Serikali iangalie ubora wa vipimo vya hospitali vinaweza kuleta shida kwa wagonjwa

Mchaga Tajiri

Member
Mar 14, 2023
10
16
Sina majibu kamili lakini ni Jambo la kushangaza. Kuna Hali ambayo imekuwa ilijitokeza kwa baadhi hospitali zetu za Serikali na binafsi napata mkanganyo.

Msichana mmoja alikuwa akiumwa sana, alipopelekwa moja ya hospitali aliambiwa kwamba hakuna anachoumwa zaidi ya kumpa Panadol tu. Hali yake iliendelea kuwa mbaya siku hadi siku ikambidi aende hospitali nyingine kupima, alipopima aligundulika kuwa na malaria mbili .Na hii si mara ya kwanza kupatwa na tatizo hili ni mara nyingi.

Unakuta unapima hospitali hii inaonekana una ugonjwa na ukienda nyingine unaambiwa hakuna unachoumwa. Kutokana na hili nilimuuliza mmoja wa daktari akaniambia hiyo ipo kutokana na aina ya vipimo vinavyotumika.

Pamoja na majibu haya aliyonipa daktari nadhani hii inaweza kuwa mbaya kwa wananchi kupoteza uhai Kwa kukosa vipimo sahihi.
 
Back
Top Bottom