Pundamilia07
JF-Expert Member
- Oct 29, 2007
- 1,439
- 53
Coaster, DCM nazo kuondolewa Dar
2008-09-12 11:18:07
Na Richard Makore
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), inatarajia kubadili mfumo wa usafiri kwa mabasi ya abiria (daladala) jijini Dar es Salaam kutoka kwa umiliki wa mtu mmoja mmoja kuwa wa makampuni makubwa binafsi na ya umma na kuondoa magari yote yanayobeba abiria chini ya 65.
Hatua hiyo ilitangazwa jana na Ofisa Mfawidhi wa Sumatra Kanda ya Mashariki, Walukani Luhamba, alipokuwa akizungumza na Nipashe.
Alisema baada ya mfumo huo kukamilika, Jiji la Dar es Salaam litakuwa na huduma safi na bora za usafiri kama zipatikanazo nchini Japan.
Aliishauri serikali kulifufua Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), ili liweze kuingia katika biashara hiyo kusaidiana na makampuni binafsi yatakayojitokeza.
Alisema, UDA bado ni shirika zuri na kinachotakiwa kufanywa na serikali ni kuwachukulia hatua za kisheria viongozi wake waliohusika kuliua na wale wanaoendelea kulimalizia.
Luhamba alisema mchakato wa kusajili makampuni hayo utaanza baada ya miezi sita ijayo, ambapo muombaji atatakiwa kutuma maombi maalum ya kutaka kutoa huduma ya usafiri jijini.
Aliongeza kuwa Sumatra imeweka utaratibu mzuri ambapo kila kampuni itakayojitokeza itapewa barabara yake kwa ajili ya kupitisha magari itakayokuwa nayo.
Alitaja baadhi ya barabara zitakazokabidhiwa kwa kampuni hizo kuwa ni pamoja na zile za Morogoro, Ali Hassan Mwinyi, Nyerere na kwamba kila kampuni haitaingilia barabara ya mwenzake.
Kuhusu umiliki wa mtu mmoja mmoja anayemiliki daladala alisema, atatakiwa kuingia mkataba na kampuni kubwa husika na hivyo kukabidhi gari lake huko.
Sumatra jana ilirudia kauli yake kuwa mabasi madogo maarufu kama \'vipanya\' hayatapata usajili pamoja na magari yote yaliyotengenezwa kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita.
Ofisa huyo alisema katika kuboresha usafiri hapa jijini wamesajili magari makubwa 3,000 na kwamba hali hiyo imepunguza foleni wakati wa asubuhi na jioni.
Aidha, alisema kila siku mabasi madogo 15 yanaondolewa katika mfumo wa kutoa huduma ya usafiri na yatazuiwa kuingia katikati ya Jiji.
Alifafanua kuwa baada ya mchakato wa kupata makampuni makubwa ya mabasi, mabasi aina ya Coaster na DCM nayo yataondolewa na kubakiza magari makubwa yenye uwezo wa kuchukua abiria zaidi ya 65 kwa wakati mmoja.
Alifafanisha hali ya usafiri Dar es Salaam, kwamba itakavyokuwa kama Japan, nchi ambayo ina magari mazuri na makubwa na kwamba hilo linawezekana.
Wadau,
Huyu ofisa aliyekaririwa hapo juu ameongea hayu kama maoni yake binafsi au maoni ya serikali?
Je, ni lini serikali itajitoa katika kufanya biashara? Leo hii bado kuna ofisa wa serikali anaongelea kufufua UDA?
Leo bado kuna ofisa wa serikali bado anaongelea kuleta kampuni kubwa badala ya kuwajengea uwezo wananchi waendelee kutoa huduma kwa maana ya kujijengea uwezo wa kiujasiriamali? Huyu ofisa anakwenda mbali na kuonesha kuwa maamuzi yamekwisha tolewa kuwa kila mwenye gari lake akalikabidhi kwa kampuni kubwa.
Iko haja atuelezee hayo mawazo ameyapata wapi? na pili huenda anamjua huyu mwenye kampuni kubwa, kuna kaharufu hapa?
