Kasheshe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 4,694
- 787
Kazi kweli kweli!!!!
Kamata hiyo !!!!
==================================================
Hokororo: Serikali ina mgogoro na Mwananchi
Salim Said
MKURUGENZI msaidizi wa Maelezo, Raphael Hokororo ameieleza Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii kuwa, serikali ina mgogoro na kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti, kuhusu umiliki wake.
Akizungumza kwenye semina ya kamati hiyo iliyofanyika ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Hokororo alisema serikali ina mgogoro na kampuni hiyo kwa vile inamilikiwa kwa kiasi kikubwa na wageni, kitu ambacho alisema hakitakiwi.
Hokororo, ambaye alikuwa akichangia suala la ukamilishwaji wa sheria mpya ya habari, ambayo pia inazungumzia umiliki wa vyombo vya habari, alisema sheria inataka wageni wasimiliki chombo cha habari kwa zaidi ya asilimia 50, lakini kampuni ya Mwananchi inamilikiwa na wageni kwa asilimia 60.
"Tumebaini kuwa mwekezaji wa kigeni anamiliki hisa nyingi zaidi kuliko mzawa mzalendo," alisema mkurugenzi huyo.
Wageni wanamiliki hisa nyingi zaidi ya asilimia 60 kuliko mzawa na hii ni kwa sababu wazawa waliokuwa na hisa katika kampuni hiyo waliamua kuuza hisa zao kwa wageni. Kutokana na hali hiyo, gazeti la Kingereza la The Citizen linalochapishwa na kampuni hiyo, linahaririwa jijini Nairobi Kenya na kuchapwa Tanzania, lakini wenyewe hawaoni taabu. Jambo hili hatukubaliani nalo."
Gazeti la Kingereza la TheCitizen linalochapishwa na kampuni ya mwananchi linahaririwa jijini Nairobi Kenya na kuchapwa Tanzania na wala wenyewe hawaoni tabu, alisistiza.
Hata hivyo, sheria inayounda tume huru ya ushindani wa kibiashara nchini inamruhusu mwekezaji wa kigeni kumiliki hata asilimia 98 ya hisa katika kiwanda chochote nchini, ingawa sera ya habari inataka wageni wasimiliki chombo cha habari kwa zaidi ya asilimia 50.
Akizungumzia kauli hiyo, Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Mwananchi, Theophil Makunga alisema amesikitishwa na kauli hiyo ya mwandishi huyo mkongwe, akisema kuwa mzungumzaji huyo anatoka ofisi ya msajili wa magazeti na anajua usajili wa The Citizen ulivyo.
Alisema taarifa hizo ni za kusikitisha kwa kuwa hazina ukweli wowote kutokana na ukweli kuwa, gazeti hilo liko mikononi mwa Watanzania ambao ni wazawa.
Alisisitiza kuwa gazeti la The Citizen si tu kwamba halihaririwi Nairobi, bali hata mhariri wake mtendaji, mhariri wa habari, msanifu mkuu, wahariri wengine na waandishi wote ni Watanzania na kazi zote za kuandaa, kuhariri na kuchapa gazeti hilo zinafanyika Dar es Salaam.
Kuhusu muswada wa sheria ya habari, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera alisema marekebisho ya sheria hiyo namba tatu ya mwaka 1976 ya magazeti ipo jikoni na itawasilishwa bungeni kujadiliwa wakati wowote itakapokamilika.
Akihitimisha semina ya kamati hiyo ya bunge, Bendera alisema: Kwa sasa rasimu iko jikoni inachapwa kwa wataalamu wa ICT na ikimaliza hapo itapelekwa wizarani na baadaye bungeni kwa ajili ya kujadiliwa na hatimaye kupitishwa kama sheria.
Alisema vyombo vya habari ni kama bomu na kwamba kama umakini hautakuwepo katika marekebisho ya sheria hiyo, nchi haitatawalika.
"Hebu tuangalie nchi za Rwanda na Burundi, mauaji yote ya kimbari yaliyotokea ni kazi ya vyombo vya habari tu. Hivyo tusipokuwa makini wabunge nchi haitatawalika," alisema.
Alisistiza kuwa wao wabunge kwa kuwa wana dhamana kubwa kwa wananchi, hawapaswi kuachia mambo nyeti yaende ovyo ovyo kwa kuwa wakifanya hivyo nchi haitatawalika.
"Najua kuwa sheria hii imepitwa na wakati na ndio maana tunataka kuileta bungeni ijadiliwe. Lakini kuna watu wanataka tupigane, hivyo tumieni busara zenu ili sheria hii iweze kuwa nzuri," alisisitiza Bendera.
Miongoni mwa mambo yaliyo kwenye sheria hiyo ni uanzishwaji wa baraza la habari la serikali, ambalo linapingwa na wadau wa habari kwa kuwa wanaliona halitakuwa huru kama lilivyo baraza la sasa. Pia sheria hiyo inazungumzia kuwepo kwa viwango vya elimu kwa waandishi, na umiliki wa vyombo vya habari.
