Serikali iuangalie mji wa Kahama kwa jicho la tatu

Serikali iuangalie mji wa Kahama kwa jicho la tatu

Traxtion

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2021
Posts
5,895
Reaction score
11,788
Picha zote nilizotumia kwenye uzi huu ni za Kahama
Screenshot_2026-01-13-21-45-10-712_com.google.android.youtube.png
Mimi sio mkazi wa Kahama ila huu mji unahitaji attention
Kahama ni mji unaokua kwa kasi na mzunguko wa hela upo vizuri kwa level za Kitanzania
Screenshot_2026-01-13-21-40-24-904_com.google.android.youtube.png


Screenshot_2026-01-13-21-42-42-039_com.google.android.youtube.png

Population inakua kwa kasi na sababu kuu ni shughuli za uchimbaji madini
Lakini hivi karibuni tumeona mgodi wa Buzwagi umefungwa, inaonekana madini yameisha au yamebaki kidogo
Serikali ikasema itajenga viwanda katika eneo ambapo mgodi huo ulikuwepo, ni idea nzuri lakini viwanda ni heri viwe vingi sana, sio tu mnajenga viwanda kumi. Viwepo viwanda hata zaidi ya 100 huko
Screenshot_2026-01-13-21-43-43-507_com.google.android.youtube.png
Screenshot_2026-01-13-21-46-16-544_com.google.android.youtube.png


Screenshot_2026-01-13-21-38-27-235_com.google.android.youtube.png

Mtazamo wangu ni kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kuanzisha Industrial park kubwa Kahama, ikiwezekana iwe kama ile ya SINO-TAN inayojengwa Kibaha
Screenshot_2026-01-13-21-43-23-006_com.google.android.youtube.png
Screenshot_2026-01-13-21-42-55-177_com.google.android.youtube.png

Kwa nini? Kama mji umeweza kukua kwa kasi vile bila mchango mkubwa wa serikali na sio hivyo tu, bado unaendelea kukua hadi sasahivi maana yake serikali inapaswa ichangamkie mji wa Kahama kutumika kutengeneza ajira. Kwa mkono wa serikali Kahama itaendelea zaidi tena kwa kasi ya juu.
Screenshot_2026-01-13-21-38-27-235_com.google.android.youtube.png


Miji inayokua kwa kasi ina faida sana Tanzania, kwa mfano mji kama Kahama ndani ya muda wake wa ukuaji umesaidia vijana wengi sana kujikwamua kiuchumi. Wengi wameenda kuwekeza biashara zao Kahama na matunda yake wameyaona
Screenshot_2026-01-13-21-38-07-983_com.google.android.youtube.png

Tanzania inapaswa kuhakikisha miji yote yenye watu wengi inapewa support na kuongeza mzunguko wa hela ili isizidi kukua.
Screenshot_2026-01-13-21-34-20-956_com.google.android.youtube.png
Inasikitisha kuona miji inakua kwa kasi halafu serikali inaangalia tu mpaka baadae inaanza kujifia au maendeleo yanakuwa ya konokono, kama Moshi tungekuwa nayo serious ungekuwa mji mkubwa wenye fursa nyingi za kiuchumi, badala yake umebaki kuwa mji mdogo wa watu laki 2 sijui, na maendeleo yake ni yale yaliyofanywa miaka ya nyuma
Screenshot_2026-01-13-21-38-07-983_com.google.android.youtube.png
Screenshot_2026-01-13-21-34-54-496_com.google.android.youtube.png

Kwa upande wa Kahama serikali inapaswa kuhakikisha inaboresha miundombinu. Barabara za Kahama zina mashimo, na zimejaa michanga. Zinahitaji kuwa refurbished au zijengwe upya katika viwango vya juu
Screenshot_2026-01-13-21-39-54-316_com.google.android.youtube.png
Screenshot_2026-01-13-21-40-44-104_com.google.android.youtube.png

Pia stendi ya mabasi ya Kahama ni duni, inapaswa kuboreshwa au ijengwe stand mpya lakini isijengwe mbali na makazi ya watu kama tulivyofanya maeneo mengine. To make the town more alive stand kuu ijengwe ndani ya mji
Kwa sasa stendi ya Kahama ndio hii
Screenshot_2026-01-13-21-41-51-611_com.google.android.youtube.png
Screenshot_2026-01-13-21-41-19-313_com.google.android.youtube.png


My take: Serikali haiwezi kutoa ajira kwa kila mtu lakini tunajua inaweza kuandaa mazingira mazuri ya kujiajiri. Ukiondoa kilimo na ufugaji ambavyo hufanywa zaidi vijijini, ukija mijini ili mtu ajiajiri na kupata pesa kunafaa kuwe na mzunguko wa hela

Serikali inapaswa kujenga viwanda, vyuo vikuu, miundombinu bora na kualika wawekezaji waje kuwekeza kwenye miji hii ili pesa izunguke. Inakuwa rahisi kwa Watanzania kujiajiri na kupata maisha mazuri

Sio tu Kahama, Tanzania tuna miji ambayo hatujui kuitumia. Miji yetu ina watu ambao wengi wao ni vijana, na watu ndio utajiri mkubwa kwenye nchi yoyote ile, ili kuuona utajiri wa watu ni lazima tutengeneze mazingira ya kuingiza hela kiurahisi.

