cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,317
- 7,509
Sisi wananchi tunaitaka serikali isikwepe majukumu yake ya kulinda afya za wananchi wake
Ni wajibu wa serikali kuwa wazi na kuanzisha kampeni ya kupambana na korona awamu ya pili
Tunaitaka serikali kupitia viongozi wa serikali kuu, mitaa, vyombo vya habari na viongozi wa dini kuhamasisha wananchi kuepuka misongamano mfano makanisani, misikitini, makongamano, semina, sehemu za burudani, michezo,na mikusanyiko ya kisiasa
Tunaitaka wizara ya afya iwape miongozo ya kupunguza maambukizi mashabiki wa mpira uwanjani,shuleni na vyuoni
Tunaitaka serikali kupitia wizara ya afya watoe vipeperushi na matangazo ya kutosha namna ya kijikinga na virusi vya korona
Tunaitaka serikali kupitia wizara ya afya kusisitiza uvaaji wa barakoa sehemu zenye misongamano
Wizara ya afya ifanye utafiti wa ugonjwa mpya wa korona waseme kirusi gani kwa sasa kipo nchini kwetu kama ni cha South Africa ama ni cha uingereza au ni kile cha mwanzo ili waweke mbinu na mikakati kwa wananchi ili kupambana nacho
Tunaitaka serikali kuacha mzaha mara moja kwenye afya za watu,na huku watu wanapukutika
Tuwapime watalii na wageni wanaoingia Tanzania ili kupunguza maambukizi mapya, tusipende hela kuliko afya za watu
Mnaangamiza Taifa kwa kukosa uzalendo wa kuwajali watu wengine
Uzalendo ni kuwajali wananchi wako tu,hakuna uzalendo zaidi ya huo
Ni wajibu wa serikali kuwa wazi na kuanzisha kampeni ya kupambana na korona awamu ya pili
Tunaitaka serikali kupitia viongozi wa serikali kuu, mitaa, vyombo vya habari na viongozi wa dini kuhamasisha wananchi kuepuka misongamano mfano makanisani, misikitini, makongamano, semina, sehemu za burudani, michezo,na mikusanyiko ya kisiasa
Tunaitaka wizara ya afya iwape miongozo ya kupunguza maambukizi mashabiki wa mpira uwanjani,shuleni na vyuoni
Tunaitaka serikali kupitia wizara ya afya watoe vipeperushi na matangazo ya kutosha namna ya kijikinga na virusi vya korona
Tunaitaka serikali kupitia wizara ya afya kusisitiza uvaaji wa barakoa sehemu zenye misongamano
Wizara ya afya ifanye utafiti wa ugonjwa mpya wa korona waseme kirusi gani kwa sasa kipo nchini kwetu kama ni cha South Africa ama ni cha uingereza au ni kile cha mwanzo ili waweke mbinu na mikakati kwa wananchi ili kupambana nacho
Tunaitaka serikali kuacha mzaha mara moja kwenye afya za watu,na huku watu wanapukutika
Tuwapime watalii na wageni wanaoingia Tanzania ili kupunguza maambukizi mapya, tusipende hela kuliko afya za watu
Mnaangamiza Taifa kwa kukosa uzalendo wa kuwajali watu wengine
Uzalendo ni kuwajali wananchi wako tu,hakuna uzalendo zaidi ya huo