Serikali kununua vitu vya mitumba Sheria/Katiba inasemaje?

MWALLA

JF-Expert Member
Dec 12, 2006
16,992
10,497
WAFANYAKAZI wa Kampuni ya Reli (TRL) wanaupinga mpango wa serikali wa kununua mitambo chakavu ya mwekezaji kutoka India ambayo ilikodishwa kwa ajili ya kusaidia kupunguza tatizo la usafiri.

Kampuni ya Reli ya India (Rites), ambayo ni mwekezaji mwenye asilimia 51 za hisa za TRL, iliagiza mabehewa 23 na injini tano kutoka India kwa ajili ya kuyakodisha, lakini wafanyakazi walidai kuwa ni mitumba na yanaisababishia kampuni hasara kubwa.

Akizungumza na wafanyakazi hao jana wakati wa kikao cha pamoja jijini Dar es Salaam, katibu mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu), Sylvester Rwegasira alisema hawawezi kukubaliana na serikali katika suala hilo kwa sababu wao ndio wategemizi namba moja wa reli hiyo.

“Hatuwezi kukubaliana na uamuzi wa serikali wa kununua injini chakavu na mabehewa hayo kwa sababu havina ubora na havifai kwa matumizi ya nchi hii,” alisema Rwegasira. Alisema serikali ikishikilia msimamo huo wa kununua injini hizo pamoja na mabehewa, wafanyakazi hawatakuwa tayari kuzitumia na badala yake watalazimika kuacha kazi.

“Serikali inaendelea na mchakato huu na hadi hivi sasa kuna timu ya watu watatu kutoka Dar es Salaam, Morogoro na Tabora kwa ajili ya kukagua njini hizo,” alisema Rwegasira. “Ili kuona kama zitafaa kwa matumizi na hatimaye serikali ilipe fedha hizo wakati kuna tarifa mbalimbali zimeshatolewa kuhusu ubovu wa injini hizo pamoja na mabehewa lakini hazijafanyiwa kazi hadi hivi sasa,” alisema Fortunatus Chiliko.

Chiliko alisema Mamlaka Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra) ilisimamisha mabehewa hayo kwa sababu ya ubovu kabla ya Rites kuzuia matumizi yake ikidai ilipwe fedha zake za kukodishia injini na mabehewa hayo, leo hii Rites hiyo hiyo iko tayari kuuza kwa sababu wanatambua kuwa haviwezi kufanyakazi tena. Katika hatua nyingine Rwegasira alisema wafanyakazi pia wanaitaka serikali kuiondoa menejimenti iliyowekwa na Rites kwa sababu tayari kuna uongozi wa mpito ulio chini ya wazawa
 
Nimeuliza hivi kutokana na hili suala la serikali ya CCM kuendelea na utaratibu huu tangu kipindi cha uuzwaji wa TRC kwenda TRL hali inaonyesha kuwa utaratibu huu wa manunuzi ya vifaa kwaajili ya uendeshaji shughuli za nchi wa kununua vitu vilivyotumika MITUMBA yaonyesha huu si utaratibu mzuri na ndio maana nimeonelea turudi kwenye KATIBA na SHERIA zetu je hili suala la ununuzi wa vitu vya mitumba yaani vilivyotumika je ni sahihi na kwanini isiwezekane kununua vitu VIPYA?
 
KATIBA GANI?KAMA NI KATIBA HII ITAKUWA INARUHUSU MBONA MAGUFULI ALINUNUA YALE MAPANGA BOI CASH NA KATIBA ILITULIA KIMYAA
 
FkbPw3CWQAAN7mF

nani anaeruhusu upjinga huu?

 
pamoja na kusifia na kusema amenunua mitumba lkn kinachoonekana bei iliyonunua mitumba hiyo si bei ya MITUMBA ni bei ya mabehewa mapya lkn tumeletewa MITUMBA... kwa kweli hii NNJI haijapata kutokea duniani NNJI kama hii ya TANGANYIKA
 
Back
Top Bottom