Serikali Iwaombe Fastjet Warudi Nchini Kufanya Biashara ya Usafiri wa Anga

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,060
Kati ya biashara ngumu na sophisticated ni pamoja na biashara ya usafiri wa anga. Makampuni makubwa kabisa ya ndege yenye wataalam wenye weledi na uzoefu, kuna wakati wanaishia kupata hasara. Kama hao wanafeli, itakuwaje kwa nchi kama Serikali ya Tanzania ambayo haijawahi kuendesha mradi wowote kwa faida?

Serikali ya Tanzania haina historia ya kuwa na uwezo wa kuendesha biashara yoyote kwa ufanisi na mafanikio:

1) kwenye simu, Serikali ilishindwa

2) kwenye viwanda Serikali ilishindwa

3) Kwenye madini, Serikali ilishindwa

4) kwenye usafiri wa mabasi, Serikali ilishindwa

5) kwenye umeme, mpaka leo hii tunashuhudia, imeshindwa

6) kwenye usafiri wa majini, Serikali ilishindwa

Serikali ikiingia kwenye ushindani wa biashara huwa inashindwa moja kwa moja, lakini angalao wananchi huwa wanapata huduma iliyokusudiwa.

Serikali inapo monopolize biashara, kwanza itapata hasara, na wananchi mtateseka kwa kukosa huduma.

Wale wa umri wangu wanayakumbuka yafuatayo:

1) wakati wa mwanzo, viwanda vyote vilipokuwa chini ya Serikali, sukari ilikuwa shida, bia shida, sigara shida, sabuni shida, chumvi shida, kuunganishwa simu ilikuwa shida, usafiri ilikuwa shida, kanga ilikuwa shida, betri za radio ilikuwa shida, n.k.

2) sasa hivi baada ya utawala wa Magufuli kuwafukuza fastjet, bei ya tiketi za ndege hazishikiki. Wakati fastjet kama ukiwahi kukata tiketi, kulikuwepo mpaka ticket za sh 80,000. Leo hata tiketi ya sh. 200,000 ATCL hupati.

3) tuna reli ya TAZARA inayofanya safari kati ya Dar mpaka Kaprimposhi, Zambia, ikipitia Tunduma, Mbeya, Makambako, Ifakara mpaka Dar. Kutokana na kawaida ya Serikali kuendesha miradi yote vibaya, reli hiyo haina msaada wowote. Wafanyabiashara bado wanaona aheri kutumia malori kuliko kusafirisha kwa treni ukakutane na ukiritimba wa Serikali. Kama TAZARA ingekuwa inaendeshwa kwa ufanisi, mahindi, mbao, viazi kutoka Mbeya, Njombe, Mafinga hata Songea, vyote vingesafirishwa kwa TAZARA, lakini kwa atitude za watendaji wa Serikali na mashirika ya umma, wengi hawapendi kutumia reli hiyo.

Sasa tuna ndege hizi za ATCL, zinafanya usafiri wa anga bila mshindani yeyote, bado zinaishia kwenye hasara. Na hakika nawahakikishieni, hata reli mpya inayojengwa, kama itaendeshwa na Serikali, itaishia kwenye hasara tu.

Serikali ya Tanzania haina uwezo wa kuendesha kwa faida hata genge la nyanya. Iache biashara zote ziendeshwe na Sekta binafsi. Ni aheri ndege zetu zote pamoja, reli ya TAZARA na SGR itakapomalizika, vikodishwe kwa sekta binafsi kwa uendeshaji. Bila hivyo tutegemee miradi hiyo kuwa na hasara wakati wote, na hu⁵duma duni.
 
Yaani kwenye usafiri wa mabasi hasa huu wa DART ndio huwa siielewi kabisa Serikali kushindwa kuuendesha, maana factors muhimu zote zipo
1.Abiria wa kutosha kabisa,

2.Miundo mbinu mizuri hasa DART Phase I

3.Sole operator kwa baadhi ya njia

KWANINI mradi unasuasua??..INASHANGAZA SANA
 
Pole sana.

Hawa ATCL, bei zao ni za ajabu. Ndege badala ya kuonekana ni usafiri wa kawaida, wanataka kuufanya kiwe kipimo cha utajiri.

Mimi nimepunguza sana kutumia ndege maana sasa hivi hata muda hauzingatiwi. Na usalama pia huwezi kuwa na uhakika nao.
ATCL ni full ubabaishaji, hawana ratiba iliyosimama na kuna wakati mnaweza chelewa kwa kumngoja abiria waziri ambaye yupo uwanjani akifanya maongezi na rafikie, suala la usalama ndio kabisaa naomba nikae kimya
 
Yaani kwenye usafiri wa mabasi hasa huu wa DART ndio huwa siielewi kabisa Serikali kushindwa kuuendesha,maana factors muhimu zote zipo
1.Abiria wa kutosha kabisa,
2.Miundo mbinu mizuri hasa DART Phase I
3.Sole operator kwa baadhi ya njia
KWANINI mradi unasuasua??..INASHANGAZA SANA
Wizi wizi wizi wizi wizi wizi wizi wizi!

Hakuna tatizo zaidi ya hilo....

Watanzania woote ni wezi tupu!
 
Pole sana.

Hawa ATCL, bei zao ni za ajabu. Ndege badala ya kuonekana ni usafiri wa kawaida, wanataka kuufanya kiwe kipimo cha utajiri.

