juve2012
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 3,343
- 2,040
Problem-Reaction-Solution.
Hii ndio mbinu ya kijasusi inayotumiwa na serikali nyingi duniani pale kunapotokea jambo lisilowapendeza kwenye jamii.Watatumia mamluki wao kujipenyeza ndani ya jamii,waligeuze jambo hilo kuwa na sura mbaya,halafu watu wakililalamikia,serikali inachukulia advantage malalamiko hayo kuchukua hatua ambazo ndio hasa ilikuwa lengo,na hatua hizi mara nyingi huwa sheria kali au marufuku.
Ndio maana kwenye legal ethics inasemwa kuwa si hekima kutunga sheria kwa kuendeshwa na matukio ya mwanzo.Leo limetokea hili,mmetunga,kesho lile,mmetunga,no,ni vema kuyahukumu mambo kwa sheria zilizopo au kutunga sheria mpya baada ya kujiridhisha na kiini cha matatizo husika ni kipi.
Na sheria zilizopo hazizuii mijadala kama hii yenye tija.
Nadhani sheria zilizopo zinatoa fursa kuwadhibiti wafanya fujo.
Mijadala hii ya katiba ni jambo la maana,watu wanaelimishwa,hauwezi kuipiga marufuku,wala hakuna ushahidi kuwa wanaoiandaa wana lengo la kuleta fujo.
Baadhi ya watu ndio wanataka kuigeuza kuwa fujo,na watu hao hawahusiki kuiandaa,watafutwe,sheria zilizopo ziwashughulikie kama wahalifu.Suala si kupiga marufuku mijadala hii,au kuwazuia akina Warioba wasielimishe watu,bali suala ni kuwakamata hawa wahuni kama huyo "konda" wa Lumumba na wahuni wenzie wapelekwe kwenye sheria.
Asipochukuliwa hatua huyu na wahuni wenzie,basi ni wazi katumwa kazi hiyo ya problem,reaction,solution,na utakuwa mwendelezo tu wa zile fujo za pale bungeni(ili watu waone bunge halifai,bahati mbaya Ukawa wakastukia chezo,wakatoka,mbinu ikawa chungu manake bunge likaonekana la ovyo bila Ukawa),kwenye mikutano ya vyama n.k.
Hii nchi inaongozwa kimafia sana.Watu hawajui tu.
Hii ndio mbinu ya kijasusi inayotumiwa na serikali nyingi duniani pale kunapotokea jambo lisilowapendeza kwenye jamii.Watatumia mamluki wao kujipenyeza ndani ya jamii,waligeuze jambo hilo kuwa na sura mbaya,halafu watu wakililalamikia,serikali inachukulia advantage malalamiko hayo kuchukua hatua ambazo ndio hasa ilikuwa lengo,na hatua hizi mara nyingi huwa sheria kali au marufuku.
Ndio maana kwenye legal ethics inasemwa kuwa si hekima kutunga sheria kwa kuendeshwa na matukio ya mwanzo.Leo limetokea hili,mmetunga,kesho lile,mmetunga,no,ni vema kuyahukumu mambo kwa sheria zilizopo au kutunga sheria mpya baada ya kujiridhisha na kiini cha matatizo husika ni kipi.
Na sheria zilizopo hazizuii mijadala kama hii yenye tija.
Nadhani sheria zilizopo zinatoa fursa kuwadhibiti wafanya fujo.
Mijadala hii ya katiba ni jambo la maana,watu wanaelimishwa,hauwezi kuipiga marufuku,wala hakuna ushahidi kuwa wanaoiandaa wana lengo la kuleta fujo.
Baadhi ya watu ndio wanataka kuigeuza kuwa fujo,na watu hao hawahusiki kuiandaa,watafutwe,sheria zilizopo ziwashughulikie kama wahalifu.Suala si kupiga marufuku mijadala hii,au kuwazuia akina Warioba wasielimishe watu,bali suala ni kuwakamata hawa wahuni kama huyo "konda" wa Lumumba na wahuni wenzie wapelekwe kwenye sheria.
Asipochukuliwa hatua huyu na wahuni wenzie,basi ni wazi katumwa kazi hiyo ya problem,reaction,solution,na utakuwa mwendelezo tu wa zile fujo za pale bungeni(ili watu waone bunge halifai,bahati mbaya Ukawa wakastukia chezo,wakatoka,mbinu ikawa chungu manake bunge likaonekana la ovyo bila Ukawa),kwenye mikutano ya vyama n.k.
Hii nchi inaongozwa kimafia sana.Watu hawajui tu.