Wadau wa habari pia wanadai kuwa hawakushirikishwa katika kuandaa muswaada huo na hivyo wanauona kuwa utazaa sheria ambayo itaendeleza mapungufu yaliyo kwenye sheria ya sasa.
Katibu mkuu wizara hiyo, Dk Florens Turuka aliridhia kufanyika kwa vikao vya ziada baina ya wabunge wa kamati, serikali na wadau wa habari lakini akataka kusiwe na shinikizo kutoka kwa wadau na wanaharakati.
"Tutakaa na kuangalia vipengele vyote vilivyo na udhaifu halafu tutavijadili na kuvirekebisha, kikiwemo hichi cha nguvu ya waziri," alisema Dk Turuka.
Kaimu mwenyekiti wa kamati hiyo ya bunge ya Maendeleo ya Jamii, Haroub Said (Mbunge) alisisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wadau katika kujadili marekebisho ya sheria hiyo.
"Hatujakaa na serikali na wadau kujadili na kutoa mapendekezo ya sheria hii... ikiwa tutakutana hakutakuwa na mashaka... wala serikali isiwe na wasiwasi lakini kama itapelekwa bungeni bila ya kuwashirikisha wadau tutakuwa hatujawatendea haki," alisisitiza.
Kama idara haina fedha ya kufanya vikao hivyo, basi mkurugenzi aandae bajeti kwa katibu wa kamati hii na yeye atajua ni jinsi gani ya kupata fedha za kufanyia vikao na wadau.
Naye mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo), Habib Nyundo alikiri kuwepo kwa upungufu na changamoto katika sheria hiyo na kuongeza kwamba kuna haja kubwa ya kuifanyia marekebisho.
Alisema sheria hiyo haiweki utaratibu wa kutekeleza maelekezo ya Ibara ya 18 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977.
"Sheria pia haifafanui mambo kadhaa muhimu yanayohitajika katika uendeshaji wa sekta nzima ya habari nchini," alisema Nyundo.
Nyundo alisema changamoto nyingine inayowakabili ni kuwa sheria hiyo haipendwi hata kidogo na wadau wa habari nchini, hususan vyombo vya habari.
"Vyombo vya habari haviitaki kabisa sheria namba 3 ya 1976 kwa sababu vinadai serikali imepewa uwezo mkubwa wa kuviingilia, kuvifungia na hata kuchukua mali zao pindi vinapokosea," alisema. Semina hiyo inaendelea tena leo kwenye ukumbi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora uliopo jijini hapa.
Kamata hiyo !!!!
==================================================
Hokororo: Serikali ina mgogoro na Mwananchi
Salim Said
MKURUGENZI msaidizi wa Maelezo, Raphael Hokororo ameieleza Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii kuwa, serikali ina mgogoro na kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti, kuhusu umiliki wake.
Akizungumza kwenye semina ya kamati hiyo iliyofanyika ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Hokororo alisema serikali ina mgogoro na kampuni hiyo kwa vile inamilikiwa kwa kiasi kikubwa na wageni, kitu ambacho alisema hakitakiwi.
Hokororo, ambaye alikuwa akichangia suala la ukamilishwaji wa sheria mpya ya habari, ambayo pia inazungumzia umiliki wa vyombo vya habari, alisema sheria inataka wageni wasimiliki chombo cha habari kwa zaidi ya asilimia 50, lakini kampuni ya Mwananchi inamilikiwa na wageni kwa asilimia 60.
"Tumebaini kuwa mwekezaji wa kigeni anamiliki hisa nyingi zaidi kuliko mzawa mzalendo," alisema mkurugenzi huyo.
Wageni wanamiliki hisa nyingi zaidi ya asilimia 60 kuliko mzawa na hii ni kwa sababu wazawa waliokuwa na hisa katika kampuni hiyo waliamua kuuza hisa zao kwa wageni. Kutokana na hali hiyo, gazeti la Kingereza la The Citizen linalochapishwa na kampuni hiyo, linahaririwa jijini Nairobi Kenya na kuchapwa Tanzania, lakini wenyewe hawaoni taabu. Jambo hili hatukubaliani nalo."
Gazeti la Kingereza la TheCitizen linalochapishwa na kampuni ya mwananchi linahaririwa jijini Nairobi Kenya na kuchapwa Tanzania na wala wenyewe hawaoni tabu, alisistiza.
Hata hivyo, sheria inayounda tume huru ya ushindani wa kibiashara nchini inamruhusu mwekezaji wa kigeni kumiliki hata asilimia 98 ya hisa katika kiwanda chochote nchini, ingawa sera ya habari inataka wageni wasimiliki chombo cha habari kwa zaidi ya asilimia 50.
Akizungumzia kauli hiyo, Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Mwananchi, Theophil Makunga alisema amesikitishwa na kauli hiyo ya mwandishi huyo mkongwe, akisema kuwa mzungumzaji huyo anatoka ofisi ya msajili wa magazeti na anajua usajili wa The Citizen ulivyo.
