Serikali imemtenga Brg Gen Balele

Serikali imemtenga Brg Gen Balele

Bururu

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2016
Posts
877
Reaction score
585
Pamoja na kuitumikia Serikali kwa muda mrefu, kupigana vita Uganga, Kutibu wagonjwa Mashuhuri ktk Hospital ya Kijeshi Lugalo, Kubadilisha Elimu Mkoa wa Shinyanga, Kuisimamia Simiyu mpaka kuwa Mkoa, lakini Serikali ya awamu ya 4 haikuona hayo yote na Serikali ya awamu ya 5 pia kuendelea na ‘Ban’ kwa huyu muheshimiwa.

Kweli tenda wema nenda zako, wanafiki ndio wajaliwao.

Inasikitisha sana.
 
Kama anachapa kazi hajui kutoa matamko na sio mwingi wa maneno aendelee tu kusubiri awamu nyingine.
 
Siku hizi JF tuna shida kubwa; sasa hapa ndio umesema nini kwa hadhira yako?

Mnatupa wakati mgumu kuelewa mmeandika kitu gani.

Yes 4 stars General Balele amewahi kuwa Dr. huko Lugalo na pia kuwa Mkuu wa Mikoa fulani.

Hizo ni facts sasa kusema sijui katengwa mbona hujasema katengwa ki vipi? Hapati haki zake au ni nini?
 
Mkuu mbna una mseMEa sana huyu mzee????ni nani yako??? maana UZI nyingi sana hapa JF kuhusu huyu mzee ni wewe ndiye unaezileta hapa...KULIKONI????
 
Vipi kamanda, Brigedia kakulalamikia nn umeamua uwasilishe Ujumbe hapa??? Ifike mahali tuwe na kiasi, kwenye taifa la watu mil.48 ukitaka ww utumike hadi kufa kuna wengine watakufa unused na mwisho wataenda kuulizwa walitumiaje talanta zao...
 
Alokwambia wana kumbuka ni nani? Tenda wema
 
Kuna mzee mmoja pia ni Marehemu wa Arusha Kijenge alikuwa jeshini anaitwa Balele ni ndugu hawa
 
Mwenye uzi inaonekana unengea Direct Coded Message kwa mtu fulani. Hata sisi tukichagia ni kama tunaingikia maongezi binafsi.
 
kwani nini maana ya kustaafu?mbona hata sisi wazazi wetu pamoja na kutoa mchango mkubwa kwa taifa lkn hakuna anaewakumbuka baada ya kustaafu?
 
Vipi kamanda, Brigedia kakulalamikia nn umeamua uwasilishe Ujumbe hapa??? Ifike mahali tuwe na kiasi, kwenye taifa la watu mil.48 ukitaka ww utumike hadi kufa kuna wengine watakufa unused na mwisho wataenda kuulizwa walitumiaje talanta zao...
Sina mengi ya kuongea sababu ulichokisema umeniwakilisha nami kwanza utengwaji hajauweka wazi kwa kweli tuna shida sana na uwasilishaji wa vitu haihitaji uwe mwandishi ndio utoe khabari nzuri kwa mada kama hii
 
Siku hizi JF tuna shida kubwa; sasa hapa ndio umesema nini kwa hadhira yako? Mnatupa wakati mgumu kuelewa mmeandika kitu gani. Yes 4 stars General Balele amewahi kuwa Dr. huko Lugalo na pia kuwa Mkuu wa Mikoa fulani. Hizo ni facts sasa kusema sijui katengwa mbona hujasema katengwa ki vipi? Hapati haki zake au ni nini?

Mkuu Kimbunga nadhani umeteleza kama Balele alikuwa Brg Gen basi ni one star general si four star Gen.Brg Gen ni one star Gen,Major Gen ni two star Gen,Lt Gen ni three star Gen na General ni four star Gen.Hapa Tanzania four star General ni wakuu wa majeshi CDF,four star General ambaye hakuwa CDF ni General Tumainiel Kiwelu huyu alikuwa Chief of Staff wenzake wote waliishia three star General (Lt General).
 
Back
Top Bottom