Ukiona Rais ambaye ni mtumishi namba moja wa wananchi anaweka malengo ili wananchi wake waishi kama Mashetani huyo ni wa kupingwa na kila mtu.
Ukiona Rais anayesema msinidrive, msinijaribu kisa tu hataki kukosolewa, jua taifa lina changamoto.
Ukiona Rais asiyependa uhuru wa habari, huyo yupo mita moja kabla ya udikteta.
Ukiona Rais anakataza shughuli halali za kisiasa na kuwafunga wapinzani bila sababu maalumu, huyo ni wa kumpinga.
Ukiona Rais anayepanga na kupangua kila siku, jua uwezo wa kuona kizuri na kukiteua ni the first place ni mdogo.
Ukiona mamilioni wanasema fulani ni dikteta, jua siyo wote wamekurupuka.