Serikali lazima izuie Ongezeko La Watu!

Serikali lazima izuie Ongezeko La Watu!

Kijakazi

Platinum Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
9,353
Reaction score
15,075
Muda umefika sasa kwa Serikali yetu izuie ongezeko la watu nchini mwetu, ihakikishe tusivuke milioni 45!
Ikiwezekana Wanawake wawezeshwe kwa kupewa vidonge vya kuzuia Mimba kwa wale wenye uwezo wanunue na kwa Wale wasio nao basi kuwe na utaratibu wa kuwapatia (vidonge) bure!

Hili pia linawezekana kwa kuweka kiwango cha Watoto ambao Mwanamke anaweza kuwa nao, mimi nashauri kila Mwanamke asivuke watoto wawili, na atayevukisha hapo basi Baba wa mtoto aadhibiwe kwa kulazimishwa kulipa kodi kubwa zaidi kuliko wengine na pia kutokupandishwa cheo kazini!

Nasema hivi kwa maana hali inatisha sana, sasa hivi nchini mwetu kila Mwanamke analeta Duniani wastani wa Matatizo (watoto) 5.2 hii ni idadi kubwa sana na hatuwezi kuendelea ni hii Hali...

Matokeao yake tunayaona kila mahali kuna mapungufu ya kila kitu nchini mwetu kuanzia Wagonjwa kulala chini mahospitalini, watu wengi kutokuwa na uwezo wa kupata Chakula cha kutosha achilia mbali bora, Kila siku tunazika watu tena wengi wao wamezaliwa miaka ya 1980, hii yote inaletwa na kuwa na mlundiko mkubwa wa Watu na Watu kuendelea kuzaa kama Sungura...
 
Sasa hivi tuko karibu 50 milioni wewe uko 45 milion.
 
Muda umefika sasa kwa Serikali yetu izuie ongezeko la watu nchini mwetu, ihakikishe tusivuke milioni 45!
Ikiwezekana Wanawake wawezeshwe kwa kupewa vidonge vya kuzuia Mimba kwa wale wenye uwezo wanunue na kwa Wale wasio nao basi kuwe na utaratibu wa kuwapatia (vidonge) bure!

Hili pia linawezekana kwa kuweka kiwango cha Watoto ambao Mwanamke anaweza kuwa nao, mimi nashauri kila Mwanamke asivuke watoto wawili, na atayevukisha hapo basi Baba wa mtoto aadhibiwe kwa kulazimishwa kulipa kodi kubwa zaidi kuliko wengine na pia kutokupandishwa cheo kazini!

Nasema hivi kwa maana hali inatisha sana, sasa hivi nchini mwetu kila Mwanamke analeta Duniani wastani wa Matatizo (watoto) 5.2 hii ni idadi kubwa sana na hatuwezi kuendelea ni hii Hali...

Matokeao yake tunayaona kila mahali kuna mapungufu ya kila kitu nchini mwetu kuanzia Wagonjwa kulala chini mahospitalini, watu wengi kutokuwa na uwezo wa kupata Chakula cha kutosha achilia mbali bora, Kila siku tunazika watu tena wengi wao wamezaliwa miaka ya 1980, hii yote inaletwa na kuwa na mlundiko mkubwa wa Watu na Watu kuendelea kuzaa kama Sungura...
Uchumi wa Taifa unakua vizuri matarajio ya hali bora inaongezeka kutokana na kuanza kuzalishwa rasilimali ya gesi. Pili tuna ardhi ya kutosha.Hivyo huo mpango wako ni batili.
 
We akili zako unazijua mwenyewe, ili iweje?
Tanzania kubwa, acha kujifungia ulipo, na ina resources za kulisha nchi hii na majirani zake wote. Sasa sababu nini?
Kama vipi hamia China!
 
Wastani wa matatizo ( mtoto ) .. kwa hio wazee wko kukuzaa ni kosa umekuwa tatizo ? Acha kumezeshwa na wazungu .
 
Wewe ni mtoto wa ngapi kuzaliwa? unajuaje mtoto wa saba ndiye atakuwa waziri au mkuu wa mkoa?
 
