Serikali imevifuta Vituo vyote vya huduma za Afya ya VVU na UKIMWI kwa watu wa makundi maalumu

asubuhi sana

JF-Expert Member
Mar 18, 2015
1,666
1,402
Serikali kupitia Wizara Ya Afya imevifuta Vituo vyote vinavyotoa huduma za Afya ya VVU Na Ukimwi kwa Makundi Maalum baada ya kubainika kwamba Vituo hivyo vinahusika na kuhamasisha Mapenzi ya Jinsia Moja na Ushoga.



Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari

SOURCE; Muungwana blog

========

Ufafanuzi Kuhusu Kufutwa Vituo vya Huduma za VVU na UKIMWI

1. Ifahamike kuwa tuna Vituo vya Kutoa huduma za VVU na UKIMWI takribani 4,737 katika ngazi na Halmashauri mbalimbali nchini. Hivi vinaendelea kutoa huduma ikiwa ni pamoja na huduma za kitabibu (Bio-Medical interventions); Huduma za mabadiliko ya Kitabia (Behavioural Interventions) na Huduma za kuwajengea utengamano na za kiuchumi wenye maambukizi ya VVU

2. Tumefuta Utaratibu wa kutoa huduma za VVU na UKIMWI kwa Makundi Maalum kupitia Vituo Maalum (Drop In Centres). Na Vituo hivi havizidi 40 nchi nzima. Huduma zitatolewa katika Vituo vya kutolea Huduma za afya. Na pale itakapolazimu huduma za mkoba (Outreach services) kwa kutumia watoa huduma za afya itatolewa.

3. Serikali imeweza kupata ushahidi wa kina kuwa Vituo hivi vingi (Drop In Centres) vimekuwa vikitumika kuraghibisha (promote) vitendo vya mapenzi ya Jinsia moja, jambo ambalo ni kinyume na Sheria za Nchi.

4. Nimeagiza Mamlaka zote za Utoaji huduma za Afya kuhakikisha Huduma za VVU na UKIMWI zinapatikana kwa mtu yoyote nchini bila Ubaguzi wa aina yoyote kwa kuwa ubaguzi katika utoaji wa huduma za afya ni kinyume cha Sheria na Sera za nchi.

Ummy Mwalimu
WAMJW
16 Feb. 2017
 
Serikali imevifuta Vituo vyote vya huduma za Afya ya VVU Na Ukimwi

Serikali kupitia Wizara Ya Afya imevifuta Vituo vyote vinavyotoa huduma za Afya ya VVU Na Ukimwi kwa Makundi Maalum baada ya kubainika kwamba Vituo hivyo vinahusika na kuhamasisha Mapenzi ya Jinsia Moja na Ushoga.

Kitu chochote kibaya huwa kinafichwa na neno zuri ili kionekane kizuri. Makundi maalum in short ni mashoga.

Waziri wa afya amefanya jambo la maana, japo watakuja hapa watetezi wa haki za binadamu kulalamika.

Mwanaume au mwanamke anapoamua kuwa shoga/msagaji, anafanya hicho kitendo chumbani kwake au mafichoni. Huhitaji kumtafuta na kumpa mafuta laini kwa vyovyote vile. Kumtafuta na kumpa mafuta laini ni kukuza na kulibariki hilo jambo.
 
Serikali imevifuta Vituo vyote vya huduma za Afya ya VVU Na Ukimwi

Serikali kupitia Wizara Ya Afya imevifuta Vituo vyote vinavyotoa huduma za Afya ya VVU Na Ukimwi kwa Makundi Maalum baada ya kubainika kwamba Vituo hivyo vinahusika na kuhamasisha Mapenzi ya Jinsia Moja na Ushoga.


=============================================================

Serikali kupitia Wizara Ya Afya imevifuta Vituo vyote vinavyotoa huduma za Afya ya VVU Na Ukimwi kwa Makundi Maalum baada ya kubainika kwamba Vituo hivyo vinahusika na kuhamasisha Mapenzi ya Jinsia Moja na Ushoga.

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari

SOURCE; Muungwana blog
Inamaana "mashoga tu ndo walengwa na huduma za vitio hivyo!"..na "nini uwiano kati ya mashoga na waathirika?"..tone moja,lisichafue bahari nzima.
 
Naona hawa watu wanaendelea kuongeza matatizo, bora wangesema lingine lakini si hili la kupromote ushoga!
 
Dunia sasa hivi ina SDG's 17 (Sustainable Development Goals 2015-2030), moja kati ya hizo goals ni "kuhakikisha watu wote wa rika zote wana maisha yenye afya nzuri na ustawi mzuri". Jambo hili lilikuwa linachangia kwa kiasi kikubwa kulifikia lengo hilo tajwa kati ya hayo 17. Kwa uamuzi huu naona kama tuko kinyume na hilo lengo sasa. Kwa mtazamo wangu lakini. Vipo vituo vinavyosaidia waathirika kweli wasi generalize.
Samahani kwa kuchanganya lugha.
 
Back
Top Bottom