Serikali na baadhi ya watu haielewi hoja ya wakazi wa mtwara...hii ndo hoja yao ya msingi

spartacus

JF-Expert Member
Sep 26, 2010
428
142
habari,
hivi karibuni baada ya maandamano ya wanamtwara tarehe 27/12/2012, kupinga uamuzi wa serikali kusafirisha gesi kwenda mkoani dar es salaam, umezuka mjadala mkubwa ambao pia umefanya watu watoe maoni yao mbalimbali juu ya uamuzi huo.
hii imepelekea hata baadhi ya wahariri wa magazeti kuandika makala mbalimbali wakisema wanamtwara wanakosea, kwa kutaka gesi ibaki mtwara....kiukweli kwa ufahamu wangu mdogo na utafiti wa siku 7 nilizokaa mtwara, nimegundua kuwa si kweli kwamba wanamtwara hawataki gesi iende mkoani Dar es salaam, bali wanataka iende sehemu tu ya gesi hiyo kwa ajili ya matumizi mengine, ila kwa suala la umeme,ni vema serikali ikajenga power plant mkoani humo, ili mkoa uwe na umeme wa uhakika, na kuvutia uwekezaji ili mkoa huo ujiinue kiuchumi, baada ya tegemeo lao la zao la korosho kunufaisha wachache...
kiukweli kwa mtwara, raslimali pekee waliyobaki nayo ni hiyo gesi, wanajiuliza, kama wameanza kuuza korosho tangu miaka ya 60 haijawasaidia, gesi hii ikiondoka, mkoa huu utabaki na nini??
mrahaba wa gesi unaochukuliwa na halmashauri husika, ni asilimia 0.3, yani kwenye tshs 100,000, halmashauri inapata tshs 3,000/=....hayo maendeleo yatafika lini.....
afu, hivi kiwanda kikijengwa mtwara, viwanda vingine vya wawekezaji vikajengwa mtwara, je mapato ya kodi yatachukuliwa na mtwara?? je kuna MTWARA REVENUE AUTHORITY?? Jibu ni hapana, regardless, kiwanda kijengwe wapi, mapato yanaingia taifani....kumbe hoja kubwa ya watu wa mtwara, si kupata mapato yatokanayo na gesi hiyo, hapana, bali, ni fursa za ajira, ambazo serikali yao haijawahi kuwapa tangu enzi za utawala wa hayati JK NYERERE.
waharirir waliondika makala kupinga madai ya wanamtwara, pengine wafanye tafiti na kueleza watanzania, mrahaba wa gesi ya songosongo na somanga, umewafikia watu wa wilaya ya kilwa mkoani lindi?? na je lindi, imenufaika na nini kinachoonekana..?? wafanye hivyo hivyo kwa kidatu, panapozalishwa umeme na kupelekwa dar es salaam.
alafu, serikali inakiri kuwa dar es salaam inazalisha 80% ya mapato ya nchi, je ni halali kwa serikali kufurahishwa na jambo hilo, nchi yenye mikoa zaidi ya 30 kutegemea mapato ya mkoa mmoja?? kwanini wasianzishe dar es salaam zingine hata tano, kwa maana kuwe na mikoa mingine zaidi ya mitano yenye kuzalisha mapato ya aina hiyo..?? ni hadi lini wasomi wote watabaki dar es salaam, ni hadi lini dar es salaam iendelee kufurika wakazi kwa kutafuta ajira na kubanana, itafika siku mji huo utafurika, hivi sasa wakazi wanatoka bagamoyo na mlandizi kwenda kufanya kazi kkoo na posta, je 2020 watatokea wapi? kwa nini serikali isitengeneze sehem nyingine ya kupeleka watu kwa lengo la kuinua uchumi wa maeneo husika na taifa kwa ujumla??
 
Mkuu hili swala Simbachawene juzi kajibu vizuri sana na hasa hili la umeme,
Nanaomba ni liseme nilivyo muelewa.
Dar kutazalishwa umeme wa zaidi ya 750 MW kwa hii gesi sasa ukijenga huu mtambo mtwara utaitaji lini Tatu za 250 MW kutoka mtwara kuja Dar na tukubaliane kuwa matumizi makubwa ya umeme nchi hii ni Dar. So Grarama ya kujenga hizo line tatu ni kubwa kuliko hilo Bomba, pia tukumbuke kuwa Gesi hii itatumika Majumbani na kwenye Magari na wanategemea kuza. Umeme utakao kuwa na gharama ya 8 Cent Dola kwa unit wakati kwasasa mafuta ni 40 cent Dola, na tanesco wanauza 13 Cent Dola. So itasaidia kupunguza gharama za umeme.

