Serikali inakosea sana kuwatenganisha Kikazi Wanandoa

rushanju

JF-Expert Member
Nov 3, 2011
3,131
4,620
Mimi ni mfanyakazi wa Serikali na ni mtumishi wa muda mrefu nimebakiza miaka mitatu kustaafu. Mkewe wangu nae ni mfanyakazi wa Serikali ila yeye alibaki Dar. Tumetenganishwa kwa nguvu na hili la Dodoma. Tumebahatika kupata watoto.

Baadhi ya watoto wetu wako kwenye ndoa na wengine wako vyuoni nasi. Mke wangu bado ana miaka 13 kazini kabla ya kustaafu. Majuzi amenitembelea hapa Dodoma, alifika akiwa anajisikia vibaya na tukafanya utaratibu wa kwenda hospital. Tulikutana na Dr mstaarabu na akatushauri tupime Ukimwi kwa pamoja.

Majibu yalitoka na mke wangu akiwa Chanya + tulipima tena hospital nyingine na bado ilibaki vilevile. Sasa nabaki najiuliza, jamii itatuelewaje? Watoto watatuelewaje? Wakwe watatuelewaje? Nimekata tamaa na nimebaki bila majibu.

Jamani wenzangu mkae mkijua kuwa hili limetokea kwangu, ukweli wenyewe wengi mko kwenye maisha hayo. Serikali imefanya makosa makubwa sana kutenganisha ndoa za watu kwa makusudi. Watoto wengi walioko mitaani hawana maadili kwa kukosa malezi ya baba na mama.

Hapa tunajenga taifa au tunabomoa. Nimebaki njia panda. Nimfukuze? Nimuue? Au nifanyeje. Huu ni utumishi Serikalini au ni utumwa serikalini. Nimeshindwa kula hata kazini sijaenda. Mke wangu karudi Dar nae sijui anaenda kujiua!

Mbali na lawama kwa mke wangu bado zigo la lawama nawatupia Serikali kwa kukatisha ndoa yangu na pengine itakatisha maisha ya mke wangu aliyeondoka kwa kuchanganyikiwa. Hili la Dodoma linaonekana kama masihara lakini ni janga kubwa sana. Tumejichimbia kaburi kimzaha.
 
Pole sana mkuu.
Mimi pia niko huku Dodoma.
Nashuhudia wimbi kubwa la waume walioko kwenye ndo wakiwa peke yao bila wake zao.
Anyway, ila kujitunza ni suala la mtu mwenyewe binafsi, kuhamishiwa Dodoma sidhani kama ni kikwazo, japo kuna ukweli ndani yake.
 
Hilo ni jambo la kawaida, ukimwi siku hizi sio ugonjwa mzee wangu, ogopa kansa, pressure, nk! Wewe unaogopa jamii na wattoto wenu, mtaenda kuwatangazia?? Kuna watu wanashida nyingi kuliko hata zako wamekaa nazo kimya na maisha yanaenda, hivyo tuliza akili na chukulia ukimwi na ugonjwa mwingine na mtakula bata mpaka miaka 100 mzee wangu!! Ndo maana ya kiapo cha ndoa kwenye shida na raha! Mtie moyo mkeo , wewe kwa sasa ndo faraja yake! Sio wewe tena mwanaume kuanza kupaparika, simama kiume mzee!! Ukihitaji msaada zaidi njoo pm
 
Hilo ni jambo la kawaida, ukimwi siku hizi sio ugonjwa mzee wangu, ogopa kansa, pressure, nk! Wewe unaogopa jamii na wattoto wenu, mtaenda kuwatangazia?? Kuna watu wanashida nyingi kuliko hata zako wamekaa nazo kimya na maisha yanaenda, hivyo tuliza akili na chukulia ukimwi na ugonjwa mwingine na mtakula bata mpaka miaka 100 mzee wangu!! Ndo maana ya kiapo cha ndoa kwenye shida na raha! Mtie moyo mkeo , wewe kwa sasa ndo faraja yake! Sio wewe tena mwanaume kuanza kupaparika, simama kiume mzee!! Ukihitaji msaada zaidi njoo pm
Yataka moyo!
 
