ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,114
- 49,840
Nawapa Tano Serikali Kwa uamuzi huu, Sasa ni Mwendo wa biashara tuu.
Pia msisahau kulinganisha matozo ya taasisi zote Ili tulipe mara Moja badala ya kuzunguka kwenye Kila taasisi.
====
Katika kuendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini, Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara inatarajia kuanza kutoa leseni zote kupitia Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Awali Leseni Daraja A zilizikuwa zikitolewa na Wakala huo na Leseni Daraja B zilikuwa zikitolewa na Halmashauri nchini hali iliyokuwa ikilalamikiwa na wafanyabiashara kote nchini kuwepo kwa urasimu pindi wanapo safirisha bidhaa au mazao kutoka halmashauri moja kwenda nyingine.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji alipokutana wafanyabiashara pamoja na wajasiriamali wa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kuwasikiliza pamoja na kutatua changamoto zinawazowakabili.
“Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wafanyabishara juu ya hizi leseni zinazokatwa na Halmashauri. Mfano nikiwa na leseni niliyokata Bahi nikiwa napeleka mzigo wangu Chamwino nikipita Dodoma Jiji wananikamata wanataka niwe na leseni ya Jiji na nikifika Chamwino wananikamata wanataka niwe na leseni ya Chamwino. Sasa huu ni usumbufu, hatumsaidii Mhe Rais. Mtu akitoka Kagera kama anapeleka bidhaa Dodoma si atakuwa na leseni 10,” alihoji Waziri Kijaji.
“Tulichokiamua tutakuwa na leseni moja itakayokatwa kupitia BRELA itakayokuwezesha kufanya biashara nchi nzima. Hicho tutakwenda kukifanya ili dhamira ya Mhe Rais wetu ya kurahisisha mazingira ya uwekezaji nchini,” amesema Dk. Kijaji.
Waziri Kijaji amesema kuwa awali Halmashauri zilipewa mamlaka hiyo ya kukata leseni za biashara kutokana na mifumo ya upatikanaji wa leseni zamani ilikuwa ni lazima mfanyabiashara asafiri kwenda Dar es Salaam kwa ajili ya kupata leseni ya biashara lakini kwa sababu ya maendeleo ya Sayansi na Teknolojia wananchi hawana sababu tena ya kusafiri kwenda Dar Es Salaam kwa ajili kupata.
Pia msisahau kulinganisha matozo ya taasisi zote Ili tulipe mara Moja badala ya kuzunguka kwenye Kila taasisi.
====
Katika kuendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini, Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara inatarajia kuanza kutoa leseni zote kupitia Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA).
Awali Leseni Daraja A zilizikuwa zikitolewa na Wakala huo na Leseni Daraja B zilikuwa zikitolewa na Halmashauri nchini hali iliyokuwa ikilalamikiwa na wafanyabiashara kote nchini kuwepo kwa urasimu pindi wanapo safirisha bidhaa au mazao kutoka halmashauri moja kwenda nyingine.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Ashatu Kijaji alipokutana wafanyabiashara pamoja na wajasiriamali wa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kuwasikiliza pamoja na kutatua changamoto zinawazowakabili.
“Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wafanyabishara juu ya hizi leseni zinazokatwa na Halmashauri. Mfano nikiwa na leseni niliyokata Bahi nikiwa napeleka mzigo wangu Chamwino nikipita Dodoma Jiji wananikamata wanataka niwe na leseni ya Jiji na nikifika Chamwino wananikamata wanataka niwe na leseni ya Chamwino. Sasa huu ni usumbufu, hatumsaidii Mhe Rais. Mtu akitoka Kagera kama anapeleka bidhaa Dodoma si atakuwa na leseni 10,” alihoji Waziri Kijaji.
“Tulichokiamua tutakuwa na leseni moja itakayokatwa kupitia BRELA itakayokuwezesha kufanya biashara nchi nzima. Hicho tutakwenda kukifanya ili dhamira ya Mhe Rais wetu ya kurahisisha mazingira ya uwekezaji nchini,” amesema Dk. Kijaji.
Waziri Kijaji amesema kuwa awali Halmashauri zilipewa mamlaka hiyo ya kukata leseni za biashara kutokana na mifumo ya upatikanaji wa leseni zamani ilikuwa ni lazima mfanyabiashara asafiri kwenda Dar es Salaam kwa ajili ya kupata leseni ya biashara lakini kwa sababu ya maendeleo ya Sayansi na Teknolojia wananchi hawana sababu tena ya kusafiri kwenda Dar Es Salaam kwa ajili kupata.