Kila mfanyabiashara ana haki ya kufanya biashara LAKINI kwa utaratibu uliopo sasa wa kuwaruhusu Machinga kuzagaa kila sehemu inaleta simanzi kubwa kwa wafanyabiashara wakubwa.
Mfano hai njoo hapa Mwanza mtaa wa Nyerere panatisha. Mbele ya maduka makubwa yamevamiwa na machinga na kuwanyima wafanyabiashara wanaolipa mapato makubwa, leseni na mapato mengine kupata wateja.
Wafanyabiashara hawa wakubwa hawana pa kusemea lakini wanaumia sana rohoni. Hivi kwa nini Machinga wamepewa uhuru wa kufanya watakalo? Hata sababu kubwa ya Wafanyabiashara wa Kilimanjaro kufunga biashara zao mojawapo ni Machinga.
Nashauri suala hili lifanyiwe utafiti na hata kuwa na kikao cha Wafanyabiashara na Serikali ione tatizo la machinga na kulipatia ufumbuzi.
Mfano hai njoo hapa Mwanza mtaa wa Nyerere panatisha. Mbele ya maduka makubwa yamevamiwa na machinga na kuwanyima wafanyabiashara wanaolipa mapato makubwa, leseni na mapato mengine kupata wateja.
Wafanyabiashara hawa wakubwa hawana pa kusemea lakini wanaumia sana rohoni. Hivi kwa nini Machinga wamepewa uhuru wa kufanya watakalo? Hata sababu kubwa ya Wafanyabiashara wa Kilimanjaro kufunga biashara zao mojawapo ni Machinga.
Nashauri suala hili lifanyiwe utafiti na hata kuwa na kikao cha Wafanyabiashara na Serikali ione tatizo la machinga na kulipatia ufumbuzi.