But all in all mtwara na lindi wanaoja nyingine za umuhimu na serekali lazima izione na kuzifanyia kazi na sio kutuma watu kama MUONGO kuja kuita watu WAAHINI kwa DATA za uongo eti Mtwara wapo kwenye Grid ya taifa yani waziri mzima hajuhi na povu lina mtoka kwa kuongea uongo.
 
Nijuavyo mimi, hakuna mtu yeyote anayebisha ya kuwa raslimali yeyote ile inayopatikana hapa nchini ni ya watanzania wote katika ujumla wao. Kitu kinachobishaniwa linapokuja ili suala la gasi ya Mtwara ni iwapo kuna ulazima wowote wa kuisafirisha gasi hiyo ikiwa ghafi hadi Dar-es-salaam, ndipo itumike kuzalisha umeme. Kulingana na nadharia ya uwekezaji, viwanda hujengwa ama pale marighafi husika inapokutwa au karibu na soko la bidhaa itakayozalishwa, kutegemea ni kipi kati ya hivyo viwili kuna hafueni ya gharama. Katika suala la gesi ya Mtwara, mimi naona hafueni ya gharama iko katika kuzalisha umeme huko na halafu ukasafirisha umeme huo kwa kutumia "line" ya "gride" ya taifa ambayo tayari ipo. Kwa njia hii itaokoa mabilioni ya fedha itakayotumika kujenga bomba ya kusafirishia gesi hadi Dar.

Inavyoelekea, nchi yetu imekuwa na mazoea ya kutozingatia gharama husika katika maamuzi yake kuhusiana na uwekezaji; ndiyo maana tunaruhusu mchanga wetu wenye madini kubebwu hadi ughaibuni eti kwaajili ya uchambuzi wa madini! Ebu tujiulize kipi rahisi, kuleta mitambo ya kuchambua hayo madini hapa nchini au kusafirisha huo mchanga mpakahuko ughaibuni? Jibu unalo wewe msomaji.
 
Mbona kabla ya hapo mpango ulikuwa ni kujenga power plant mtwara na hii hoja ya kujenga bomba kutoka mtwara kwenda Dar haukuwepo? halafu hizi data zinaandaliwa na watu tu. ukitaka kufahamu haya sikiliza kauli ya prof muhongo aliyesema mtwara tumo kwenye grid ya taifa!
 
Unachokisema ni kweli kabisa na ninachojua serikali si kwamba haijawaelewa wanamtwara mwana maana gani ila upotoshaji umefanyika kimakusudi kwa lengo la kisiasa...Ukiangalia tamko la serikali katika kujibu hoja za gesi wali base sana kulaumu vyama vya upinzani kushinikiza maandamao lakini si kaitika kujibu kile kilichokuwa kinaandamaniwa. Ninachoamnini ni kuwa kuna watu wana maslahi ya binafsi katika ishu hii ya gesi ila wanajificha nyuma ya "ubinafsi" wa watu wa mtwara.....
 
Join Date : 24th October 2010
Posts : 824
Rep Power : 581
Likes Received 26
Likes Given 0

Kwa nini hutoi like kwa wenzio!!!!

Hoja: "Wakazi wa Mtwara wana haki ya kuwa watu wa kwanza kuipata gesi hiyo tena kwa bei nafuu, na pia wana haki ya kupata manufaa mengine yanayotokana na gesi hiyo kama ajira, kuboreshwa kwa miundombinu kabla ya gesi kusafirishwa kwa wengine...maendeleo yanapaswa kuanzia pale zinakopatikana maliasili husika"-Johnson Mbwambo
 
Naishangaa serikali hii kwani wananchi wa Mtwara siyo watanzania? Tusipoangalia tunaweza kujikuta badala ya kuinua uchumi tunazidi kuuzorotesha kutokana na kujiongezea mzigo wa madeni. Tumeambia hela ya kujenga bomba ni takribani trilioni 4 na huu ni mkopo kutoka benki ya exim ya China. Tungeweza tumia kiasi kidogo cha hela yetu ya ndani kwa kujenga mitambo huko huko Mtwara ukanda wote wa kusini mikoa ya Ruvuma, Mbeya, Iringa na hata Morogoro ikapewa umeme wa uhakika na ule umeme uliokuwa unatumika mikoa hiyo ukaelekezwa Dar. Rais Museven aliwahi kusema katika hatua za kujiletea maendeleo sharti uanze na eneo moja baada ya kukamilisha ndiyo uende sehemu nyingine. Fikiria kama hiyo trilioni 4 ingewekezwa huko huko Mtwara mabadiliko ya wazi yangeweza kuonekana na kwa sababu bado utafiti unaendelea tunaweza kukuta kumbe hata Dar kuna gesi.
 
