Serikali inataka kuua na kuzorotesha shule binafsi?

Serikali inataka kuua na kuzorotesha shule binafsi?

Freyzem

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2013
Posts
10,318
Reaction score
25,111
Miongoni mwa sekta ambazo zimekuwa hazifanyi vyema kwa muda mrefu ni haswa kwenye sekta ya elimu.

Sekta hii imechezewa na kukumbwa na mabadiliko ya mara kwa mara ambayo kimsingi yamekuwa hayana tija kubwa.

Shule binafsi ni miongoni mwa shule ambazo zimekuwa zikifanya vyema hasa kutokana na uwekezaji na mikakati iliyojiwekea katika kutoa elimu.

Serikali hivi sasa imejipambanua kwa sera yake ya elimu bure, jambo ambalo limesababisha idadi kubwa ya watoto kupelekwa kwenye shule za Serikali.

Hali hii imepelekea idadi kubwa sana ya wanafunzi wanaopelekwa shule binafsi kupungua kwa kiwango kikubwa sana, jambo linalotishia uhai wa shule hizi ambazo zimewekezwa kwa fedha nyingi na pia kutishia kupoteza ajira kwa walioajiriwa huko!

Mbaya zaidi ni huu ubaguzi ambao "mkubwa" ameounyesha hadharani kwenye suala la mikopo ya elimu ya juu.

Kwa kweli hii itapelekea zaidi kudidimiza shule binafsi kwani wazazi wengi hawana uwezo wa kusomesha watoto wao vyuo vikuu.

Tutarajie mwakani idadi ndogo zaidi ya wanafunzi kupelekwa shule binafsi, na hata waalimu wengi walioajiriwa huko kwenye shule binafsi kupoteza ajira zao, siyo hayo tu bali hata kufungwa kwa shule nyingi kutokana na kukosa wanafunzi na kushindwa kujiendesha.

Ikumbukwe pia zipo shule nyingine ambazo zilijengwa kwa mikopo kutoka benk, hizi nazo hazitobaki salama mnada utazipitia.

Sasa hivi kwenye kusoma namba, tupo "conic section".
 
Hii ni vita watanzania tunatandikwa kila sehem. Lakini Mungu yu pamoja nasi
 
WATAKUJA KUSEMA WALIYOSOMA NJE VYUO HUKO HAKUNA KUWAPA AJIRA TZ

OVA
 
ni kweli mana ukijaribu kuangalia trend za matukio na maneno yanayolenga private schools unaona wazi kuna chuki ama siasa za kijinga ama za kipumbavu
kwani mtu akisoma private school ana laana? au private schools ni shule za mashetani? hata kama humpi mkopo mwambie kistaarabu lakini sio kudhihaki hadharani
"ubaguzi wa kielimu"

wajue tu ya kwamba hata mtoe elimu ya bure kwa shule za serikali kama hamna mipango madhubuti ya kuweka mazingira bora ya kusoma na kutoa elimu bora na sio bora elimu basi labda mnaweza kuendana na private school, kutoa elimu bure haina mana kama kuna wanafunzi bado wanakaa kwenye matofali na kuandika kwenye mavumbi na choo kinatumika kimoja na wanafunzi pamoja na walimu na madarasa yana ufa ..lakini viongozi wakubwa wa eneo hilo kuanzia diwani hadi mbunge hadi mkuu wa mkoa wanatembelea v8 na watoto wao wako private schools tena za nje ya nchi.
 
Miongoni mwa sekta ambazo zimekuwa hazifanyi vyema kwa muda mrefu ni haswa kwenye sekta ya elimu..

Sekta hii imechezewa na kukumbwa na mabadiliko ya mara kwa mara ambayo kimsingi yamekuwa hayana tija kubwa!

Shule binafsi ni miongoni mwa shule ambazo zimekuwa zikifanya vyema hasa kutokana na uwekezaji na mikakati iliyojiwekea katika kutoa elimu!

Serikali hivi sasa imejipambanua kwa sera yake ya elimu bure, jambo ambalo limesababisha idadi kubwa ya watoto kupelekwa kwenye shule za serikali!

Hali hii imepelekea idadi kubwa sana ya wanafunzi wanaopelekwa shule binafsi kupungua kwa kiwango kikubwa sana, jambo linalotishia uhai wa shule hizi ambazo zimewekezwa kwa fedha nyingi na pia kutishia kupoteza ajira kwa walioajiriwa huko!

Mbaya zaidi ni huu ubaguzi ambao "mkubwa" ameounyesha hadharani kwenye suala la mikopo ya elimu ya juu...

Kwa kweli hii itapelekea zaidi kudidimiza shule binafsi kwani wazazi wengi hawana uwezo wa kusomesha watoto wao vyuo vikuu!

Tutarajie mwakani idadi ndogo zaidi ya wanafunzi kupelekwa shule binafsi, na hata waalimu wengi walioajiriwa huko kwenye shule binafsi kupoteza ajira zao, siyo hayo tu bali hata kufungwa kwa shule nyingi kutokana na kukosa wanafunzi na kushindwa kujiendesha!

Ikumbukwe pia zipo shule nyingine ambazo zilijengwa kwa mikopo kutoka benk, hizi nazo hazitobaki salama mnada utazipitia....

Sasa hivi kwenye kusoma namba, tupo "conic section".
Kuna taarifa kuwa kuanzia 2021 watakaokuwa wanapewa kipaumbele kwenye kuajiriwa katika taasisi za serikali eti ni wale waliosoma shule za serikali inasemekana rais ametoa maagizo hayo hiii ni hatariii Sana tena Sana
 
dah ile speech ilitekenya hadi kongosho yangu kuhusu mkopo
 
Wanaosoma shule / vyuo binafsi wasikate tamaa. Wasome kwa juhudi ili wapate uwezo wa kuanzisha shughuli za kujiajiri na pia waweze kuajiri wenzao na wengineo!
 
Tuanze na ka research kadogo, hivi kweli wooote waliosoma private wamekosa mikopo, kama uko chuo umekosa mkopo au umeshindwa kwenda chuo kwa kukosa mkopo ebu tujuze tujue ukweli.

Na kama umesoma private na umepata mkopo pia tujuze ila iwe kweli usiropoke tu kama jingalao!!!
 
Kwa hyo mkulu akitoka bado hali itaendelea kuwa huvyo?mi naona tuautishane sana,akiondoka watakuja na yao na siajabu walio soma binafis watapewa kipaumbele.wewe unayemtakia mtoto Elimu bora kaza buti tu mkulu akienda sana mwisho ni 2025,atakaye kuja atakuja na grisi,hii haina miongozo kila mkulu huja na miongozo yake.rejea Kwa jk,mtoto akipata mimba baada ya kujifungua arejee school.Je?sasa hivi?
 
Watakufa wao....kama shule zao zilivyokufa tayari.
 
Back
Top Bottom