Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Mimi sio mtaalamu wa masuala ya elimu , lakini kuna suala moja limenigusa nalo ni hili la shule za kata , katika miaka karibu 5 iliyopita shule za kati zimekuwa kwa wingi sana hapa nchini , watu mbali mbali wamepeleka watoto wao katika shule hizo , shule hizo nyingi hazina walimu wa kutosha na wale wenye uzoefu na kazi hizo matokeo yake ni kwa watoto wanaosoma katika shule hizi kutokumaliza shule au kufeli kwa wingi na matatizo mengine mengi .
Sijapata kuona ripoti yoyote inayoonyesha mafanikio ya shule hizi za kata ambazo zimezagaa sana nchini kwa sasa , zaidi ya kusikia habari za kutisha na kusikitisha toka katika wanafunzi wanaosoma humo au wazazi waliokuwa na wanafunzi katika shule hizo
Vile vile katika elimu ya juu ni nadra sana kukuta mwanafunzi pale aliyetoka katika shule za kata au katika masoko ya ajira nayo ni vile vile tumezoea kuona wanafunzi wa shule zile zile toka wakati wa uhuru
Serikali imejipanga vipi kuhusu matatizo ya shule hizi ambayo kwa kiasi kikubwa yanachochewa na mipango ambayo sio endelevu ya wizara husika pamoja na maslahi mengine ya kisiasa zaidi kuliko mambo halisi ?
Serikali imejiandaa vipi na suala la ajira huko mbeleni kwenye jumuiya ya afrika ya mashariki wakati wanafunzi wengi wa shule za kata ambao wangeweza kuleta ushindani huko mbeleni wanaishia njiani kutokana na mipango hii ?
Sijapata kuona ripoti yoyote inayoonyesha mafanikio ya shule hizi za kata ambazo zimezagaa sana nchini kwa sasa , zaidi ya kusikia habari za kutisha na kusikitisha toka katika wanafunzi wanaosoma humo au wazazi waliokuwa na wanafunzi katika shule hizo
Vile vile katika elimu ya juu ni nadra sana kukuta mwanafunzi pale aliyetoka katika shule za kata au katika masoko ya ajira nayo ni vile vile tumezoea kuona wanafunzi wa shule zile zile toka wakati wa uhuru
Serikali imejipanga vipi kuhusu matatizo ya shule hizi ambayo kwa kiasi kikubwa yanachochewa na mipango ambayo sio endelevu ya wizara husika pamoja na maslahi mengine ya kisiasa zaidi kuliko mambo halisi ?
Serikali imejiandaa vipi na suala la ajira huko mbeleni kwenye jumuiya ya afrika ya mashariki wakati wanafunzi wengi wa shule za kata ambao wangeweza kuleta ushindani huko mbeleni wanaishia njiani kutokana na mipango hii ?