Memento
JF-Expert Member
- Jun 13, 2021
- 4,423
- 9,963
Wote ni mashuhuda kwa jinsi serikali ilivyojipambanua kukabiliana na janga la corona, na hii imepelekea wengi kupongeza hatua ambazo serikali imepanga/ilipanga kuzichukua.
Serikali imeweka mkazo mkubwa sana ili kulinda watu wake dhidi ya corona na ndio maana matamko mengi yametolewa na wakuu wa mikoa ili kukabiliana na hili suala.
Mkuu wa Mkoa Dar alisema daladala ziwe level seat, watu wote wavae barakoa na mikusanyiko hairuhusiwi.
Ni ukweli usiopingika kuwa corona inaua na imeua ndugu zetu wengi na bado inaendelea kuua.
Hivyo hatua hizi za mkuu wa mkoa Amos Makalla zipo sahihi Sana, lakini kwa nini hazisimamii?
Tatizo lipo hapo, matamko ya kila namna katoa kuhusu corona na mikusanyiko, lakini amekuwa ndio wa kwanza kuvunja kule nacho yeye mwenyewe aliagiza.
Au corona imeisha? Kama ni hivyo basi watu waambiwe, na Kama corona bado ipo mbona mnashindwa kusimamia maagizo yenu?
Jana mkuu wa mkoa alikuwa kwenye mkusanyiko huko wa ndondo cup, huku uwanja ukifurika bila watu kuchukua tahadhari zozote.
Leo tena uwanja wa taifa umefurika, hakuna social distancing Wala barakoa. Lakini mkuu wa mkoa yupo kimya kama haoni vile
Kama Jambo ni gumu kulitekeleza, serikali msiwe mnatoa matamko.
Serikali imeweka mkazo mkubwa sana ili kulinda watu wake dhidi ya corona na ndio maana matamko mengi yametolewa na wakuu wa mikoa ili kukabiliana na hili suala.
Mkuu wa Mkoa Dar alisema daladala ziwe level seat, watu wote wavae barakoa na mikusanyiko hairuhusiwi.
Ni ukweli usiopingika kuwa corona inaua na imeua ndugu zetu wengi na bado inaendelea kuua.
Hivyo hatua hizi za mkuu wa mkoa Amos Makalla zipo sahihi Sana, lakini kwa nini hazisimamii?
Tatizo lipo hapo, matamko ya kila namna katoa kuhusu corona na mikusanyiko, lakini amekuwa ndio wa kwanza kuvunja kule nacho yeye mwenyewe aliagiza.
Au corona imeisha? Kama ni hivyo basi watu waambiwe, na Kama corona bado ipo mbona mnashindwa kusimamia maagizo yenu?
Jana mkuu wa mkoa alikuwa kwenye mkusanyiko huko wa ndondo cup, huku uwanja ukifurika bila watu kuchukua tahadhari zozote.
Leo tena uwanja wa taifa umefurika, hakuna social distancing Wala barakoa. Lakini mkuu wa mkoa yupo kimya kama haoni vile
Kama Jambo ni gumu kulitekeleza, serikali msiwe mnatoa matamko.