sheria ni msumeno
kama ndivyo wezi wa fedha za IPTL-Escrow wangeshitakiwa
sheria ni msumeno
huyu mhuni mbowe lazima ashughulikiwe ipasavyo
Good umempa za uso huyo gamba
ujinga kama huu kamwe huwa hautoki
Mtatanga tanga sana nyie ccm
Hai. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameingia matatani baada ya Mahakama ya Wilaya ya Hai kuona ana kesi ya kujibu katika mashtaka ya kumshambulia mwangalizi wa ndani katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.
Uamuzi huo ulitolewa jana na hakimu mfawidhi wa wilaya hiyo, Denis Mpelembwa mbele ya Mbowe, wakili wake, Issa Rajabu na mwendesha mashtaka, Inspekta Marwa Mwita.
Mpelembwa alisema mashahidi saba wa upande wa mashtaka wameishawishi mahakama kuwa siku hiyo kuna tafrani ambayo ilitokea na ambayo Mbowe
atatakiwa kutoa ufafanuzi wa kuhusika kwake.
Alisema ingawa upande wa utetezi ukiongozwa na wakili Albert Msando na baadaye Rajabu, ulitoa hoja kuwa ushahidi wa Jamhuri uliacha mashimo mengi, yeye anaona Mbowe ana kesi ya kujibu.
Katika hoja zao (utetezi) wanaona ukiacha ushahidi wa Nassir Yamin, hakuna shahidi mwingine aliyethibitisha kushuhudia Nassir akipigwa, alisema akinukuu hoja za mawakili wa utetezi.
Hakimu aliongeza kusema: Utetezi pia walitoa hoja kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuwaita akina mama ambao wanaodaiwa kushuhudia, hivyo kuacha mashimo mengi katika ushahidi wao.
Hata hivyo, hakimu alisema katika hoja zao ambazo ziliishawishi mahakama, upande wa mashitaka ulijibu kuwa sheria haiwabani kuleta kila shahidi kujenga msingi wa kesi yao.
Ni rai yao (mashtaka) kuwa mashahidi wao saba wameweza kuthibitisha shtaka dhidi ya mshtakiwa pasipo kuacha mashaka ama mianya kama utetezi walivyodai, alisema Mpelembwa.
Hakimu Mpelembwa alisema baada ya kupitia hoja za mawakili wa pande zote mbili, anaona upande wa Jamhuri umeweza kuishawishi mahakama kuwa mshtakiwa ana kesi ya kujibu.
Kutokana na uamuzi huo, Hakimu alisema mahakama inampa nafasi Mbowe kujitetea na kesi hiyo imepangwa kutajwa Julai 17, siku upande wa utetezi utakapotoa orodha ya mashahidi wao.
Katika uchaguzi huo mkuu wa 2010, Mbowe aliibuka mshindi kwa kupata kura 28,585 akifuatiwa na Fuya Kimbita (CCM), kura 23,349, Hawa Kihogo (UDP) 258 na Petro Kisimbo (TLP) 135.
Chanzo: Mwananchi
*****************
Hapa ndio Gongo haijahahalishwa rasmi sijui ikihalalishwa itakuwaje?
Wenu
Tume ya Katiba
Katika kile
kinachoonekana kumweka bussy Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe tayari
kesi iliyofunguliwa miaka minne huko nyuma imefufuliwa.
Kesi hiyo iliyoratibiwa na CCM alifunguliwa Mbowe kipindi cha uchaguzi
mkuu uliopita kwa madai kwamba alimshambulia msimamizi wa Uchaguzi huko
HAI.
Hapo jana kesi hiyo iliibuka na Hakimu akasoma kile kilichosemwa ni
hukumu ya awali kwa kusema kwamba Mbowe ana kesi ya Kujibu na anapaswa
kujitetea.
Ikumbukwe kwa sasa Mbowe mbali ya kuwa Mwenyekiti wa Chadema ndiye
Mwenyekiti pia wa Ukawa na ndiye kinara wa mapambano ya Katiba ya
wananchi.
Yana mwisho haya tunakaribia mwishoni
Tuwekee ushahidi. Uhalifu wake unafanana na wa Razalo Nyalandu, Change, Riziwani, Lowasa, Werema na Magamba wote.Mbowe ni mharifu kama wahalifu wengine tu hivyo lazima sheria ichukue nafasi yake kwa watu wahalifu kama yeye.
Mbowe ni mharifu kama wahalifu wengine tu hivyo lazima sheria ichukue nafasi yake kwa watu wahalifu kama yeye.
kama ndivyo wezi wa fedha za IPTL-Escrow wangeshitakiwa
miaka yote4 walikiwa wapi?
Sheria wameijua leo? UKAWA hawatorudi bungeni kwa style hii ng'o
Mbowe alimpiga vibao wakala wake kwa kuhisi kuwa anapanga kumsaliti.
mkulu lwakatare part 2 lini?madhara ya kutumia kichwa kufugia tu nywele yameanza kukutesa
sheria ni msumeno
Kama nyie sio vibaraka na watumwa wa mabwana zenu,yule mwanasheria Mkuu kachukuliwa hatua gani kwa kumtishia kumkata kichwa Kafulila na kumkata mangumi ndani ya bunge??!!
Rage na wenzie pale Dodoma walichukuliwa hatua gani kwa kumpiga kwa miti na mawe kada wa CHADEMA??!!
Mnalipwa bure tu hapo Lumumba,bora wote mngekuwa na jinsia kama ya Juliana Shonza tungewavumilia uhalali wa malipo yenu!!!