CCM ishatuona si majinga! Kila kitu Dar na tunachekelea. We ujenge daraja la mabilioni huku sisi hatuna maji ya kunywa. Upuuzi kabisa huu
 
Nijuavyo mimi, hakuna mtu yeyote anayebisha ya kuwa raslimali yeyote ile inayopatikana hapa nchini ni ya watanzania wote katika ujumla wao. Kitu kinachobishaniwa linapokuja ili suala la gasi ya Mtwara ni iwapo kuna ulazima wowote wa kuisafirisha gasi hiyo ikiwa ghafi hadi Dar-es-salaam, ndipo itumike kuzalisha umeme. Kulingana na nadharia ya uwekezaji, viwanda hujengwa ama pale marighafi husika inapokutwa au karibu na soko la bidhaa itakayozalishwa, kutegemea ni kipi kati ya hivyo viwili kuna hafueni ya gharama. Katika suala la gesi ya Mtwara, mimi naona hafueni ya gharama iko katika kuzalisha umeme huko na halafu ukasafirisha umeme huo kwa kutumia "line" ya "gride" ya taifa ambayo tayari ipo. Kwa njia hii itaokoa mabilioni ya fedha itakayotumika kujenga bomba ya kusafirishia gesi hadi Dar.

Inavyoelekea, nchi yetu imekuwa na mazoea ya kutozingatia gharama husika katika maamuzi yake kuhusiana na uwekezaji; ndiyo maana tunaruhusu mchanga wetu wenye madini kubebwu hadi ughaibuni eti kwaajili ya uchambuzi wa madini! Ebu tujiulize kipi rahisi, kuleta mitambo ya kuchambua hayo madini hapa nchini au kusafirisha huo mchanga mpakahuko ughaibuni? Jibu unalo wewe msomaji.

Kwanza napenda kukupongeza mleta uzi huu kwa uzalendo wako,pamoja nakuwa watakuja washabiki wa ''CHAMASUMU'' hapa kuku-tukana na kuku-kebehi lakini wataka usawa haki na maendeleo yenye uwiano na umoja wa kitaifa hatuta-choka kuwatetea watu wa MTWARA na KUSINI KWA UJUMLA,
Mleta mada kaongelea umuhimu wa eneo husika kupewa kipau mbele kwa uendeshwaji na uzalishaji wa zao husika na mahala litakapo tumika,pia kuokoa mzigo wa deni kuuubwa lisilo na msingi hali ya kuwa ni Rahisi mradi huo kujengwa jirani na gesi itokapo badala ya ku-isafirisha mpaka DAR.
Nina uhakika yote hayo viongozi wa serikali na hao wa JANI LA TUMBAKU wanajua hili kwa undani sana ila kwa kuwa wame-la lia 10% zao walizoficha USWIS ndo mana wameshupaa na kushadadia GESI ije DAR pasi na sabubu ya maana na tija zaidi ya kulalama oooh tutaivunja nchi vipande vipande ili mradi tu watishe watu kwa propaganda ''hawana sababu ya msingi hata moja'',mara ooooh umeme ukisafirishwa unapotea njiani,aaaaghvilaza kweli nyie usiposafirishwa utatumikaje nchi nzima?.mtera hausafirishwi!, unapotea kiwango gani?,acheni u-TUPOI
Ki msingi M-TANZANIA yeyote mzalendo anaejali wa-TZ wenzetu waishio MTWARA na kusini kwa ujumla japo kwa robo ya kiwango anacho jijali yeye mwenyewe,hawezi kusapoti suala la kurundika kila kitu DAR na kupelekea mrundikano wa watu hapa,
Sijaona tatizo lolote ikiwa GESI itazalisha umeme MTWARA na ku-unganishwa kwenye GRIDI ya TAIFA.U-taifa utakuwepo na gesi itafaidisha taifa bila utengano wowote,magamba mnao lazimisha kuleta gesi DAR ndo mnataka kuleta mtafaruku wa hujuma za bomba hilo ikiwa litawekwa bila wenyeji kuridhika.mbona kiwanda cha kusindika samaki kipo mwanza karibu na ziwa na hakuna mpasuko? tumewachoka MAFISADI na propaganda zenu na hatudanganyiki.
USHAURI : ni ulele MTWARA......GESI KWANZA vyama baadae,wazalendo wote nchini tuwa unge mkono wana mtwara kwenye sakata hili la mapambano na magamba.
 