Screenshot_2026-01-13-21-34-37-896_com.google.android.youtube.png

Sio tu Kahama, serikali inapaswa ianze kuja na mipango ya kuifanya miji ya Tanzania kuwa alive zaidi kibiashara. Miji kama
1. Morogoro
2. Moshi
3. Mbeya
4. Mtwara mjini
5. Kigoma mjini
6. Iringa
7. Katoro
8. Geita
9. Makambako
10. Bukoba
11. Songea
12. Njombe
13. Sumbawanga
14. Masasi
15. Babati
16. Kibaigwa
17. Gairo
18. Tunduma
19. Tunduru
20. Tandahimba
21. Ikwiriri
22. Mkuranga
23. Buseresere
24. Kasulu
25. Chalinze
26. Songwe
Na mingine mingi ina watu wengi lakini kinachokosekana ni mzunguko wa hela wa kutosha.

Tufikirie, tutafute namna ya kuiamsha miji yetu kibiashara

Si mnaona jiji la Dar lilivyo. Dar es Salaam ni one of Tanzania's biggest success. Licha ya kuwa jiji lenye matatizo mengi lakini ni kitovu cha biashara kwa Tanzania. Ni jiji lililosaidia watu wengi sana kufanikiwa kimaisha kupitia biashara. Naliheshimu sana jiji la Dar
Sasa haya mambo yasiishie Dar tu, tusambaze maendeleo na kuongeza mzunguko wa hela ili vijana wajitafute kimaisha kwenye maeneo mengi kupitia biashara. Isiwe Dar tu
 
Serikali haina mchango wowote.
Kahama wananchi Wana maji yao binafsi
Kahama wananchi wqna umeme wao binafsi
Kahama wananchi wanajijengea mabarabara ya lami

Kwa mujibu wa picha hizo ofisi za umma kahama hakuna kabisa, wananchi ni kama wapo katika nchi yao kivyao vyao...

Maandiko mengine ni mazuri ila..
 
Upo sawa. Ongeza miji mingine midogo kama Babati, Kibaigwa, Gairo, Tunduma, Tunduru, Tandahimba, Ikwiriri, Mkuranga, Buseresere, Kasulu, Chalinze ni miji midogo inayokua kwa kasi sana ambayo inahitaji attention ya serikali ili ikue kisasa.
 
Sasa mji umekuwa bila mchango wa serikali, unahofu gani serikali ikiendelea kuwa kimya bila kutoa mchango wowote?
Mji unapokuwa kwa kasi bila serikali kuingilia kati kunasababisha mapungufu mengi
Mfano angalia Kahama, wananchi wanajenga nyumba kali, supermarkets, hotels, lodges nk lakini they can't go beyond that
Kuna vitu ni lazima serikali iingilie kati. Barabara za Kahama kwa mfano, ni za vumbi, nyingi zimechakaa, zimejaa mchanga na mashimo kila kona, stendi ni ya vumbi bado, watu wanajenga bila kufuata mpangomji, pia inabidi waboreshe usambazaji wa maji nk. Mwisho wa siku mji unakuwa shaghalabaghala kama serikali ikikaa kimya
Ni muhimu serikali kuingilia kati miji yote yenye potential Tanzania na kuiamsha kiuchumi miji iliyolala

Pia kwa mji unaokua kama Kahama, serikali inahitaji kuongeza uwekezaji tu bila kulazimisha maendeleo, mji unakua. Kwa sababu mji una activities nyingi za kiuchumi, maana yake kuongeza uwekezaji kunakuza mji, kipato cha watu na cha taifa kiujumla
 
Upo sawa. Ongeza miji mingine midogo kama Babati, Kibaigwa, Gairo, Tunduma, Tunduru, Tandahimba, Ikwiriri, Mkuranga, Buseresere, Kasulu, Chalinze ni miji midogo inayokua kwa kasi sana ambayo inahitaji attention ya serikali ili ikue kisasa.
Sahihi, nimepita Chalinze mara nyingi, ule mji unajengeka kwa kasi, na wenyewe unahitaji attention ya serikali
Kuanzia Chalinze, Babati, Kasuli na miji yote uliyoitaja hapo
 
