G-Mdadisi
Senior Member
- Feb 15, 2018
- 157
- 99
Anaandika Gaspary Charles.
Ukifuatilia kwa jicho la ndani namna mwenendo wa uhamasishaji jamii zoezi la Sensa ya watu na makaazi linavyoendelea kuchukuliwa nchini utagundua kuna jambo haliendi sawasawa eidha kwa makusudi au bahati mbaya na linahitaji kurekebiswa mapema kabla ya siku yenyewe ili kufanya zoezi hili kufanikiwa kwa kiwango kikubwa na watanzania wote wanahesabiwa.
Mpaka sasa ukidadisi vizuri utabaini kwamba zoezi limebebwa zaidi kwa mtazamo wa kiserikali kutokana na kundi lililo msitari wa mbele zaidi kwenye uhamasishaji na utoaji elimu zaidi ni viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya mtaa na hata serikali kuu, wakiongozwa na kamisaa wa Sensa kitaifa, Anna Makinda kwa Bara, na Balozi Moh'd Haji Hamza kwa Zanzibar, maDC, DED, RC nk. na kwa mbali kabisa Chama cha Mapinduzi CCM.
Ni wazi ushiriki wa Asasi za kiraia katika uhamasishaji wa watu bado ni mdogo na pengine hii inatokana na namna ambavyo mamlaka zimeratibu zoezi hili imepelekea asasi kujiona mchango wake ni mdogo katika zoezi hili, na hivyo kushindwa kujitokeza mbele kusaidia ufikishaji wa elimu moja kwa moja.
Ukifungua TV, ukasikiliza radio na kusoma magazeti na mitamdao ya kijamii, habari kuu ya Sensa ni kuhusu kamisaa wa Sensa kitaifa Mhe. Makinda au Balozi Hamza wa Zanzibar ambao wamefunga kambi na kutembea nchi nzima mkoa kwa mkoa kuhakikisha jamii inafahamu umuhimu wa kuhesabiwa, jambo ambalo linatafakarisha na kutia mashaka juu ya uwezekano wa watanzania wote kufikiwa na elimu hii.
Ikiwa ni karibu siku 40, takriban mwezi mmoja tu umebaki kufika August 23, Vyama vya siasa hasa upinzani vipo kimya kuhusu zoezi hili, Asasi za Kiraia zipo kimya. Hii si sawa hata kidogo, hili ni zoezi ambalo linahitaji ushiriki wa kila mmoja kwa nafasi yake.
Licha ya juhudi na kazi kubwa inayofanywa na viongozi wandamizi wa serikali, zoezi hili linahitaji ushiriki wa makundi yote katika ufikishaji wa elimu ili lifanikiwe kwa ukamilifu na sio serikali kujibebesha mzigo ambao sekta binafsi kupitia asasi za kiraia kama wadau wa maendeleo wangeweza kusaidia kwa kiwango kikubwa.
Hili ni zoezi la kitaifa, sio la serikali, chama wala kundi fulani.
JIANDAE KUHESABIWA.
Ukifuatilia kwa jicho la ndani namna mwenendo wa uhamasishaji jamii zoezi la Sensa ya watu na makaazi linavyoendelea kuchukuliwa nchini utagundua kuna jambo haliendi sawasawa eidha kwa makusudi au bahati mbaya na linahitaji kurekebiswa mapema kabla ya siku yenyewe ili kufanya zoezi hili kufanikiwa kwa kiwango kikubwa na watanzania wote wanahesabiwa.
Mpaka sasa ukidadisi vizuri utabaini kwamba zoezi limebebwa zaidi kwa mtazamo wa kiserikali kutokana na kundi lililo msitari wa mbele zaidi kwenye uhamasishaji na utoaji elimu zaidi ni viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya mtaa na hata serikali kuu, wakiongozwa na kamisaa wa Sensa kitaifa, Anna Makinda kwa Bara, na Balozi Moh'd Haji Hamza kwa Zanzibar, maDC, DED, RC nk. na kwa mbali kabisa Chama cha Mapinduzi CCM.
Ni wazi ushiriki wa Asasi za kiraia katika uhamasishaji wa watu bado ni mdogo na pengine hii inatokana na namna ambavyo mamlaka zimeratibu zoezi hili imepelekea asasi kujiona mchango wake ni mdogo katika zoezi hili, na hivyo kushindwa kujitokeza mbele kusaidia ufikishaji wa elimu moja kwa moja.
Ukifungua TV, ukasikiliza radio na kusoma magazeti na mitamdao ya kijamii, habari kuu ya Sensa ni kuhusu kamisaa wa Sensa kitaifa Mhe. Makinda au Balozi Hamza wa Zanzibar ambao wamefunga kambi na kutembea nchi nzima mkoa kwa mkoa kuhakikisha jamii inafahamu umuhimu wa kuhesabiwa, jambo ambalo linatafakarisha na kutia mashaka juu ya uwezekano wa watanzania wote kufikiwa na elimu hii.
Ikiwa ni karibu siku 40, takriban mwezi mmoja tu umebaki kufika August 23, Vyama vya siasa hasa upinzani vipo kimya kuhusu zoezi hili, Asasi za Kiraia zipo kimya. Hii si sawa hata kidogo, hili ni zoezi ambalo linahitaji ushiriki wa kila mmoja kwa nafasi yake.
Licha ya juhudi na kazi kubwa inayofanywa na viongozi wandamizi wa serikali, zoezi hili linahitaji ushiriki wa makundi yote katika ufikishaji wa elimu ili lifanikiwe kwa ukamilifu na sio serikali kujibebesha mzigo ambao sekta binafsi kupitia asasi za kiraia kama wadau wa maendeleo wangeweza kusaidia kwa kiwango kikubwa.
Hili ni zoezi la kitaifa, sio la serikali, chama wala kundi fulani.
JIANDAE KUHESABIWA.