"Taarifa kutoka Benki Kuu ya Uswis inaonyesha kuwa makampuni yanayojishughulisha na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi ndiyo walioweka Mabilioni kwenye akaunt za Viongozi waandamizi aka VIGOGO"...Mwisho wa kunukuu...

Vigogo wako kwenye hatua ya utekelezaji kwasasa, deal lilisha ingiwa/pangwa zamani sana...Ukweli mchungu lakini bado utaendelea kusimama maana hata baadhi ya hawa Viongozi wanaotokwa povu kama akina prezzo wanachokililia ni mgao wao tu!...
 
wanaotaka kila kitu kikafanyike dar wanadhan msumbij ni south africa ya zaman na hvo makaburu watatuhujumu maana itakuwa jiran nao.
 
Sera za nchi hii toka uhuru hazijaruhusu sehemu yenye kupatikana malighafi kuendelezwa! Wale vijana wa zamani kama mimi watakumbuka kuwa mji wa Morogoro ulipendelewa sana kwa ujenzi wa viwanda ingawa hawakuwa wazalishaji wakubwa wa malighafi. Viwanda vya ngozi, maturubai, viatu vilijengwa pale ingawa wafugaji wakubwa na walimaji wa pamba wapo ukanda wa Ziwa! Kwa hiyo, hii kasumba inayoendelea hadi leo ya kuwafanya wananchi wa Mtwara na Lindi kuwa wapuuzi na wahaini inatokana na sera hizo za kizamani.(Sina hakika kama tuna sera za nchi kweli!)
 
Naishangaa serikali hii kwani wananchi wa Mtwara siyo watanzania? Tusipoangalia tunaweza kujikuta badala ya kuinua uchumi tunazidi kuuzorotesha kutokana na kujiongezea mzigo wa madeni. Tumeambia hela ya kujenga bomba ni takribani trilioni 4 na huu ni mkopo kutoka benki ya exim ya China. Tungeweza tumia kiasi kidogo cha hela yetu ya ndani kwa kujenga mitambo huko huko Mtwara ukanda wote wa kusini mikoa ya Ruvuma, Mbeya, Iringa na hata Morogoro ikapewa umeme wa uhakika na ule umeme uliokuwa unatumika mikoa hiyo ukaelekezwa Dar. Rais Museven aliwahi kusema katika hatua za kujiletea maendeleo sharti uanze na eneo moja baada ya kukamilisha ndiyo uende sehemu nyingine. Fikiria kama hiyo trilioni 4 ingewekezwa huko huko Mtwara mabadiliko ya wazi yangeweza kuonekana na kwa sababu bado utafiti unaendelea tunaweza kukuta kumbe hata Dar kuna gesi.

Gesi nyingine ipo mkuranga.!!!,hawataki kuizungumzia kabisa.
 
Join Date : 24th October 2010
Posts : 824
Rep Power : 581
Likes Received 26
Likes Given 0

Kwa nini hutoi like kwa wenzio!!!!

Hoja: "Wakazi wa Mtwara wana haki ya kuwa watu wa kwanza kuipata gesi hiyo tena kwa bei nafuu, na pia wana haki ya kupata manufaa mengine yanayotokana na gesi hiyo kama ajira, kuboreshwa kwa miundombinu kabla ya gesi kusafirishwa kwa wengine...maendeleo yanapaswa kuanzia pale zinakopatikana maliasili husika"-Johnson Mbwambo

Hakuna kitufe cha LIKE kwenye mashine yake
 
Nikweli yale uliyofafanua katika mpango mzima wa Gesi mtwara tatizo lipo kwa wenzetu wasiopenda kusikia ukweli ukiwekwa hadharani,nakubaliana na mtoa hoja kwa jinsi alivyokwenda mtwara na kufanya utafiti kidogo dhidi ya wananchi wanachotaka tofauti na upotoshaji unaofanywa na wasiopenda maendeleo ya mikoa ya kusini.
 
Back
Top Bottom