Mimi nampongeza mtoa hoja kwaani tukiendelea na hoja ya kila mtoto huja na bahati yake Taifa halitafika popote na tutabaki kuwalaumu wanasiasa bure. Embu jiulize mtu masikini wa kawaida anakuwa na watoto watano je, ataweza kuwahudumia ipasavyo? Ukizingatia saivi kila huduma mwananchi anatakiwa kuchangia, iwe Elimu, Afya na nyingine nyingi. Kuna wengine wanatumia mfano wa china, Urusi na Marekani kuwa zina idadi kubwa ya watu lakini wako juu kimaendeleo lakini wanasahau kuwa nchi zote hizo zina wastani wa chini ya watoto 2 kwa kila mwanamke. Analia nchi yoyote yenye uchumi angalau wa kati kama itakuwa na wastan wa zaidi wa watoto watutu kwa kila mwanamke. Kwakweli tunahitaji kubadilika!