Hakyanan hawa wote waliochangia hapo juu wana watoto zaidi ya wawili.(mm naunga mkono hoja ya mleta mada)
 
Muda umefika sasa kwa Serikali yetu izuie ongezeko la watu nchini mwetu, ihakikishe tusivuke milioni 45!
Ikiwezekana Wanawake wawezeshwe kwa kupewa vidonge vya kuzuia Mimba kwa wale wenye uwezo wanunue na kwa Wale wasio nao basi kuwe na utaratibu wa kuwapatia (vidonge) bure!

Hili pia linawezekana kwa kuweka kiwango cha Watoto ambao Mwanamke anaweza kuwa nao, mimi nashauri kila Mwanamke asivuke watoto wawili, na atayevukisha hapo basi Baba wa mtoto aadhibiwe kwa kulazimishwa kulipa kodi kubwa zaidi kuliko wengine na pia kutokupandishwa cheo kazini!

Nasema hivi kwa maana hali inatisha sana, sasa hivi nchini mwetu kila Mwanamke analeta Duniani wastani wa Matatizo (watoto) 5.2 hii ni idadi kubwa sana na hatuwezi kuendelea ni hii Hali...

Matokeao yake tunayaona kila mahali kuna mapungufu ya kila kitu nchini mwetu kuanzia Wagonjwa kulala chini mahospitalini, watu wengi kutokuwa na uwezo wa kupata Chakula cha kutosha achilia mbali bora, Kila siku tunazika watu tena wengi wao wamezaliwa miaka ya 1980, hii yote inaletwa na kuwa na mlundiko mkubwa wa Watu na Watu kuendelea kuzaa kama Sungura...
Acha ujuha wewe nchi hii bado inahitaji nguvu kazi kubwa sana ili kuweza kupata maendeleo na pia kuwa na nguvu ya soko!

Ushauri ni kwamba watoto wazaliwe kwa kuzingatia uzazi wa mpango ili tusiwe na Taifa la wagonjwa wa utapia mlo!!
 
We inaonekana ni mgumba halafu mbinafsi sana,kuna siku ulileta thread humu eti serikali izuie watu wa mikoani wasiingie dar,leo unataka kucontrol watu wasizaliane,kwani population ikiwa kubwa kuna tatizo gani,mbona Nigeria ,U.S.A,Russia,China,wapo wengi na wametuzidi uchumi.
 
I am a center-right conservative so I am against birth control. It's evil and targeted. Suala la kupata watoto ni mapenzi na baraka za Mungu, mwanadamu hana nafasi wala mamlaka ya kuamua kiumbe gani aishi na yupi asiishi. Hizi ni mbinu za watu wa magharibi kusitisha ukuaji wa vizazi vya watu wa dunia ya tatu kwa kuwa wao (magharibi) wamemkaidi Mungu kwa kutotaka kuzaliana kama maandiko yanavyoamrisha. Idadi ya watu wa magharibi inazidi kupungua mwaka hadi mwaka kwa kuwa hawataki kuzaa.

La kujadili ni jinsi ya kuwabana wazazi hapa nchini kwetu kutunza watoto wanaowazaa. Ukipewa watoto na Muumba ni lazima uwatunze na sio kuwa-dump kwa ndugu zako wakutunzie wana wako. Baba au mama hujui watoto wanakula au kuvaa nini halafu unadai uheshimiwe? Haiwezekani. Kama umejaaliwa watoto hata 20 ni vema ili mradi uwatimizie mahitaji yao yote na sio kuwaachia walipa kodi wakubebee zigo lote. My gist being tuache kukumbatia hizi plan za wamagharibi ambazo hazina manufaa kwetu. Ufahari wa mwafrika ni watoto!
 
Acha akili za kuvuta ugolo kijana Nigeria ambayo ina ukubwa wa eneo kama Tanzania inakaribia milioni 200 idadi ya watu. Wewe hutaki watu wazaliane kisa huduma mbovu badala ya kuiambia serikali iache kusamehe makampuni yalipe kodi na viongozi waache kupeleka pesa kwenye mabenki ya Ulaya.

Muda umefika sasa kwa Serikali yetu izuie ongezeko la watu nchini mwetu, ihakikishe tusivuke milioni 45!
Ikiwezekana Wanawake wawezeshwe kwa kupewa vidonge vya kuzuia Mimba kwa wale wenye uwezo wanunue na kwa Wale wasio nao basi kuwe na utaratibu wa kuwapatia (vidonge) bure!

