Serikali ya Tanzania kufungia matumizi ya mitandao ya kijamii kwenye intaneti ya serikali

Kama ni kufungia matumizi yasiyo rasimi muda wa kazi naunga mkono %100 coz hakna kitu kinachokera kama waenda office flani kutaka huduma waambiwa mtaandao unasumbua njoo siku nyingine na hapo umefunga safari labda kutoka Lushoto hadi Tanga mjini.
 
Hao wafanyakazi wenyewe kuwakuta ofisini mtihani saa ngapi wanafanya hayo mambo
Kuna chuo nilienda kipo mjini kabisa muhasibu anaingia saa3 na nusu na saa8 kashatoka ofisini
 
Watumishi wabanwe kufikia malengo na sio kupigana na mitandao. Bora watumishi wawapo kazini wasalimishe simu zao. Wanaotumia mitandao ni wengi mfano wafanya biashara wawapo katika ofisi za serikali wakisubiri huduma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu ni wagumu kuelewa jamani,iyo ishu inahusu wale wanaotumia rasilimali gvt ikiwemo internet kwa matumizi binafsi wakati serikali inalipia.Ukihitaji mitandao ya kijamii+kudownload movies tumia rasilimali zako binafsi.mfano mzuri wakati tuko college kuna net ya bure ambayo wanafunzi tunaitumia vibaya ikiwemo kudownload movies,ngono kinyume na utaratibu.
Sawa kabisa kutumia internet ya kazini kwa matumizi binafsi ni kosa na ni vibaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Safi sana
wanalipwa mishahara kwa kodi zetu halafu wao wanashinda kwenye FB
 
Serikali ya Tanzania kufungia matumizi ya mitandao ya kijamii kwenye intaneti ya serikali wakati wa kazi, kuanzia saa 1:30 asubuhi hadi saa 9:30 alasiri.

Inaonekana serikali haijatambua 80% ya biashara za kisasa zinafanyikia mtandaoni,huko insta na facebook watu wanamobile electronic shops.

Wameshazoea kudraw pesa za mshahara kila mwisho wa mwezi wamesahau kuna vingine vinavyowapa wenzao kula kama biashara kupitia mitandao.

Wanadhani mitandao ni sehemu ya kutafutia mademu na kujionyesha La hasha hizi ni ofisi kama zilivyo zakwao.

Kama ukiweza kumanage biashara kiganjani kwako wewe ni bora kuliko mwenye fremu kibao anaeka kusubiri wanaopita.

Mimi nadhani ni muda wa serikali kutambua mitandao ya kijamii ni ofisi za watu.

Kama wanataka kufungia wadisconnect network katika majengo yao ya serikali tu.
View attachment 849176View attachment 849175View attachment 849174View attachment 849173

======

Serikali ya Tanzania imezuia matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watumishi wa umma wakati wa kazi kwa madai yanaathiri kasi ya mtandao wa intaneti ya Serikali.

Pia, imedai watumishi wengi wanapoteza muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii kuliko kutekeleza majukumu yao.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk Laurean Ndumbaro kwa taasisi zote za umma, imeonya juu ya matumizi mabaya ya mitandao ya mawasiliano ya Serikali na kwamba, hatua hiyo imelenga kudhibiti matumizi ya mitandao.

“Kasi ya mtandao wa Serikali inapungua kutokana na matumizi makubwa ya mitandao ya kijamii hususan inayopakua video, mfano “YouTube” na hivyo kusababisha watumishi wengine wanaotumia mtandao wa intaneti wa Serikali katika kutekeleza majukumu yao kuathirika,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Aidha, taarifa hiyo inaeleza juu ya upakuaji wa nyaraka zenye hatimiliki bila idhini ya wamiliki kwa kutumia Intaneti ya Serikali kinyume na utaratibu.

“Mitandao ya kijamii haitapatikana kwenye intaneti ya Serikali wakati wa muda wa kazi kuanzia saa 1:30 asubuhi hadi saa 9:30 alasiri,” inaeleza taarifa hiyo.

Hata hivyo, Menejimenti ya Utumishi imezitaka taasisi zenye mahitaji maalumu ya matumizi ya mitandao ya kijamii wakati wa saa za kazi, kuwasilisha maombi yao kwa katibu mkuu wa utumishi yakiambatana na sababu za maombi hayo.

“Watumishi wa umma hawataweza kupakua nyaraka, picha na video zenye hatimiliki kwenye intaneti ya Serikali bila idhini ya wamiliki.”

Kwa mara kadhaa, Serikali imekuwa ikitoa miongozo ya matumizi ya Tehama kwa taasisi za Serikali ikiwamo kukataza matumizi ya mitandao kupitia intaneti ya Serikali saa za kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
it could have been done sooner…I wondered why our government tolerated this for too long! As usual, my responsible 5th government regime almost always spot on, took the correct measure! bravo!
 
