gemmanuel265
JF-Expert Member
- Feb 16, 2016
- 8,485
- 18,047
Utawala huu wa awamu ya tano umekuwa utawala wa hovyo sana toka nchi hii kupata uhuru wake, ni utawala unaotoa haki kwa double standard sana
Wakati anaingia madarakani Rais Magufuli alianza kuvunja katiba na sheria za nchi kwa kupiga marufuku shughuli halali za vyama vya siasa (upinzani) maana ccm wao waliendelea kuzunguka nchi nzima pamoja na yeye Rais Magufuli alikuwa anazunguka nchini kwa mwamvuli wa ziara za kiserikali, lakini ukweli hazikuwa ziara za kiserikali maana alikuwa anapokea wanachama wapya wa ccm kutoka vyama pinzani.
Mara baada ya uchaguzi mkuu 2015 aliyekuwa mgombea urais kupitia Chadema kwa muungano wa Ukawa Edward Lowassa alitaka kuanza ziara nchi nzima kuwashukuru wapiga kura wake milioni 6, lakini alipigwa marufuku kufanya hivyo kwa sababu za kijinga kwamba siasa hadi 2020.
Leo hii Edward Lowassa amerudi ccm ameruhusiwa kufanya mikutano ya kisiasa sababu yuko ccm! Lakini Wapinzani wanaambiwa wafanye mikutano kwenye majimbo yao ya uchaguzi pekee vinginevyo wataishia jela, hii ni hatari sana kuwa na rais anayenyima haki wananchi wake.
Tumeona mahakama ilivyogeuka kuwa sehemu uporaji haki kwa wakosoaji wa serikali hii, wale mahakimu/majaji wenye kukandamiza haki za wapinzani wamekuwa wakizawadiwa nafasi za juu zaidi maana msimamizi wa haki amegeuka kuwa mporaji wa haki za wananchi.
Tumeona wapinzani wakipigwa, kujeruhiwa na hata kuuawa lakini hakuna siku Rais aliwahi kunyanyua mdomo wake na kuviagiza vyombo vya usalama kukomesha matukio hayo, kwenye tukio la kupigwa risasi Mh Lissu aliishia kutweet tu kana kwamba halikuwa tukio la kusikitisha.
Wakosoaji wakubwa wa serikali hii wamekuwa wakipitia maisha magumu sana kwa awamu hii, wako watu wamefilisiwa, kuuawa, kujeruhiwa na wengine kubaki na vilema vya maisha lakini vyombo vya usalama vimekuwa na makengeza juu ya matukio hayo.
Tukio la kushambuliwa Mh Lissu na serikali kukataa kumpa haki zake za matibabu pamoja na kukataa kufanya uchunguzi wa tukio hilo ni ushahidi wa wazi kuwa serikalini kuna tatizo kubwa sana kwenye mfumo wa utoaji haki nchini.
Tumeona rangi yao halisi hakuna jambo jema na lenye maana kama kuongea ukweli usiowapendeza watawala wasiotenda haki katika jamii.
Tunalazimishwa kuwa kimya kwa sababu eti kuna maendeleo yanafanywa! Huu ni aina ya ukoloni kama ule wa kabla ya uhuru 1960, binadamu hakuumbwa kula na kufanya kazi tu, hata katiba inatoa uhuru wa watu kuongea, kukosoa na kukosolewa na haki ya kwenda popote, haki ya kukutana na kukusanyika.
Wakoloni walijenga miundo mbinu, hospital, shule n.k lakini tuliwakataa kwa sababu walitunyima haki yetu ya asili, haki ya kujiamulia, kushirikishwa, kusikilizwa, kulindwa na kukusanyika, leo haya yote tumenyimwa kwa kigezo kile kile cha kikoloni kujengewa reli na barabara, tunataka sheria na katiba iwe ndio muongozo wa kitaifa, hatuhitaji urais wa kifalme katika karne hii ya 21 wakati sisi ni democratic society.
Tunahitaji kuona mamlaka ya nchi ikipambana na hali mbaya ya;
Uchumi
Elimu bure mbovu
Biashara kudorora
Usalama wa raia
Kilimo
Umoja wa kitaifa
Utawala bora
Haki za binadamu
Deni la taifa
Uduni wa maisha
Diplomasia ya kimataifa, n.k
Bado ccm ni ile ile haina dhamira ya kweli kujenga taifa lenye watu wema na waadilifu wanaoweza kujitoa muhanga kulinda maslahi ya umma kwa gharama ya kukosa.
