Serikali kukomesha kizuri cha Mabenki ya Biashara

Izack Mwanahapa

JF-Expert Member
Apr 21, 2011
497
236
HONGERA SERIKALI KWA JITIHADA ZA KUMALIZA KIBURI CHA MABENKI YA BIASHARA

Hatua ya Serikali kuhamishia fedha zake zote kutoka kwenye mabenki ya kibiashara inatajwa kuwa inalenga kumaliza kiburi na mikogo ya MABENKI ya biashara dhidi ya wafanyabiashara na wajasiriamali wa kawaida.

Tanzania inatajwa kuwa moja kati ya nchi zenye mabenki mengi lakini inakadiriwa kwamba ni asilimia ishirini tu ya wananchi wake ndio wananufaika na huduma za kibenki japo kuwa fedha zao za kodi kupitia mashirika mbalimbali ya umma ndizo zinazoendeleza mabenki hayo. Kwa sasa Tanzania ina mabenki yapatayo 52.

Kutokana na Serikali na taasisi zake kuweka fedha zake na kufanya miamala mikubwa na mabenki ya kibiashara baadhi ya benki zilijiziuka sana na kuanza kupuuza wafanyabiashara na wajasiriamali wa kawaida wanaohitaji kufanya biashara na benki hizo kutokana na benki hizo kuwa na uwezo wa kujiendesha kwa miamala ya Serikali pekee hivyo wateja wengine kuonekana kama ZIADA.

Hatua ya Serikali kuhamisha fedha zake kutoka kwenye mabenki hayo na kuzielekeza BOT itazilazimisha benki za biashara kurejesha heshima kwa wateja wake (wafanyabiashara/wajasiriamali) wa kawaida ili waweze kujiendesha kwani hakuna namna tena ya kujinufaisha na kujiendesha kwa fedha za Serikali na taasisi zake.

Kwa muda mrefu kumekuwa na urasimu mkubwa kwa mabenki kutokuwa tayari kuelekeza nguvu katika kuwawezesha wajasiriamali wa kawaida kwa kigezo kwamba HAWAKOPESHEKI kwakuwa si walipaji wazuri. Sasa ni wakati wa mabenki kutenga fungu la elimu kwa umma waelimishe wateja wao wa kawaida ili wakopesheke na si kuwakimbia kama walivyokuwa wakifanya Mwanzo kwani kila linalotokea linasababu ya kutokea.

Ni wazi kwamba kutokopesheka kwa watanzania walio wengi kunatokana na kukosa uelewa kuhusu masuala ya kifedha, katika karne ya sasa mabenki yetu yanapaswa kubadilika na kuanza kufanya Business Development Services (BDS) ya mara kwa mara kwa wateja wake badala ya kukaa tu wakisubiri kuuza dhamana baada ya mtu kushindwa kurejesha mkopo. Vikwazo vingi vya kibiashara vinavyomkwamisha mtu/watu kulipa mikopo kwa wakati vinaweza kuepukika ikiwa mabenki yataamua kuwekeza kwenye elimu ya biashara kwa wateja wake.

Hatua hii haimaanishi kwamba sasa ni wakati wa neema kwa wananchi kukopa tu hata kama huna shughuli au kukopa kwa matumizi ambayo si ya kibiashara la hasha! Wananchi wajasiriamali tunapaswa kubadilika pia ili kuunga mkono jitihada za Serikali kwa sisi wenyewe kujitengenezea mazingira ya kuaminika na kukopesheka.

Mabenki pia yanapaswa kuanza kudhamini mawazo mazuri ya kibiashara kama hatua ya msingi. Wasomi wengi katika nchi yetu wanashindwa kuendelea kwasababu ya kukosa mitaji, wanamawazo bunifu mazuri ambayo yakitekelezwa yanaweza kuleta tija katika nchi lakini kwakuwa mabenki yetu hayathamini mawazo (ideas) nzuri za kibiashara badala yake inadhamini hati za nyumba, viwanja, mashamba na magari basi ni wazi ndoto za wasomi wachanga wanaochipukia katika ujasiriamali haziwezi kutimia na ndio maana wanakimbilia siasa.

Mabenki yetu yanapaswa kubadilika ili kuendana na hali halisi ya maisha ya watanzania, uwekezaji mkubwa unatakiwa kufanyika katika kuanzisha na kuendeleza biashara mpya bunifu, zitakazozalisha ajira mpya kwa wingi kwa vijana wa Taifa hili vinginevyo tutakuwa na kundi kubwa la wasomi mizigo ambao asilimia 90 ya taaluma yao itatumika kukosoa na kuhujumu maendeleo ya watu wengine baada ya wao kukosa kazi na fursa za kujiendeleza katika nchi yao.