Watu ni wagumu kuelewa jamani,iyo ishu inahusu wale wanaotumia rasilimali gvt ikiwemo internet kwa matumizi binafsi wakati serikali inalipia.Ukihitaji mitandao ya kijamii+kudownload movies tumia rasilimali zako binafsi.mfano mzuri wakati tuko college kuna net ya bure ambayo wanafunzi tunaitumia vibaya ikiwemo kudownload movies,ngono kinyume na utaratibu.
wenye akili kama hizi ni wachache sana mijitu inajua kukosoa tuuu haiangalii hata kuelewa kilichoongelewa.
 
Bora unakuta mtu customer officer anaacha kuhudumia wateja yuko busy JF au kwenye ma blogs

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii bado haitamzuia mfanyakazi wa serikali kutumia muda wake kama inavyopaswa, kwani anaweza kununua bando kwa gharama zake binafsi. Kubwa tu waseme wanapunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa serikali... Sababu nyingine sizielewi japo najaribu kuzielewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sioni sababu ya watanzania kulalama... Kweli matumizi ya internet ya serikali mara nyingi siyo kwa lengo husika... Kwa makadirio zaidi ya 80% wanaitumia kwa kudaka vistori vya mtaani na kucheki clips za matukio mbalimbali nje na malengo ya kazi.... Naunga serikali mkono katika hili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ya Tanzania kufungia matumizi ya mitandao ya kijamii kwenye intaneti ya serikali wakati wa kazi, kuanzia saa 1:30 asubuhi hadi saa 9:30 alasiri.

Inaonekana serikali haijatambua 80% ya biashara za kisasa zinafanyikia mtandaoni,huko insta na facebook watu wanamobile electronic shops.

Wameshazoea kudraw pesa za mshahara kila mwisho wa mwezi wamesahau kuna vingine vinavyowapa wenzao kula kama biashara kupitia mitandao.

Wanadhani mitandao ni sehemu ya kutafutia mademu na kujionyesha La hasha hizi ni ofisi kama zilivyo zakwao.

Kama ukiweza kumanage biashara kiganjani kwako wewe ni bora kuliko mwenye fremu kibao anaeka kusubiri wanaopita.

Mimi nadhani ni muda wa serikali kutambua mitandao ya kijamii ni ofisi za watu.

Kama wanataka kufungia wadisconnect network katika majengo yao ya serikali tu.
View attachment 849176View attachment 849175View attachment 849174View attachment 849173

======

Serikali ya Tanzania imezuia matumizi ya mitandao ya kijamii kwa watumishi wa umma wakati wa kazi kwa madai yanaathiri kasi ya mtandao wa intaneti ya Serikali.

Pia, imedai watumishi wengi wanapoteza muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii kuliko kutekeleza majukumu yao.

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dk Laurean Ndumbaro kwa taasisi zote za umma, imeonya juu ya matumizi mabaya ya mitandao ya mawasiliano ya Serikali na kwamba, hatua hiyo imelenga kudhibiti matumizi ya mitandao.

“Kasi ya mtandao wa Serikali inapungua kutokana na matumizi makubwa ya mitandao ya kijamii hususan inayopakua video, mfano “YouTube” na hivyo kusababisha watumishi wengine wanaotumia mtandao wa intaneti wa Serikali katika kutekeleza majukumu yao kuathirika,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Aidha, taarifa hiyo inaeleza juu ya upakuaji wa nyaraka zenye hatimiliki bila idhini ya wamiliki kwa kutumia Intaneti ya Serikali kinyume na utaratibu.

“Mitandao ya kijamii haitapatikana kwenye intaneti ya Serikali wakati wa muda wa kazi kuanzia saa 1:30 asubuhi hadi saa 9:30 alasiri,” inaeleza taarifa hiyo.

Hata hivyo, Menejimenti ya Utumishi imezitaka taasisi zenye mahitaji maalumu ya matumizi ya mitandao ya kijamii wakati wa saa za kazi, kuwasilisha maombi yao kwa katibu mkuu wa utumishi yakiambatana na sababu za maombi hayo.

“Watumishi wa umma hawataweza kupakua nyaraka, picha na video zenye hatimiliki kwenye intaneti ya Serikali bila idhini ya wamiliki.”

Kwa mara kadhaa, Serikali imekuwa ikitoa miongozo ya matumizi ya Tehama kwa taasisi za Serikali ikiwamo kukataza matumizi ya mitandao kupitia intaneti ya Serikali saa za kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwani hao IT System administrator wanafanya nn kama hawajui kufanya configuration za Firewall and Implememnt security protocal to filter kila kitu
 
Back
Top Bottom