Hilo ni jambo la kawaida, ukimwi siku hizi sio ugonjwa mzee wangu, ogopa kansa, pressure, nk! Wewe unaogopa jamii na wattoto wenu, mtaenda kuwatangazia?? Kuna watu wanashida nyingi kuliko hata zako wamekaa nazo kimya na maisha yanaenda, hivyo tuliza akili na chukulia ukimwi na ugonjwa mwingine na mtakula bata mpaka miaka 100 mzee wangu!! Ndo maana ya kiapo cha ndoa kwenye shida na raha! Mtie moyo mkeo , wewe kwa sasa ndo faraja yake! Sio wewe tena mwanaume kuanza kupaparika, simama kiume mzee!! Ukihitaji msaada zaidi njoo pm
Watoto lazima watajua maana hapa ndoa hakuna tena. Hata mie nikipotezea, mke wangu hawezi kukaa tena pale. Katoka akiwa amechanganyikiwa na ataogopa kukaa pale maana hajui reaction yangu. Najua yuko humu nadhani nae anasoma hii thread kama kweli atapata muda wa kufanya hivyo
 
Haya ,mwaya poleni unajua ukiongea haisadii maana imeshatokea mwombe Mungu akupe nguvu yakuendelea kuishi kunywa maji mengi,fanya mazoezi kula mboga za majani,na vyakula vyakuongeza nguvu basi.
Endelea kuishi kunywa dawa usisahau saa 12 kamili saa sita mchana na,saa nne kila siku
 
Baada ya kugundulika hivyo, wote tulipigwa butwaa na hakujua ni nini kitaendelea. Kakurupuka na kurudi Dar japo sijui kama kweli karud huko. Nampigia anapoke lkn analia na hatusikilizani vyema
Mkuu umeishi zaidi ya nusu karne unajuaje mama ana huo ugonjwa ulipohamia dodoma tu? ukute mmeishi miaka na hali hiyo, mimi ntakushauri kitu kimoja, liendee hilo jambo vyema na usimpanikishe kwanza jaribu kumtafuta umwambie wewe umelipokea ili ashushe presha, halafu baada ya hapo utatizama moyo wako unamili wapi.
 
Mimi ni mfanyakazi wa Serikali na ni mtumishi wa muda mrefu nimebakiza miaka mitatu kustaafu. Mkewe wangu nae ni mfanyakazi wa Serikali ila yeye alibaki Dar. Tumetenganishwa kwa nguvu na hili la Dodoma. Tumebahatika kupata watoto.

Baadhi ya watoto wetu wako kwenye ndoa na wengine wako vyuoni nasi. Mke wangu bado ana miaka 13 kazini kabla ya kustaafu. Majuzi amenitembelea hapa Dodoma, alifika akiwa anajisikia vibaya na tukafanya utaratibu wa kwenda hospital. Tulikutana na Dr mstaarabu na akatushauri tupime Ukimwi kwa pamoja.

Majibu yalitoka na mke wangu akiwa Chanya + tulipima tena hospital nyingine na bado ilibaki vilevile. Sasa nabaki najiuliza, jamii itatuelewaje? Watoto watatuelewaje? Wakwe watatuelewaje? Nimekata tamaa na nimebaki bila majibu.

Jamani wenzangu mkae mkijua kuwa hili limetokea kwangu, ukweli wenyewe wengi mko kwenye maisha hayo. Serikali imefanya makosa makubwa sana kutenganisha ndoa za watu kwa makusudi. Watoto wengi walioko mitaani hawana maadili kwa kukosa malezi ya baba na mama.

Hapa tunajenga taifa au tunabomoa. Nimebaki njia panda. Nimfukuze? Nimuue? Au nifanyeje. Huu ni utumishi Serikalini au ni utumwa serikalini. Nimeshindwa kula hata kazini sijaenda. Mke wangu karudi Dar nae sijui anaenda kujiua!

Mbali na lawama kwa mke wangu bado zigo la lawama nawatupia Serikali kwa kukatisha ndoa yangu na pengine itakatisha maisha ya mke wangu aliyeondoka kwa kuchanganyikiwa. Hili la Dodoma linaonekana kama masihara lakini ni janga kubwa sana. Tumejichimbia kaburi kimzaha.
Ungemuhamisha mzee,watu mna umri mkubwa mnashindwaje kuongozana na watoto wote mmeshasomesha na ni wakubwa
 
Back
Top Bottom