za visima zinakuja,bado tozo kwenye afya,maji na mifugo bado sana!!!UNAFIKIRI DENI LA TAIFA LILILOPANDA NANI ATALIPA?KILA MTZ MILION MOJA!!!
 
Kama wameharibu uchumi na gawio lahitahika njia pekee ni kwa watumiaji wa huduma
 
Kwa akili zenu mtaitwa WANYONGE mpaka mwisho,endeleeni kuisoma namba na hamasisha Wenzio mfanye2 maandamano kuunga juhudi za ndugu Chatle.
 
Kingjr2,
Mkuu kipi bora ubaki na bei za zamani lakini maji yasiwepo kutokana na mamlaka husika kushindwa kugharamia gharama za uendeshaji? Unit moja ni sawa na ndoo za lita 20 hamsini (50); kwa bei ya TZS 1600 kwa unit ni sawa ni TZS 32 kwa ndoo; linganisha na bei na ubora wa maji unayouziwa huko mtaani pindi maji ya mamlaka yakikosekana kwenye mabomba.

Kabla ya EWURA hawajapitisha hizo tozo kuna mikutano hufanyika kuwahusisha wadau; nadhani wewe ulikuwa umebanwa na majukumu hukuhudhuria.
 
CCM OYE EEE sisi wanyonge tulio kosa elimu OOOYEEEEEE natuna weka na kapambio KIDUMU MILELEEEEE.
 
Ndachuwa, Wajinga wa kiwango chako hamkosekani kamwe, yaani na wewe umeona hii ni comment ya kumpa mlipa kodi wa nchi hii?
 
Kingjr2,
Wengi ni mkumbo tu ukiwauliza kwa nn wanaisifia thithiem utasikia wanasema huoni madaraja,nidhamu serikalini jamaa linatumbua tu muda wowote yaan lile jamaa pamoja na akili zake kuwa hvy ila likiamua limeamua yaan ni upuuz tu wakitoka hapo hata nauli za kwenda kutafutia kazi hawana,wazee ndio kabisa wanasifia wakimaliza wanalalamika hawana hela maisha magumu,tuwaache tu na uzwazwa wao,tufanyeje sasa huku wamesharogwa na wakarogeka na vifuvu na vishanga vikiinuliwa tu chali wanajichekesha chekesha
 
Back
Top Bottom