Nchi nyingi zilizoendelea zilidhamini mawazo na ubunifu wa wataalam wake katika uvumbuzi na uendeshaji wa mambo mbalimbali ya kibiashara. Hakuna sababu ya kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi katika vyuo mbalimbali kama wote wanategemea kuajiriwa na si kutengeneza ajira kwao na kwa wengine pia.

Izack Mwanahapa
 
HONGERA SERIKALI KWA JITIHADA ZA KUMALIZA KIBURI CHA MABENKI YA BIASHARA

Hatua ya Serikali kuhamishia fedha zake zote kutoka kwenye mabenki ya kibiashara inatajwa kuwa inalenga kumaliza kiburi na mikogo ya MABENKI ya biashara dhidi ya wafanyabiashara na wajasiriamali wa kawaida.

Tanzania inatajwa kuwa moja kati ya nchi zenye mabenki mengi lakini inakadiriwa kwamba ni asilimia ishirini tu ya wananchi wake ndio wananufaika na huduma za kibenki japo kuwa fedha zao za kodi kupitia mashirika mbalimbali ya umma ndizo zinazoendeleza mabenki hayo. Kwa sasa Tanzania ina mabenki yapatayo 52.

Kutokana na Serikali na taasisi zake kuweka fedha zake na kufanya miamala mikubwa na mabenki ya kibiashara baadhi ya benki zilijiziuka sana na kuanza kupuuza wafanyabiashara na wajasiriamali wa kawaida wanaohitaji kufanya biashara na benki hizo kutokana na benki hizo kuwa na uwezo wa kujiendesha kwa miamala ya Serikali pekee hivyo wateja wengine kuonekana kama ZIADA.

Hatua ya Serikali kuhamisha fedha zake kutoka kwenye mabenki hayo na kuzielekeza BOT itazilazimisha benki za biashara kurejesha heshima kwa wateja wake (wafanyabiashara/wajasiriamali) wa kawaida ili waweze kujiendesha kwani hakuna namna tena ya kujinufaisha na kujiendesha kwa fedha za Serikali na taasisi zake.

Kwa muda mrefu kumekuwa na urasimu mkubwa kwa mabenki kutokuwa tayari kuelekeza nguvu katika kuwawezesha wajasiriamali wa kawaida kwa kigezo kwamba HAWAKOPESHEKI kwakuwa si walipaji wazuri. Sasa ni wakati wa mabenki kutenga fungu la elimu kwa umma waelimishe wateja wao wa kawaida ili wakopesheke na si kuwakimbia kama walivyokuwa wakifanya Mwanzo kwani kila linalotokea linasababu ya kutokea.

Ni wazi kwamba kutokopesheka kwa watanzania walio wengi kunatokana na kukosa uelewa kuhusu masuala ya kifedha, katika karne ya sasa mabenki yetu yanapaswa kubadilika na kuanza kufanya Business Development Services (BDS) ya mara kwa mara kwa wateja wake badala ya kukaa tu wakisubiri kuuza dhamana baada ya mtu kushindwa kurejesha mkopo. Vikwazo vingi vya kibiashara vinavyomkwamisha mtu/watu kulipa mikopo kwa wakati vinaweza kuepukika ikiwa mabenki yataamua kuwekeza kwenye elimu ya biashara kwa wateja wake.

Hatua hii haimaanishi kwamba sasa ni wakati wa neema kwa wananchi kukopa tu hata kama huna shughuli au kukopa kwa matumizi ambayo si ya kibiashara la hasha! Wananchi wajasiriamali tunapaswa kubadilika pia ili kuunga mkono jitihada za Serikali kwa sisi wenyewe kujitengenezea mazingira ya kuaminika na kukopesheka.

Mabenki pia yanapaswa kuanza kudhamini mawazo mazuri ya kibiashara kama hatua ya msingi. Wasomi wengi katika nchi yetu wanashindwa kuendelea kwasababu ya kukosa mitaji, wanamawazo bunifu mazuri ambayo yakitekelezwa yanaweza kuleta tija katika nchi lakini kwakuwa mabenki yetu hayathamini mawazo (ideas) nzuri za kibiashara badala yake inadhamini hati za nyumba, viwanja, mashamba na magari basi ni wazi ndoto za wasomi wachanga wanaochipukia katika ujasiriamali haziwezi kutimia na ndio maana wanakimbilia siasa.