2008-09-12 11:18:07
Na Richard Makore
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), inatarajia kubadili mfumo wa usafiri kwa mabasi ya abiria (daladala) jijini Dar es Salaam kutoka kwa umiliki wa mtu mmoja mmoja kuwa wa makampuni makubwa binafsi na ya umma na kuondoa magari yote yanayobeba abiria chini ya 65.
Hatua hiyo ilitangazwa jana na Ofisa Mfawidhi wa Sumatra Kanda ya Mashariki, Walukani Luhamba, alipokuwa akizungumza na Nipashe.
Alisema baada ya mfumo huo kukamilika, Jiji la Dar es Salaam litakuwa na huduma safi na bora za usafiri kama zipatikanazo nchini Japan.
Aliishauri serikali kulifufua Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), ili liweze kuingia katika biashara hiyo kusaidiana na makampuni binafsi yatakayojitokeza.
Alisema, UDA bado ni shirika zuri na kinachotakiwa kufanywa na serikali ni kuwachukulia hatua za kisheria viongozi wake waliohusika kuliua na wale wanaoendelea kulimalizia.
Luhamba alisema mchakato wa kusajili makampuni hayo utaanza baada ya miezi sita ijayo, ambapo muombaji atatakiwa kutuma maombi maalum ya kutaka kutoa huduma ya usafiri jijini.
Aliongeza kuwa Sumatra imeweka utaratibu mzuri ambapo kila kampuni itakayojitokeza itapewa barabara yake kwa ajili ya kupitisha magari itakayokuwa nayo.
Alitaja baadhi ya barabara zitakazokabidhiwa kwa kampuni hizo kuwa ni pamoja na zile za Morogoro, Ali Hassan Mwinyi, Nyerere na kwamba kila kampuni haitaingilia barabara ya mwenzake.
Kuhusu umiliki wa mtu mmoja mmoja anayemiliki daladala alisema, atatakiwa kuingia mkataba na kampuni kubwa husika na hivyo kukabidhi gari lake huko.
Sumatra jana ilirudia kauli yake kuwa mabasi madogo maarufu kama \'vipanya\' hayatapata usajili pamoja na magari yote yaliyotengenezwa kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita.
Ofisa huyo alisema katika kuboresha usafiri hapa jijini wamesajili magari makubwa 3,000 na kwamba hali hiyo imepunguza foleni wakati wa asubuhi na jioni.
Aidha, alisema kila siku mabasi madogo 15 yanaondolewa katika mfumo wa kutoa huduma ya usafiri na yatazuiwa kuingia katikati ya Jiji.
Alifafanua kuwa baada ya mchakato wa kupata makampuni makubwa ya mabasi, mabasi aina ya Coaster na DCM nayo yataondolewa na kubakiza magari makubwa yenye uwezo wa kuchukua abiria zaidi ya 65 kwa wakati mmoja.
Alifafanisha hali ya usafiri Dar es Salaam, kwamba itakavyokuwa kama Japan, nchi ambayo ina magari mazuri na makubwa na kwamba hilo linawezekana.
Wadau,
Huyu ofisa aliyekaririwa hapo juu ameongea hayu kama maoni yake binafsi au maoni ya serikali?
Je, ni lini serikali itajitoa katika kufanya biashara? Leo hii bado kuna ofisa wa serikali anaongelea kufufua UDA?
Leo bado kuna ofisa wa serikali bado anaongelea kuleta kampuni kubwa badala ya kuwajengea uwezo wananchi waendelee kutoa huduma kwa maana ya kujijengea uwezo wa kiujasiriamali? Huyu ofisa anakwenda mbali na kuonesha kuwa maamuzi yamekwisha tolewa kuwa kila mwenye gari lake akalikabidhi kwa kampuni kubwa.
Iko haja atuelezee hayo mawazo ameyapata wapi? na pili huenda anamjua huyu mwenye kampuni kubwa, kuna kaharufu hapa?