Alisema taarifa hizo ni za kusikitisha kwa kuwa hazina ukweli wowote kutokana na ukweli kuwa, gazeti hilo liko mikononi mwa Watanzania ambao ni wazawa.
Alisisitiza kuwa gazeti la The Citizen si tu kwamba halihaririwi Nairobi, bali hata mhariri wake mtendaji, mhariri wa habari, msanifu mkuu, wahariri wengine na waandishi wote ni Watanzania na kazi zote za kuandaa, kuhariri na kuchapa gazeti hilo zinafanyika Dar es Salaam.
Kuhusu muswada wa sheria ya habari, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera alisema marekebisho ya sheria hiyo namba tatu ya mwaka 1976 ya magazeti ipo jikoni na itawasilishwa bungeni kujadiliwa wakati wowote itakapokamilika.
Akihitimisha semina ya kamati hiyo ya bunge, Bendera alisema: Kwa sasa rasimu iko jikoni inachapwa kwa wataalamu wa ICT na ikimaliza hapo itapelekwa wizarani na baadaye bungeni kwa ajili ya kujadiliwa na hatimaye kupitishwa kama sheria.
Alisema vyombo vya habari ni kama bomu na kwamba kama umakini hautakuwepo katika marekebisho ya sheria hiyo, nchi haitatawalika.
"Hebu tuangalie nchi za Rwanda na Burundi, mauaji yote ya kimbari yaliyotokea ni kazi ya vyombo vya habari tu. Hivyo tusipokuwa makini wabunge nchi haitatawalika," alisema.
Alisistiza kuwa wao wabunge kwa kuwa wana dhamana kubwa kwa wananchi, hawapaswi kuachia mambo nyeti yaende ovyo ovyo kwa kuwa wakifanya hivyo nchi haitatawalika.
"Najua kuwa sheria hii imepitwa na wakati na ndio maana tunataka kuileta bungeni ijadiliwe. Lakini kuna watu wanataka tupigane, hivyo tumieni busara zenu ili sheria hii iweze kuwa nzuri," alisisitiza Bendera.
Miongoni mwa mambo yaliyo kwenye sheria hiyo ni uanzishwaji wa baraza la habari la serikali, ambalo linapingwa na wadau wa habari kwa kuwa wanaliona halitakuwa huru kama lilivyo baraza la sasa. Pia sheria hiyo inazungumzia kuwepo kwa viwango vya elimu kwa waandishi, na umiliki wa vyombo vya habari.
Wadau wa habari pia wanadai kuwa hawakushirikishwa katika kuandaa muswaada huo na hivyo wanauona kuwa utazaa sheria ambayo itaendeleza mapungufu yaliyo kwenye sheria ya sasa.
Katibu mkuu wizara hiyo, Dk Florens Turuka aliridhia kufanyika kwa vikao vya ziada baina ya wabunge wa kamati, serikali na wadau wa habari lakini akataka kusiwe na shinikizo kutoka kwa wadau na wanaharakati.
"Tutakaa na kuangalia vipengele vyote vilivyo na udhaifu halafu tutavijadili na kuvirekebisha, kikiwemo hichi cha nguvu ya waziri," alisema Dk Turuka.
Kaimu mwenyekiti wa kamati hiyo ya bunge ya Maendeleo ya Jamii, Haroub Said (Mbunge) alisisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wadau katika kujadili marekebisho ya sheria hiyo.
"Hatujakaa na serikali na wadau kujadili na kutoa mapendekezo ya sheria hii... ikiwa tutakutana hakutakuwa na mashaka... wala serikali isiwe na wasiwasi lakini kama itapelekwa bungeni bila ya kuwashirikisha wadau tutakuwa hatujawatendea haki," alisisitiza.
Kama idara haina fedha ya kufanya vikao hivyo, basi mkurugenzi aandae bajeti kwa katibu wa kamati hii na yeye atajua ni jinsi gani ya kupata fedha za kufanyia vikao na wadau.
Naye mkurugenzi msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo), Habib Nyundo alikiri kuwepo kwa upungufu na changamoto katika sheria hiyo na kuongeza kwamba kuna haja kubwa ya kuifanyia marekebisho.
Alisema sheria hiyo haiweki utaratibu wa kutekeleza maelekezo ya Ibara ya 18 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977.
"Sheria pia haifafanui mambo kadhaa muhimu yanayohitajika katika uendeshaji wa sekta nzima ya habari nchini," alisema Nyundo.
Nyundo alisema changamoto nyingine inayowakabili ni kuwa sheria hiyo haipendwi hata kidogo na wadau wa habari nchini, hususan vyombo vya habari.
"Vyombo vya habari haviitaki kabisa sheria namba 3 ya 1976 kwa sababu vinadai serikali imepewa uwezo mkubwa wa kuviingilia, kuvifungia na hata kuchukua mali zao pindi vinapokosea," alisema. Semina hiyo inaendelea tena leo kwenye ukumbi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora uliopo jijini hapa.