Kutegemea maendeleo yaletwe na serikali ya CCM ni ndoto mbaya sana, billions of dollars zinatoka Kahama kila mwaka lakini barabara zimejaa vumbi tupu
Lakini mbona Dar na Dodoma wanaziendeleza vizuri. Inafika hatua mtu akitaja Tanzania anafikiria tu Dar, Dodoma, Zanzibar au Arusha
Nguvu walizotumia kuendeleza hiyo miji wazihamishie kwenye miji midogo sasa. Tanzania tukiangalia miji kama Dar au Mwanza tunajiona tumemaliza kazi ila actually kazi ni kubwa sana
Mikoani huku kila kukicha inaibuka miji inakua kwa kasi, serikali haileti maendeleo kuikeep miji alive, matokeo yake muda unaenda, miji inajifia maendeleo yanastop au yanapungua speed
 
Buzwagi haina mchango kiviiile kwenye maendeleo ya mji wa Kahama!!

Migodi midogo ndiyo kila kitu,Barrick wameikuta Kahama inakimbiza na wameiacha.

NB:Hayo mashimo unayoyaona barabarani (Tabora Rd-Ngaya Rd) ni uchomaji matairi 29/10/2025!!
 
Buzwagi haina mchango kiviiile kwenye maendeleo ya mji wa Kahama!!

Migodi midogo ndiyo kila kitu,Barrick wameikuta Kahama inakimbiza na wameiacha.

NB:Hayo mashimo unayoyaona barabarani (Tabora Rd-Ngaya Rd) ni uchomaji matairi 29/10/2025!!
Kama ukuaji wake unategemea migodi midogo basi ni vyema
Lakini hizi picha za Kahama ni before October 29. Nimezitoa kwenye video ya Bertin
Mashimo ya kwenye barabara ni miundombinu mibovu. Hapo ni kabla ya October 29
 
Kuna dogo mmoja juzi ananambia huko ushirombo watu wanataka kung'oa lami mna imelalia madini dah sasa sijui wamefikia wapi
 
Kama ukuaji wake unategemea migodi midogo basi ni vyema
Lakini hizi picha za Kahama ni before October 29. Nimezitoa kwenye video ya Bertin
Mashimo ya kwenye barabara ni miundombinu mibovu. Hapo ni kabla ya October 29
Barabara ya lami iliyokuwa na mashimo before 29th October ni Isaka Rd na ilishafumuliwa lami yote kabla hata ya uchaguzi.

Barabara zenye mashimo yasiyohusiana na October 29 kwa sasa ni vipande viwili (Brbr la kupanda/Clinic Rd na Brbr la Kushuka)
 
Barabara ya lami iliyokuwa na mashimo before 29th October ni Isaka Rd na ilishafumuliwa lami yote kabla hata ya uchaguzi.

Barabara zenye mashimo yasiyohusiana na October 29 kwa sasa ni vipande viwili (Brbr la kupanda/Clinic Rd na Brbr la Kushuka)
Sijui labda tunatofautiana mawazo. Ila barabara kama hizi hazina mashimo lakini zimechoka na zimejaa mchanga. Binafsi naona unapaswa ziwe refurbished
Mji una watu wengi na biashara zinakua, it really needs better roads, not just "roads"
Screenshot_2026-01-13-21-40-44-104_com.google.android.youtube.png
 
Sijui labda tunatofautiana mawazo. Ila barabara kama hizi hazina mashimo lakini zimechoka na zimejaa mchanga. Binafsi naona unapaswa ziwe refurbished
Mji una watu wengi na biashara zinakua, it really needs better roads, not just "roads"
View attachment 3529683
Hope wamekusikia,ukipata muda ingia Barabara za mitaani ndanindani ndiyo hasa wakazi wa mji huo wanazilalamikia kuliko hata hizo lami.
 
Sijui labda tunatofautiana mawazo. Ila barabara kama hizi hazina mashimo lakini zimechoka na zimejaa mchanga. Binafsi naona unapaswa ziwe refurbished
Mji una watu wengi na biashara zinakua, it really needs better roads, not just "roads"
View attachment 3529683
Unajua umri wa hiyo barabara?

Mara ya mwisho kufika kahama ni lini?

Muhimu ni kuzihudumia hizo barabara kwa kuzifanyia usafi, McFerrin iwe Safi, wananchi watimize wajibu wao wa kulinda na kutunza miundombinu.

Mahitaji ni mengi, sasa hivi Kuna ujenzi mkubwa wa hospital kubwa hapo kahama, kwenye hiyo video haujaoneshwa hilo pia?

Fika kahama kaka ukapate viwanja vinavyo uzwa na halmashauri ya Manispaa
 
Back
Top Bottom