Kama kwa umeme huu hawawezi kuzalisha kwa bei ya tija, wa nje waruhusiwe tu.Kwa umeme huu watashindana vipi bila kuwabeba labda waambiwe wafunge viwanda! Au serikali ipunguze makodi tuu!
Lawama zote kwa January Makamba kuchezea nishati ya umeme na majaribio yake ya ajabu pale TANESCO.Kwa umeme huu watashindana vipi bila kuwabeba labda waambiwe wafunge viwanda! Au serikali ipunguze makodi tuu!
Maji na Umeme nazo tupunguze matumizi kisa nchi imeshindwa upatikanaji wake? Unakuaje ndugu yangu kwa kufikiri?Wananchi wapunguze matumizi ya sukari.
Waziri yuko sahihi wamelondwa vya kutosha, wameshindwa kutumia fursa, acha washindane.Waziri Bashe akiwa Ikulu, Dar ameongelea sakata la sukari nchini.
Bashe: Wafanyabiashara wana option mbili tu, waache kuuza sukari, Serikali itatafuta option nyingine. Wenye viwanda wana option mbili, wafate utaratibu wa Serikali au waache hii kazi.
Serikali haiwezi kuruhusu, tumewaprotect vya kutosha kama nchi lakini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu mwezi wa sita kwenye Bunge la bajeti kama waziri mwenye dhamana ninapeleka mabadiliko ya sheria kwaajili ya ku libelarize biashara ya sukari, wata- compete na competing companies kutoka nje na wenyewe watapata incentives zilizo ndani ili kuwaprotect.
Hatuwezi kuendelea na irresponsible private sector kwenye nchi kwa hali hii inayoendelea. Wakulima wa miwa wako 12,500 nchini, tutasota mwaka mmoja, mabonde yale tutayageuza ya mpunga, there is no problem.. zipo nchi ambazo zimeacha kulima sukari.
Magine watu wamepewa tenda kuagiza tani elfu 10..wanaagizi buku moja tu..majizi ya mwendo kasi.SUKARI inaweza ikatoka Brazil mbali Huko na still tukainunua kwa sh 2000 kilo MOJA.believe it or not.hakuna haja ya kuprotect majizi.
Kwa akili kama hiz, watanzania na Afrika Kwa ujumla tuna safari ndefu sana.Magufuli alikuwa mshamba asiyeelewa uchumi na hiyo solution yake ilikuwa ya kishamba. Huyu ndiye aliyeingusha biashara ya korosho akaiharibu, alitaka wanajeshi wabangue korosho hata kwa meno. Ujinga mtupu.
Magufuli alikuwa kama mtu mwenye nyundo ambaye tatizo lolote anaona kulitatua ni kulipiga nyundo.
Nakwambia hivi, serikali haiwezi kutatua suala la bei kwa kutumia nguvu, serikali inatakiwa kutumia akili zaidi ya nguvu.
Magufuli alikuwa anatumia nguvu zaidi ya akili.
Kutumia nguvu zaidi ya akili ndiyo hizo habari za msako wa walanguzi. Hizo habari tumezifanya tangu enzi za Sokoine na hazijawahi kufanikiwa. Ni maigizo ya kuchota akili watu wajinga wasioelewa uchumi tu.
Kutumia akili zaidi ya nguvu ni kuziachia nguvu za supply and demand zipange bei zenyewe, kwa fair competition.
Hiki ndicho Bashe anasema anaenda kufanya.
Kwa akili kama hiz, watanzania na Afrika Kwa ujumla tuna safari ndefu sana.
Utumie akili kupambana na watu wanaokudidimiza Kwa makusudi? Wewe utakua rais au mtumwa wao?
Hiyo akili wananchi watasubilia wakiumia Hadi Lin?
Hao wenyewe hawana akili unayoiwaza wewe?
Intelligence ya wafanyabiàshara ni kubwa. Hata huko mnakokwenda kununua sukari nje wanaweza Fanya mtanzania yoyete anujue Kwa bei juu Ili bei hapa nchin isishuke. Wanamuungano na sio mtengamano.
Vibari vya kuagiza sukari vinatoka Kwa masharti Gani, unayajua? Hivyo vibari havitoki kiholera, ni deal za watu. Usipoweka asilimia yao hupati kibali.
Unashangilia Kwa wenzako kutengeneza mianya ya kupiga pesa duuhh.
Hatari sana.
Mzigo wa kwanza ni KIZIMKAZI.Huyu waziri ni mzigo
Naunga mkono hoja ,najua amemueleza mama akampa go ahead.Waziri Bashe akiwa Ikulu, Dar ameongelea sakata la sukari nchini.
Bashe: Wafanyabiashara wana option mbili tu, waache kuuza sukari, Serikali itatafuta option nyingine. Wenye viwanda wana option mbili, wafate utaratibu wa Serikali au waache hii kazi.
