Grace Komba
Senior Member
- May 26, 2013
- 131
- 48
Takribani wiki mbili sasa, tangu tume ya katiba, chini ya uenyekiti wa jaji mstaafu WARIOBA, watangaze rasimu ya kwanza ya katiba mpya.
Tume hii imekuja na mapendekezo kadhaa ambayo yanahitaji umakini mkubwa katika kuyajadili ili kama taifa tuweze kufanikisha suala hili.
Ila baada ya uzinduzi wa rasimu hii, ghafla makundi hasa ya wanasiasa na vyama vyao wametokea kulivalia njuga suala la serikali tatu, na hata baadhi yao kulihusisha na uhai wa muungano wetu,(Zanzibar na Tz bara).
NASISITIZA, SIPINGI kwa wanasiasa na wananchi kwa ujumla kujadili suala hili la serikali tatu, kama ilivyo pendekezwa na tume ya katiba.
Kinachonipa HOFU ni nguvu kubwa itumikayo na wanasiasa katika kuivuruga jamii kupitia suala hili la serikali tatu.
NI KWELI, Kujadili mifumo ya serikali zetu, na sura ya muungano wetu ni jambo muhimu na linalo hitaji umakini.
JE, suala la serikali tatu ndio PENDEKEZO PEKEE kwenye rasimu hii??
Kwanini HATUJADILI RASIMU HII KWA MAPANA YAKE??
Naomba Kuwasilisha...
Tume hii imekuja na mapendekezo kadhaa ambayo yanahitaji umakini mkubwa katika kuyajadili ili kama taifa tuweze kufanikisha suala hili.
Ila baada ya uzinduzi wa rasimu hii, ghafla makundi hasa ya wanasiasa na vyama vyao wametokea kulivalia njuga suala la serikali tatu, na hata baadhi yao kulihusisha na uhai wa muungano wetu,(Zanzibar na Tz bara).
NASISITIZA, SIPINGI kwa wanasiasa na wananchi kwa ujumla kujadili suala hili la serikali tatu, kama ilivyo pendekezwa na tume ya katiba.
Kinachonipa HOFU ni nguvu kubwa itumikayo na wanasiasa katika kuivuruga jamii kupitia suala hili la serikali tatu.
NI KWELI, Kujadili mifumo ya serikali zetu, na sura ya muungano wetu ni jambo muhimu na linalo hitaji umakini.
JE, suala la serikali tatu ndio PENDEKEZO PEKEE kwenye rasimu hii??
Kwanini HATUJADILI RASIMU HII KWA MAPANA YAKE??
Naomba Kuwasilisha...