Wakati anaingia madarakani Rais Magufuli alianza kuvunja katiba na sheria za nchi kwa kupiga marufuku shughuli halali za vyama vya siasa (upinzani) maana ccm wao waliendelea kuzunguka nchi nzima pamoja na yeye Rais Magufuli alikuwa anazunguka nchini kwa mwamvuli wa ziara za kiserikali, lakini ukweli hazikuwa ziara za kiserikali maana alikuwa anapokea wanachama wapya wa ccm kutoka vyama pinzani.
Mara baada ya uchaguzi mkuu 2015 aliyekuwa mgombea urais kupitia Chadema kwa muungano wa Ukawa Edward Lowassa alitaka kuanza ziara nchi nzima kuwashukuru wapiga kura wake milioni 6, lakini alipigwa marufuku kufanya hivyo kwa sababu za kijinga kwamba siasa hadi 2020.
Leo hii Edward Lowassa amerudi ccm ameruhusiwa kufanya mikutano ya kisiasa sababu yuko ccm! Lakini Wapinzani wanaambiwa wafanye mikutano kwenye majimbo yao ya uchaguzi pekee vinginevyo wataishia jela, hii ni hatari sana kuwa na rais anayenyima haki wananchi wake.
Tumeona mahakama ilivyogeuka kuwa sehemu uporaji haki kwa wakosoaji wa serikali hii, wale mahakimu/majaji wenye kukandamiza haki za wapinzani wamekuwa wakizawadiwa nafasi za juu zaidi maana msimamizi wa haki amegeuka kuwa mporaji wa haki za wananchi.
Tumeona wapinzani wakipigwa, kujeruhiwa na hata kuuawa lakini hakuna siku Rais aliwahi kunyanyua mdomo wake na kuviagiza vyombo vya usalama kukomesha matukio hayo, kwenye tukio la kupigwa risasi Mh Lissu aliishia kutweet tu kana kwamba halikuwa tukio la kusikitisha.
Wakosoaji wakubwa wa serikali hii wamekuwa wakipitia maisha magumu sana kwa awamu hii, wako watu wamefilisiwa, kuuawa, kujeruhiwa na wengine kubaki na vilema vya maisha lakini vyombo vya usalama vimekuwa na makengeza juu ya matukio hayo.
Tukio la kushambuliwa Mh Lissu na serikali kukataa kumpa haki zake za matibabu pamoja na kukataa kufanya uchunguzi wa tukio hilo ni ushahidi wa wazi kuwa serikalini kuna tatizo kubwa sana kwenye mfumo wa utoaji haki nchini.
Tumeona rangi yao halisi hakuna jambo jema na lenye maana kama kuongea ukweli usiowapendeza watawala wasiotenda haki katika jamii.
Tunalazimishwa kuwa kimya kwa sababu eti kuna maendeleo yanafanywa! Huu ni aina ya ukoloni kama ule wa kabla ya uhuru 1960, binadamu hakuumbwa kula na kufanya kazi tu, hata katiba inatoa uhuru wa watu kuongea, kukosoa na kukosolewa na haki ya kwenda popote, haki ya kukutana na kukusanyika.
Wakoloni walijenga miundo mbinu, hospital, shule n.k lakini tuliwakataa kwa sababu walitunyima haki yetu ya asili, haki ya kujiamulia, kushirikishwa, kusikilizwa, kulindwa na kukusanyika, leo haya yote tumenyimwa kwa kigezo kile kile cha kikoloni kujengewa reli na barabara, tunataka sheria na katiba iwe ndio muongozo wa kitaifa, hatuhitaji urais wa kifalme katika karne hii ya 21 wakati sisi ni democratic society.
Tunahitaji kuona mamlaka ya nchi ikipambana na hali mbaya ya;
Uchumi
Elimu bure mbovu
Biashara kudorora
Usalama wa raia
Kilimo
Umoja wa kitaifa
Utawala bora
Haki za binadamu
Deni la taifa
Uduni wa maisha
Diplomasia ya kimataifa, n.k
Bado ccm ni ile ile haina dhamira ya kweli kujenga taifa lenye watu wema na waadilifu wanaoweza kujitoa muhanga kulinda maslahi ya umma kwa gharama ya kukosa.