Serikali tuhurumieni watumishi

Serikali tuhurumieni watumishi

kikulu

Member
Joined
Mar 19, 2017
Posts
26
Reaction score
14
Ni mda sasa toka uhamisho kusitishwa, watumishi idara mbalimbali wamekuwa wakiomba kuhama hususani kwenda kwa wapendwa wao ( wake/waume) lakini wamezuiliwa kwa hoja ya uhakiki, ebu kuweni waungwana, mbona huko juu mnahamishana kwa kusingizia dharura?, tuna hali mbaya, kumwona mke mpaka likizo, hujui anaishije huko, anaoata vishawishi gani, au mnataka tume kwa UKIMWI? nasi tunapenda ndoa zetu kama mlivyo ninyi, tuhurumieni. Inaumiza sana
 
mkuu acha kazi, kujiajiri kunalipa!
 
Kodi juu no promotion kwa watumishi, no uhamisho, na hapa hatutoki kwasababu wakuu wakuu wa idara wooote wameshikwa pabaya. So I have made my way to go!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ntatukana bure..wacha nipite
 
mkuu acha kazi, kujiajiri kunalipa!
Ni kweli kujiajiri kunalipa na kila mmoja anatamani kufanya hivyo. Ila serikali kwa kuwa ni mwajiri, inatakiwa kuwajali waajiriwa wake. After all, hawa ndio wanaoisaidia serikali kuwahudumia watu wake. Hebu jiulize, kama ingetokea KILA MTU akajiajiri kama wewe ulivyojiajiri, ukienda hospitalini ungehudumiwa na nani? Mwanao angefundishwa na nani kama kila aliyekuwa mwalimu angejiajiri akaacha kazi ya kufundisha?

Tumezoea sana kuwakejeli watumishi wa umma au waajiriwa kwa kuwa wana maisha duni. Lakini ni muhimu tutambue kuwa kama binadamu, kila mmoja anahitaji huduma ambazo hutolewa na watu wengine. Kama kila mtu akijiajiri, maisha hayawezi kwenda. Yeye aliye mwajiri na atimize wajibu wake, na mwajiriwa kadhalika. Isije ikaonekana kama kuajiriwa ni laana.
 
Ni kweli kujiajiri kunalipa na kila mmoja anatamani kufanya hivyo. Ila serikali kwa kuwa ni mwajiri, inatakiwa kuwajali waajiriwa wake. After all, hawa ndio wanaoisaidia serikali kuwahudumia watu wake. Hebu jiulize, kama ingetokea KILA MTU akajiajiri kama wewe ulivyojiajiri, ukienda hospitalini ungehudumiwa na nani? Mwanao angefundishwa na nani kama kila aliyekuwa mwalimu angejiajiri akaacha kazi ya kufundisha?

Tumezoea sana kuwakejeli watumishi wa umma au waajiriwa kwa kuwa wana maisha duni. Lakini ni muhimu tutambue kuwa kama binadamu, kila mmoja anahitaji huduma ambazo hutolewa na watu wengine. Kama kila mtu akijiajiri, maisha hayawezi kwenda. Yeye aliye mwajiri na atimize wajibu wake, na mwajiriwa kadhalika. Isije ikaonekana kama kuajiriwa ni laana.
Ni kweli kabisa mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani kuna kitu kimefunga kwenye kifua hapa .. Ningeandka
 
Back
Top Bottom