Hili pia linawezekana kwa kuweka kiwango cha Watoto ambao Mwanamke anaweza kuwa nao, mimi nashauri kila Mwanamke asivuke watoto wawili, na atayevukisha hapo basi Baba wa mtoto aadhibiwe kwa kulazimishwa kulipa kodi kubwa zaidi kuliko wengine na pia kutokupandishwa cheo kazini!

Nasema hivi kwa maana hali inatisha sana, sasa hivi nchini mwetu kila Mwanamke analeta Duniani wastani wa Matatizo (watoto) 5.2 hii ni idadi kubwa sana na hatuwezi kuendelea ni hii Hali...

Matokeao yake tunayaona kila mahali kuna mapungufu ya kila kitu nchini mwetu kuanzia Wagonjwa kulala chini mahospitalini, watu wengi kutokuwa na uwezo wa kupata Chakula cha kutosha achilia mbali bora, Kila siku tunazika watu tena wengi wao wamezaliwa miaka ya 1980, hii yote inaletwa na kuwa na mlundiko mkubwa wa Watu na Watu kuendelea kuzaa kama Sungura...
 
Wanaosema tupunguzwe ndio wanaolipa kwao waongezeke..japani na wingi wao sasa wanajitahisi lipa watu waongezeke..population ni power...makamapuni ya ndani yanaweza fanikiwa sana kwa kufanya biashara ndani ,hata na masikini tuu India na China...wametumia sana hiyo faida.Kinachowezekana kubadili kiwango cha mafanikio ni ubora wa hiyo nguvu kazi.....ili wauze nguvu kazi ndani na nje
 
Naunga mkono hoja kwa 100%. Bila kuwa na proper and effective family plan tutaendelea kupiga maktaim na maendeleo tutayasikia kwenye bomba. Hatuwezi kuzaliana hovyo simply tuna ardhi na resources za kutosha. Hata hizo resources itafika muda zitakwisha kutokana na kulemewa na idadi ya watu Ongezeko la ovyo la idadi ya watu ni kikwazo cha maendeleo; ni lazima lidhibitiwe; zile enzi za kila mtoto huja na bahati yake zimepitwa na wakati.

Leo hii kuna "panya road", "watoto wa mbwa", n.k. hayo yote ni matokeo ya ongezeko la watu lisiloendana na uwezo wa wazazi kulea. Leo hii watu wanajizalia ovyo tu bila hata kujua ni kwanini wanazaa. Mkuu nakupongeza kwa hoja murua japo pia mfumo wa nchi yetu una matatizo yake lakini pia uzazi lazima udhibitiwe japo baadhi ya njia ulizopendekeza ni kali mno.
 
Uchumi wa Taifa unakua vizuri matarajio ya hali bora inaongezeka kutokana na kuanza kuzalishwa rasilimali ya gesi. Pili tuna ardhi ya kutosha.Hivyo huo mpango wako ni batili.
nadhani tuanze na kuwapunguza mainterani hamwe kwa sababu kuwa kwao wengi ni kiongeza matatizo kwa taifa hili!
 
Nadhani huyu jamaa atakuwa mkuu wa abortion hapa Tanzania! Gasi,mafuta,madini ya kila namna[gold, diamond, lubi, makaa ya mawe, uranium n.k], mito, bahari, maziwa, misitu, mbuga za wanyama, wanyama wa kufungwa na mazao yake na kadharika wewe unapinga watu kuzaa kwa lipi!???

Lakini pia kama tunaweza uziana bidhaa ndani kwa ndani bila tegemea nje huoni sio mbaya ukichukulia kuwa serikali ya CCM iliua viwanda vyoote na kuwa hatuna haja na exportation???
 
Dah!
Alafu unaweza kukuta ni msomi kabisa na Ofisini au Taasisi aliyopo anategemewa kuwa ndio THINK TANK wa hiyo Tasisis.
kweli WATANZANIA IQ zetu ni chini 60, lakini za huyu ni chini ya 10.
 
Ili nchi iendelee tunahitaji watu, ardhi na siasa bora!(mwalimu nyerere) sasa nikipi kimekosekana hata tuanze kampeni ya kupunguza idadi ya watu? West europe walianza kampeni kama hizo miaka ya 40-50 matokeo yake leo wanahitaji watu wa kujenga nchi zao hakuna mwanamke anaekubali kuzaa! Wake kwa wake wanapandana na waume kwa waume! Sasa hapo kuna watoto kweli watakuja?
 
Back
Top Bottom