Mimi nimepunguza sana kutumia ndege maana sasa hivi hata muda hauzingatiwi. Na usalama pia huwezi kuwa na uhakika nao.
Nilikuwa na safari ya mpanda, kuchek na atcl wana ndege mara moja kwa wiki , bei 800000 plus , one way,
 
ATCL ni full ubabaishaji, hawana ratiba iliyosimama na kuna wakati mnaweza chelewa kwa kumngoja abiria waziri ambaye yupo uwanjani akifanya maongezi na rafikie, suala la usalama ndio kabisaa naomba nikae kimya
Ccm hovyo!
 
Yaani kwenye usafiri wa mabasi hasa huu wa DART ndio huwa siielewi kabisa Serikali kushindwa kuuendesha,maana factors muhimu zote zipo...
Hapo ndipo inapodhihirisha kuwa Serikali haina uwezo wa kuendesha biashara yoyote hata iwe ni biashara rahisi na yenye faida ya kiwango gani.

Fikiria kushindwa kuendesha biashara hata ya mabasi tu! Ilishindwa kuendesha hata biashara ya mabenki kjkiwa hakuna benki binafsi hata moja.
 
Tumeshindwa endesha Mwendokasi...ndo tutaweza shirika la ndege?...Atcl ni shimo la kupoteza pesa...

Kuna mtu aliniambia alikuwa mbeya washapanda ndege ikapigwa simu kuna waziri kachelewa kuwahi airport..ndege ikabidi imsubiri...sasa hapo utapataje wateja??siasa kwenye biashara serious
 
Nilikuwa na safari ya mpanda, kuchek na atcl wana ndege mara moja kwa wiki , bei 800000 plus , one way,
Kwa sasa tumekosa vyote. Tunakosa huduma iliyo bora, tunakosa huduma inayolingana na thamani ya pesa, na nchi inakula hasara kwa kutotengeneza faida.

Kwa sasa shirika linaendelea kwa kusuasua kwa vile tu hakuna mshindani, la sivyo wangesjmama kabisa.

Pesa inayopelekwa kwenye ununuzi wa ndege ni upotevu mtupu. Ni aheri pesa hiyo ingekuwa inapelekwa kwenye ujenzi wa barabara au ujenzi wa hospitali au shule. Kwenye reli ni aheri Serikali ingejenga tu reli, treni zinunuliwe na makampuni binafsi yatakayokuwa yakiilipa Serikali kwa kutumia miundombinu yake.
 
Kati ya biashara ngumu na sophisticated ni pamoja na biashara ya usafiri wa anga. Makampuni makubwa kabisa ya ndege yenye wataalam wenye weledi na uzoefu, kuna wakati wanaishia kupata hasara. Kama hao wanafeli, itakuwaje kwa nchi kama Serikali ya Tanzania ambayo haijawahi kuendesha mradi wowote kwa faida?

Serikali ya Tanzania haina historia ya kuwa na uwezo wa kuendesha biashara yoyote kwa ufanisi na mafanikio:

1) kwenye simu, Serikali ilishindwa

2) kwenye viwanda Serikali ilishindwa

3) Kwenye madini, Serikali ilishindwa

4) kwenye usafiri wa mabasi, Serikali ilishindwa

5) kwenye umeme, mpaka leo hii tunashuhudia, imeshindwa

6) kwenye usafiri wa majini, Serikali ilishindwa

Serikali ikiingia kwenye ushindani wa biashara huwa inashindwa moja kwa moja, lakini angalao wananchi huwa wanapata huduma iliyokusudiwa.

Serikali inapo monopolize biashara, kwanza itapata hasara, na wananchi mtateseka kwa kukosa huduma.

Wale wa umri wangu wanayakumbuka yafuatayo:

1) wakati wa mwanzo, viwanda vyote vilipokuwa chini ya Serikali, sukari ilikuwa shida, bia shida, sigara shida, sabuni shida, chumvi shida, kuunganishwa simu ilikuwa shida, usafiri ilikuwa shida, kanga ilikuwa shida, betri za radio ilikuwa shida, n.k.

2) sasa hivi baada ya utawala wa Magufuli kuwafukuza fastjet, bei ya tiketi za ndege hazishikiki. Wakati fastjet kama ukiwahi kukata tiketi, kulikuwepo mpaka ticket za sh 80,000. Leo hata tiketi ya sh. 200,000 ATCL hupati.

3) tuna reli ya TAZARA inayofanya safari kati ya Dar mpaka Kaprimposhi, Zambia, ikipitia Tunduma, Mbeya, Makambako, Ifakara mpaka Dar. Kutokana na kawaida ya Serikali kuendesha miradi yote vibaya, reli hiyo haina msaada wowote. Wafanyabiashara bado wanaona aheri kutumia malori kuliko kusafirisha kwa treni ukakutane na ukiritimba wa Serikali. Kama TAZARA ingekuwa inaendeshwa kwa ufanisi, mahindi, mbao, viazi kutoka Mbeya, Njombe, Mafinga hata Songea, vyote vingesafirishwa kwa TAZARA, lakini kwa atitude za watendaji wa Serikali na mashirika ya umma, wengi hawapendi kutumia reli hiyo.

Sasa tuna ndege hizi za ATCL, zinafanya usafiri wa anga bila mshindani yeyote, bado zinaishia kwenye hasara. Na hakika nawahakikishieni, hata reli mpya inayojengwa, kama itaendeshwa na Serikali, itaishia kwenye hasara tu.

Serikali ya Tanzania haina uwezo wa kuendesha kwa faida hata genge la nyanya. Iache biashara zote ziendeshwe na Sekta binafsi. Ni aheri ndege zetu zote pamoja, reli ya TAZARA na SGR itakapomalizika, vikodishwe kwa sekta binafsi kwa uendeshaji. Bila hivyo tutegemee miradi hiyo kuwa na hasara wakati wote, na hu⁵duma duni.
5 brandi nyuu eti zinashuka sun.
 
Back
Top Bottom