Serikali iache blah blah kwa Usalama wa Taifa (National Security)

Serikali iache blah blah kwa Usalama wa Taifa (National Security)

ubongokid

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2017
Posts
2,356
Reaction score
4,626
Kama raia kuna wakti inabidi tuseme ukweli,zaidi ni lazima tuambiane ukweli na tuwaambie viongozi wetu ukweli.
Inakera sana kama taifa tunapewa majibu mepesi kwa maswali magumu bila kujali kwamba kwa kufanya hivo hatupeleki taifa Mbele.

Rafiki yangu Ben Saa Nane aliwahi kuniambia kwamba "We all have a purpose in this world and we must live by the purpose and die by the purpose.Happy is the person who can live for the purpose and die for that purpose"

Nimeamua kuweka maneno hayo rasmi ili watu waelewe kwamba Popote Ben alipo he lived with a purpose and died for that same purpose.Na mpaka leo serikali ya Magufuli haiachukua hatua yoyote ile kuhusu kupote kwa raia wake huyu.Ni aibu kwa srikali kutokujali uhai wa mwananchi wake.Miaka mitatu sasa na serikali imekaa kimya kabisa.Serikali dhaifu sana hii haiwezi kulinda raia wake bali inaoenkana inaweza kuwatisha.

Likaja Sakata la kina Roma Mkatoliki wakwakamata wakawatesa na kuwaachia na mpaka leo hakuna aliyechukuliwa hatua pamoja na ROma kuwa hai na salama.Hii sasa imekuwa ni srikali dhaifu haiwezi kulinda raia ila inaweza kuwafanyia ugaidi.

Yakaa mengi sana na yote hayajawahi kutatuliwa hata Akwilina aliyeuwawa kwa risasi za serikali bado hakupata haki yoyote.Naichukia Serikali yangu kwa kumuua dada yangu Akwilina mbele ya watu na bado kushindwa kumpa HAki.Inafikia wakati natamani Nchemba angevunjika Miguu kwenye ile ajali ile ajue kwamba "Karma is a bitch"

Likaja la Lissu nalo kila siku linazungushwa tu na kukwepwa kufanyiwa kazi.Serikali gani hii tuliyochagua.Serikali isiyo na uwezo wa kuwapatia wananchi haki.Serikal inayotaka Raia wawe waoga?Ole wangu mimi Iwapo niko sahihi

Nawaona viongozi wote kuanzia Rais,Spika na Mahakama wanakula tu kodi za wananchi bila wasiwasi wala kuwajibika na watanzania tumekaa kimya tunawatazama tu.

Ndugu zangu watanzania tunaoishi nyakati hizi.

Historia itatuhukumu tusipochukua hatua.Watoto wetu watashangaa sana kuona kuwe viongozi wetu hawakutimiza wajibu na bado hatukuwawajibisha.Kama ambavyo tunawashangaa wazee wetu waliouza utu wao zamani na sisi tutasemwa kama kizazi cha waoga,wazandiki,wanaojificha nyuma ya keyboard.

Nimemaliza na NImechafukwa

PS.Nasikia yamebaki manyoya huko kwa {Mchina}
CC.Mwakymango
 
ubongokid, Wanaseam wanasubiri Lissu aje na dereva wake, Mbona Roma na Mo wapo na hawajahojiwa na wahusika wa unyama ule hawajakamatwa.

Kitu kimoja wanavhosahau hawa watu wanadhani kutekwa kwa Mo au Roma mambonyaliishia pale. Wametulia tu wanasubiri upenyo na ipo siku waliohusika watakinywea kikombe cha damu ya moto.
 
Wanaseam wanasubiri Lissu aje na dereva wake, Mbona Roma na Mo wapo na hawajahojiwa na wahusika wa unyama ule hawajakamatwa.

Kitu kimoja wanavhosahau hawa watu wanadhani kutekwa kwa Mo au Roma mambonyaliishia pale. Wametulia tu wanasubiri upenyo na ipo siku waliohusika watakinywea kikombe cha damu ya moto.
Shida siku hizi serikali yetu ya Kigang sta.Kila Mtu mbabe hadi mpishi wa Ikulu Mbabe.Ila Sumu yao iko inapikwa watainywa tu.
 
tatazo la nchi hii ni mfumo wa chama kimoja haujawahi kumalizwa, CCM ina ndoa isiyo rasmi na idara nyeti za nchi na kama unavyoona uoga wa watanzania dhidi ya serikali yao ndivyo hata hizo idara nyeti ni waoga hivyohivyo, kuna watu wanaamini kabisa kuwa CCM ikianguka basi utakua mwisho wa uwepo wa nchi na wamejaa huko kwenye hizo idara. Badala ya kuhakikisha vyama vyote viko safi na kuviandaa vizuri ili chochote kiweze kuongoza nchi mijitu imekaa na kudumaza akili ikidhani maisha ni CCM tu, sasa tuna mfumo wa vyama vingi wa nini??? na uwajibikaji utatoka wapi?? mwisho wa siku yanashabikia upuuzi tu, mara ooh tumepata rais mzalendo, nani kakwambia rais mzalendo ndio suluhu?? pumbavu sana hawa watu.
 
Yana mwisho haya ipo siku kitaeleweka tu kwani Libya ilikuwaje na leo ipo vipi? Hakuna amani kwenye uoga huo ni utumwa
 
Serikali dhalimu zote duniani hutayarisha mafuta ya kujikaanga zenyewe ni suala la muda tu
 
Back
Top Bottom