Serikali imetulia vijana wanapoteza fursa, nasi tuandikie US kuomba ushahidi wa Makonda ili hatua zichukuliwe?

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,798
71,218
Tuhuma nzito hadi hatua zimechukuliwa serikali kimya tuu. Hatua hizo kama zingemhusu Makonda na mkewe pekee tungesema potelea mbali, lakini zimegusa hadi vijana wetu waliokuwa wanafaidika na bahati nasibu ya Visa katika utafutaji wao wa maisha huko nje.

Hivi maofisa wengine wa serikali hawawezi kuchukuwa hatua zozote kama jambo litamhusu Makonda kwa sababu ni "mpendwa" wa Rais?

Maana hasa hizo tuhuma zinazohusu kupoteza maisha zinasubiri waambiwe na Rais fuatilieni? Au wanaamini kila afanyacho Makonda kina ruhusa ya ofisi kuu?

Nadhani sasa kwa vile mtu binafsi kama Msando kaandikia "American Embassy" kupinga jambo hilo, basi kwa sasa taasisi za haki za binadamu na kidemokrasia vikiwemo vyama vya Siasa viandike navyo barua kwa "The Embassy of United States of America" kuomba watoe Ushahidi walio nao kuwa Makonda ameshiriki vitendo vya kuondoa haki ya kuishi watu kadhaa.

Usije kuta USA wanatukosanisha bure wakati Makonda ni kijana mwema na mfano wa kuigwa na wengine kwa utakatifu wake.

Na serikali yetu 'sikivu' inalijua hilo hata mpendwa Rais wetu kipenzi cha 'wanyonge' anatambua utendaji uliotukuta wa kijana huyu.

Tushinikize taasisi hizo ziandike hizo barua ili US watoe Ushahidi wao na kama ni 'fake' waumbuke.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama vyama vya upinzani na NGOs zina ushahidi si wautoe hadharani, ukiwaandikia US embassy ni kama unajiuza kwao wakuone una maana, kama una ushahidi toa mbele ya watz hao ndio wenye nchi na ndio waamuzi wa mwisho, acheni kuwa manyumbu.
 
Chakaza,
Nilisema kuwa miaka 5 ya kwanza ya JPM ni shule yake ya Urais na mitano ijayo mambo yatakuwa mazuri. Umeona anavyohandle haya masuala sasa kiutu uzima. Jana amewakata chenga ya mwili kwa kunyamaza, mlitegemea afyatuke mpate ajenda!

Katika utawala si kila jambo linatangazwa hadharani. Kuhusu Makonda sidhani ni wakati sahihi wa kumuajibisha ni bora akavuta pumzi la sivyo mtapata ajenda pia. JPM hakika ameanza kukomaa the hardway. Pole sana wapenda kwenda Ikulu kutotumia sanduku la Kura na sasa ACT inawapiku kiulaini
 
Hebu tupambane na maendeleo tuache kujipendekeza.
Kama unaona Tanzania hakuna demokrasia hamia USA au Ubelgiji ukale raha
Maendeleo wakati kuna tuhuma za mauaji? Au unazichukulia rahisi kwa vile waliohusika huna undugu nao?
Hahami mtu hapa katika nchi aliyopewa na Mungu, ila ni kuhakikisha aliyepoteza maisha ya mtu naye yake yanakumbana na sheria

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marekani walichosema ni ukweli mtupu na si kwamba watanzania walikua hawajui, bashite anavyotishia watu usiku kucha na anapeta utasema ana-own nchi, yeye na jiwe genge moja tu. Wanyonge wanampenda kweli sababu vilaza, ndiyo maana wanaitwa wanyonge, anajua kuwacontrol vizuri.
 
Tuhuma nzito hadi hatua zimechukuliwa serikali kimya tuu. Hatua hizo kama zingemhusu Makonda na mkewe pekee tungesema potelea mbali, lakini zimegusa hadi vijana wetu waliokuwa wanafaidika na bahati nasibu ya Visa katika utafutaji wao wa maisha huko nje.

Hivi maofisa wengine wa serikali hawawezi kuchukuwa hatua zozote kama jambo litamhusu Makonda kwa sababu ni "mpendwa" wa Rais?

Maana hasa hizo tuhuma zinazohusu kupoteza maisha zinasubiri waambiwe na Rais fuatilieni? Au wanaamini kila afanyacho Makonda kina ruhusa ya ofisi kuu?

Nadhani sasa kwa vile mtu binafsi kama Msando kaandikia "American Embassy" kupinga jambo hilo, basi kwa sasa taasisi za haki za binadamu na kidemokrasia vikiwemo vyama vya Siasa viandike navyo barua kwa "The Embassy of United States of America" kuomba watoe Ushahidi walio nao kuwa Makonda ameshiriki vitendo vya kuondoa haki ya kuishi watu kadhaa.

Usije kuta USA wanatukosanisha bure wakati Makonda ni kijana mwema na mfano wa kuigwa na wengine kwa utakatifu wake.

Na serikali yetu 'sikivu' inalijua hilo hata mpendwa Rais wetu kipenzi cha 'wanyonge' anatambua utendaji uliotukuta wa kijana huyu.

Tushinikize taasisi hizo ziandike hizo barua ili US watoe Ushahidi wao na kama ni 'fake' waumbuke.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mbili

 
Back
Top Bottom