Mabenki yetu yanapaswa kubadilika ili kuendana na hali halisi ya maisha ya watanzania, uwekezaji mkubwa unatakiwa kufanyika katika kuanzisha na kuendeleza biashara mpya bunifu, zitakazozalisha ajira mpya kwa wingi kwa vijana wa Taifa hili vinginevyo tutakuwa na kundi kubwa la wasomi mizigo ambao asilimia 90 ya taaluma yao itatumika kukosoa na kuhujumu maendeleo ya watu wengine baada ya wao kukosa kazi na fursa za kujiendeleza katika nchi syyao.

Nchi nyingi zilizoendelea zilidhamini mawazo na ubunifu wa wataalam wake katika uvumbuzi na uendeshaji wa mambo mbalimbali ya kibiashara. Hakuna sababu ya kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi katika vyuo mbalimbali kama wote wanategemea kuajiriwa na si kutengeneza ajira kwao na kwa wengine pia.

Izack Mwanahapa
 
Nadhani hauko updated,

Tayari serikali imekubaliana na mabenk hayo kutokuondoa mapesa yako huko... hivyo hii yako ni furaha ya swala kumtoroka Chui wakati mbele yake kuna Simba..!! Pole

BACK TANGANYIKA
 
Nadhani hauko updated,

Tayari serikali imekubaliana na mabenk hayo kutokuondoa mapesa yako huko... hivyo hii yako ni furaha ya swala kumtoroka Chui wakati mbele yake kuna Simba..!! Pole

BACK TANGANYIKA
Dah! hatari sana hii. Waraka huo wa kusitisha umetolewa wapa na lini ?
 
HONGERA SERIKALI KWA JITIHADA ZA KUMALIZA KIBURI CHA MABENKI YA BIASHARA

Hatua ya Serikali kuhamishia fedha zake zote kutoka kwenye mabenki ya kibiashara inatajwa kuwa inalenga kumaliza kiburi na mikogo ya MABENKI ya biashara dhidi ya wafanyabiashara na wajasiriamali wa kawaida.

Tanzania inatajwa kuwa moja kati ya nchi zenye mabenki mengi lakini inakadiriwa kwamba ni asilimia ishirini tu ya wananchi wake ndio wananufaika na huduma za kibenki japo kuwa fedha zao za kodi kupitia mashirika mbalimbali ya umma ndizo zinazoendeleza mabenki hayo. Kwa sasa Tanzania ina mabenki yapatayo 52.

Kutokana na Serikali na taasisi zake kuweka fedha zake na kufanya miamala mikubwa na mabenki ya kibiashara baadhi ya benki zilijiziuka sana na kuanza kupuuza wafanyabiashara na wajasiriamali wa kawaida wanaohitaji kufanya biashara na benki hizo kutokana na benki hizo kuwa na uwezo wa kujiendesha kwa miamala ya Serikali pekee hivyo wateja wengine kuonekana kama ZIADA.

Hatua ya Serikali kuhamisha fedha zake kutoka kwenye mabenki hayo na kuzielekeza BOT itazilazimisha benki za biashara kurejesha heshima kwa wateja wake (wafanyabiashara/wajasiriamali) wa kawaida ili waweze kujiendesha kwani hakuna namna tena ya kujinufaisha na kujiendesha kwa fedha za Serikali na taasisi zake.

Kwa muda mrefu kumekuwa na urasimu mkubwa kwa mabenki kutokuwa tayari kuelekeza nguvu katika kuwawezesha wajasiriamali wa kawaida kwa kigezo kwamba HAWAKOPESHEKI kwakuwa si walipaji wazuri. Sasa ni wakati wa mabenki kutenga fungu la elimu kwa umma waelimishe wateja wao wa kawaida ili wakopesheke na si kuwakimbia kama walivyokuwa wakifanya Mwanzo kwani kila linalotokea linasababu ya kutokea.

Ni wazi kwamba kutokopesheka kwa watanzania walio wengi kunatokana na kukosa uelewa kuhusu masuala ya kifedha, katika karne ya sasa mabenki yetu yanapaswa kubadilika na kuanza kufanya Business Development Services (BDS) ya mara kwa mara kwa wateja wake badala ya kukaa tu wakisubiri kuuza dhamana baada ya mtu kushindwa kurejesha mkopo. Vikwazo vingi vya kibiashara vinavyomkwamisha mtu/watu kulipa mikopo kwa wakati vinaweza kuepukika ikiwa mabenki yataamua kuwekeza kwenye elimu ya biashara kwa wateja wake.

