Serikali na taasisi zake zinaihujumu TBC, bora Ryoba ajiuzulu tuwekeze Efm na Clouds

chibuga mugeta

JF-Expert Member
Jun 29, 2012
1,176
1,055
Ni jambo la kushangaza kuona kodi zetu zikitumika vibaya katika shirika la TBC. Taasisi za serikali karibia zote ukienda mapokezi wamefungulia CLOUDS au EFM, kwenye basi za mwendokasi hivyo hivyo na kwenye treni hivyo hivyo. Sasa hadi kwenye stendi za daladala kama mawasiliano na Ubungo mkoa hivyo hivyo.

Hii redio na TV zinajitangazaje? Bora zifutwe au wajiunge na EFM au CLOUDS maana wao ndo kila sehemu unawasikia. La sivyo tunaomba kodi zetu zisipelekwe huko. Hadi nahisi kuna mkono wa mtu au kuna viongozi wana hisa na hivi vyombo vya habari vingine na wanaihujumu serikali.

Mbaya zaidi mkurugenzi wa TBC na timu yake imelala fofofo. Kama mmeshindwa kuendesha msituharibie kodi zetu la sivyo laana itawajia ninyi na kizazi chenu.
 
Kwani ni lazima kusikiliza TBC Kisa idara za serikali, itabidi watumishwi waache kutumia voda tigo na Airtel maana wanahujumu TTCL.
 
Ngoja nikupangie ubora wa taarifa za habari kwenye Television zetu ili uone TBC walipo

1. ITV
2. CHANNEL 10
3.AZAM TWO
4. STAR TV
5. Clouds
6. (Jaza mwenyewe)

Mbaya zaidi hadi viongozi wa serikali wanacheki ITV
 
Kwani ni lazima kusikiliza TBC Kisa idara za serikali, itabidi watumishwi waache kutumia voda tigo na Airtel maana wanahujumu TTCL.
mkuu kama taasisi za serikali zinashindwa hata kui promote TBC unadhani watu wengine wataisikiliza,hasa umuhimu wa hiyo redio au TV uko wapi,bora ifungwe au ipelekwe nanjilinji,mi nilidhani sababu TBC imechakaa na amekuja mkurugenzi mpya naamini kuna vitu vipya ameanzisha na angetumia hizo taasisi na magari kama ya mwendokasi kuvitangaza ili watz waipende na warudi kusikiliza redio na kuangalia stesheni yao wanayoilipia kodi
 
Ngoja nikupangie ubora wa taarifa za habari kwenye Television zetu ili uone TBC walipo

1. ITV
2. CHANNEL 10
3.AZAM TWO
4. STAR TV
5. Clouds
6. (Jaza mwenyewe)

Mbaya zaidi hadi viongozi wa serikali wanacheki ITV
Nimeipenda dah basi kazi ipo kama ndo hivyo,bora ifutwe kodi zipelekwe pengine
 
Kwa mtazamo wangu,wangeiacha ijiendeshe yenyewe kibiashara tena bila kutegemea ruzuku wala chochote serikalini,lakini serikali hii ya wafu bado haijamka.
 
Ni jambo la kushangaza kuona kodi zetu zikitumika vibaya katika shirika la TBC. Taasisi za serikali karibia zote ukienda mapokezi wamefungulia CLOUDS au EFM, kwenye basi za mwendokasi hivyo hivyo na kwenye treni hivyo hivyo. Sasa hadi kwenye stendi za daladala kama mawasiliano na Ubungo mkoa hivyo hivyo.

Hii redio na TV zinajitangazaje? Bora zifutwe au wajiunge na EFM au CLOUDS maana wao ndo kila sehemu unawasikia. La sivyo tunaomba kodi zetu zisipelekwe huko. Hadi nahisi kuna mkono wa mtu au kuna viongozi wana hisa na hivi vyombo vya habari vingine na wanaihujumu serikali.

Mbaya zaidi mkurugenzi wa TBC na timu yake imelala fofofo. Kama mmeshindwa kuendesha msituharibie kodi zetu la sivyo laana itawajia ninyi na kizazi chenu.
Watanzania kwa kulalamika hatujambo.........!!! Kila kitu ni lawama na kulialia tu hadi inakera.
 
Ni jambo la kushangaza kuona kodi zetu zikitumika vibaya katika shirika la TBC. Taasisi za serikali karibia zote ukienda mapokezi wamefungulia CLOUDS au EFM, kwenye basi za mwendokasi hivyo hivyo na kwenye treni hivyo hivyo. Sasa hadi kwenye stendi za daladala kama mawasiliano na Ubungo mkoa hivyo hivyo.

Hii redio na TV zinajitangazaje? Bora zifutwe au wajiunge na EFM au CLOUDS maana wao ndo kila sehemu unawasikia. La sivyo tunaomba kodi zetu zisipelekwe huko. Hadi nahisi kuna mkono wa mtu au kuna viongozi wana hisa na hivi vyombo vya habari vingine na wanaihujumu serikali.

Mbaya zaidi mkurugenzi wa TBC na timu yake imelala fofofo. Kama mmeshindwa kuendesha msituharibie kodi zetu la sivyo laana itawajia ninyi na kizazi chenu.
Sasa wewe unataka mambo yaende kwa matakwa yako? Yaani unaifanya kama 'mtu' fulani asiyejiweza anayetia huruma unawasemea. Kama haisikilizwi Dar sisi huku tunaisikiliza? Ifutwe kwa sababu gani?
 
Watanzania kwa kulalamika hatujambo.........!!! Kila kitu ni lawama na kulialia tu hadi inakera.
kodi zetu kodi zetu ,PAYE kubwa gharama za maisha juu ni bora wangeondoa baadhi ya vitu visivyo na msingi na manufaa ili kodi ipungue,inauma sana ,tunakatwa kodi kwa lazima ila shughuli zenyewe nyingine hazionekan mfano ndo huo wa TBC
 
Sasa wewe unataka mambo yaende kwa matakwa yako? Yaani unaifanya kama 'mtu' fulani asiyejiweza anayetia huruma unawasemea. Kama haisikilizwi Dar sisi huku tunaisikiliza? Ifutwe kwa sababu gani?
Dar ni kioo cha jamii,hata Mwanza au Arusha yaani kwenye majiji yote TBC ni dhoofu,ndo maana naitetea kuwa bas hata kwenye vituo vya serikali ingesikika hata ule mlio wa kipindi cha kifo au taarifa ya habar jamani.
 
Back
Top Bottom