Serikali haiwezi kuruhusu, tumewaprotect vya kutosha kama nchi lakini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu mwezi wa sita kwenye Bunge la bajeti kama waziri mwenye dhamana ninapeleka mabadiliko ya sheria kwaajili ya ku libelarize biashara ya sukari, wata- compete na competing companies kutoka nje na wenyewe watapata incentives zilizo ndani ili kuwaprotect.
Hatuwezi kuendelea na irresponsible private sector kwenye nchi kwa hali hii inayoendelea. Wakulima wa miwa wako 12,500 nchini, tutasota mwaka mmoja, mabonde yale tutayageuza ya mpunga, there is no problem.. zipo nchi ambazo zimeacha kulima sukari.
Sasa manake nini?Si kwamba waziri anataka kuiua sekta fulani.
Waziri anawaambia watu wa kwenye hiyo sekta waache kupenda kubebwa na protectionism, ni muda kwa kushindana na bei ya sukari kutoka nje.
Waliosoma uchumi wanajua kitu kinaitwa "competitive advantage".
Anachosema Bashe ni kwamba, kama Tanzania hatuna competitive advantage katika sukari, sukari yetu ina gharama ya juu zaidi kuizalisha, tuseme labda tunazalisha kilo moja kwa shilingi 6,000, wakati wenzetu wanaweza kuzalisha kilo hiyo kwa shilingi 3,000, hapo labda inawezekana ikawa busara kuacha kuzalisha sukari, tuagize ya nje, na hiyo ardhi ya kulima sukari tulime mpunga.
Hapo hatuna "competitive advantage" katika kutengeneza sukari.
Kauli hii pia inaweza kuwa silaha ya kisiasa, kwa mfano, ikiwa waziri anajua kuwa wafanyabiashara wa sukari wanapandisha bei kwa hila, na wanaweza kabisa kupunguza bei ikawa sawa na ile ya sukari kutoka nje ya shilingi 3,000 , kwa kupunguza gharama za uzalishaji na kuondoa upandishaji bei wa kiholela wa kutafuta faida tu, kauli hii inaweza kutumika kulazimisha wadau wa sekta ya sukari kupunguza bei.
Bei ya sukari Tanzania haipo juu naturally, ipo juu artificially. Ndiyo maana sukari ya nchi jirani kama Malawi bei yake iko chini zaidi.
Serikali inafanya kitu sahihi kuruhusu sukari ya nje ije kushindana na ya ndani kwenye soko.
Hili jambo lilitakiwa kufanyika zamani sana. Naona kama wamechelewa.
Tatizo si uwezo wa nchi kuzalisha sukari, hilo lingekuwa tatizo, kuongeza uzalishaji wa sukari kama ulivyosema, kungeweza kutatua hilo tatizo.Sasa manake nini?
Kwani hiyo sukari inayotegemewa kuingizwa si inalimwa au inazalishwa viwandani?
Kwangu mimi ingekuwa vyema waziri wa Kilimo angejitanabahi Kwa Kuongeza uzalishaji wa miwa na utengenezaji wa sukari.
Hivi mahela ya serikali aliyotumia kuwaweka vijana wa mjini wa ccm makambini eti kuwafundisha Kilimo hela yote hiyo iliyotumika kufanya huo upumbavu ingeelekezwa yote Kwenye kuongeza uzalishaji wa sukari tungekuwa tumefanya la maana kama nchi yenyewe yakaona ni kheri yatengeneze kamfumo( Big nini sijui) wazile wana ccm wengi kidogokidogo.
Seriously kabisa waziri anakomalia kwenda kufuta Sheria inayowalinda wazalishaji miwa wa ndani ili kuruhusu sukari inayotengenezwa nje kuingizwa nchini.
Mabonde yote tuliyonayo waziri ameshindwa kueleza namna ya kuboresha Kilimo cha miwa .
Kwa hiyo nilivyokuelewa kwamba tatizo sio uzalishaji wa ndani wa sukari Bali tatizo ni wafanyabiashara ambo kuwadhibiti ndio kama alivyoelekeza waziri kuagiza sukari kutoka nje.Tatizo si uwezo wa nchi kuzalisha sukari, hilo lingekuwa tatizo, kuongeza uzalishaji wa sukari kama ulivyosema, kungeweza kutatua hilo tatizo.
Tatizo ni wafanyabiashara wa sukari ku manipulate supply ya sukari, kutengeneza uhaba makusudi ili bei ipande.
Na tatizo hili linatatuliwa na serikali kuruhusu sukari kutoka nje iingie Tanzania bila vikwazo.
Wafanyabiashara wa ndani wakileta janja zao ku manipulate supply, hata wewe uweze kwenda Malawi na Zambia kuleta sukari ya huko ya bei nafuu na kupata faida.
Usichoelewa ni kipi hapo?
Naam.Kwa hiyo nilivyokuelewa kwamba tatizo sio uzalishaji wa ndani wa sukari Bali tatizo ni wafanyabiashara ambo kuwadhibiti ndio kama alivyoelekeza waziri kuagiza sukari kutoka nje.
Ndio hivyo au?