Hatua hii haimaanishi kwamba sasa ni wakati wa neema kwa wananchi kukopa tu hata kama huna shughuli au kukopa kwa matumizi ambayo si ya kibiashara la hasha! Wananchi wajasiriamali tunapaswa kubadilika pia ili kuunga mkono jitihada za Serikali kwa sisi wenyewe kujitengenezea mazingira ya kuaminika na kukopesheka.

Mabenki pia yanapaswa kuanza kudhamini mawazo mazuri ya kibiashara kama hatua ya msingi. Wasomi wengi katika nchi yetu wanashindwa kuendelea kwasababu ya kukosa mitaji, wanamawazo bunifu mazuri ambayo yakitekelezwa yanaweza kuleta tija katika nchi lakini kwakuwa mabenki yetu hayathamini mawazo (ideas) nzuri za kibiashara badala yake inadhamini hati za nyumba, viwanja, mashamba na magari basi ni wazi ndoto za wasomi wachanga wanaochipukia katika ujasiriamali haziwezi kutimia na ndio maana wanakimbilia siasa.

Mabenki yetu yanapaswa kubadilika ili kuendana na hali halisi ya maisha ya watanzania, uwekezaji mkubwa unatakiwa kufanyika katika kuanzisha na kuendeleza biashara mpya bunifu, zitakazozalisha ajira mpya kwa wingi kwa vijana wa Taifa hili vinginevyo tutakuwa na kundi kubwa la wasomi mizigo ambao asilimia 90 ya taaluma yao itatumika kukosoa na kuhujumu maendeleo ya watu wengine baada ya wao kukosa kazi na fursa za kujiendeleza katika nchi yao.

Nchi nyingi zilizoendelea zilidhamini mawazo na ubunifu wa wataalam wake katika uvumbuzi na uendeshaji wa mambo mbalimbali ya kibiashara. Hakuna sababu ya kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi katika vyuo mbalimbali kama wote wanategemea kuajiriwa na si kutengeneza ajira kwao na kwa wengine pia.

Izack Mwanahapa
Hongera sana Mwanahapa kwa analysis yako. Binafsi nikuambie tu kwanza kwa ninachokijua hilo halipo tena, fedha za serikali zitaendelea kuwekwa kwenye commercial banks kama kawaida.
Lingine,hata kama ingetokea hivyo, mimi nilifikiri ungepiga kelele kwamba hizo fedha za serikali kuliko kuwekwa benki kuuzingewekwa benki ya postaambayo inamilikiwa kwa asilimia 100 na serikali na hapo ndo wajasiriamali na wafanya biashara wakapewe mikopo huko.
Mabenki private kaka hayajaja nchini kufurahisha watanzania,yamekuja kufanya biashara yenye faida! Hayawezi kukopesha hata watu wasiokopesheka na kamwe hayataweza kufanya hizo BDS unless mkopaji mwenyewe alipie hizo ghalama. Tuwalaumu waliouza NBC naona hawakuliona hilo na ingekuwa vizuri kwa serikali kuwa na commercial bank yake na kuwa na vitengo vya BDS ingawa nayo inahitaji nguvu ya ziada maana NBC hivyo vitengo vilikuwepo na hao hao ndo walishirikiana na wakopaji kuzamisha mikopo!
Kaka hili linahitaji deep thinking na si kama unavyofikiri.
Kwa wajasiriamali wadogo kiukweli ni vigumu kukopesheka. Kuna benki moja inaitwa Access inadeal sana na wajasiriamali wadogo wadogo kama unafuatilia mienendo ya mabenki nafikiri unajua kinachoendelea. Yani hao hao wajasiriamali unaowasema hadi huwa wanakimbia sehemu zao za biashara kwa ajili ya kudaiwa! Mabenki makubwa huwa yanaona heri kukopesha only one big fish na kuhangaika na mmoja ambaye anawaingizia faida kubwa kuliko kudeal na mikopo mia mbili na vikamisheni haba.
 
Nadhani hauko updated,

Tayari serikali imekubaliana na mabenk hayo kutokuondoa mapesa yako huko... hivyo hii yako ni furaha ya swala kumtoroka Chui wakati mbele yake kuna Simba..!! Pole

BACK TANGANYIKA
Nadhani hauko updated,

Tayari serikali imekubaliana na mabenk hayo kutokuondoa mapesa yako huko... hivyo hii yako ni furaha ya swala kumtoroka Chui wakati mbele yake kuna Simba..!! Pole

BACK TANGANYIKA
Mbona Rais wakati anawahutubia majaji hivi karibuni alirudia kusema kuwa pesa yote ipelekwe bot!
 
Back
Top Bottom