Bubu Msemaovyo
JF-Expert Member
- May 9, 2007
- 4,126
- 3,475
na Lucy Ngowi
SERIKALI imesema kuwa haina uhakika kama wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Manispaa ya Tabora, wamerudishwa nyumbani baada ya shule kufungwa kutokana na wazabuni kusitisha huduma ya chakula katika shule zao.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza, alipokuwa akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake mwishoni mwa wiki iliyopita, juu ya hatima ya wazabuni waliositisha kutoa huduma ya chakula katika shule za sekondari za serikali pamoja na vyuo vya walimu.
Sina hakika kama wanafunzi wako nyumbani, sina hakika na hilo kwa kuwa sijapata taarifa ya kiofisi mezani kwangu, alisema Mahiza.
Kwa maelezo ya naibu waziri huyo, hatima ya wazabuni hao itajulikana baada ya hazina kutoa pesa hizo, kwa kuwa ni haki yao kulipwa.
Alikiri kuwa, wazabuni hao wanaidai serikali sh bilioni tisa na kuongeza kuwa ni wajibu wa serikali kulipa pesa hizo.
Hivi karibuni iliripotiwa kuwa, shule za Manispaa ya Tabora zilifungwa kutokana na wazabuni kusitisha huduma ya chakula, kwa kuwa hawajalipwa madeni yao na serikali kwa muda mrefu.
Baadhi ya wanafunzi walilalamikia kitendo hicho kwa kusema kuwa, kitawaathiri katika mitihani yao waliyokuwa wanatarajia kuifanya siku za karibuni.
Shule hizo ni Kazima, Milambo, Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora na Shule ya Sekondari ya Wasichana Tabora.
Hata hivyo, mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bwiru iliyoko Mwanza, Elia Kisuu, aliwaondoa hofu wazazi ambao watoto wao wanasoma katika shule hiyo, kwa kuwaeleza kuwa, shule yake haina tatizo la chakula na wala haijafungwa.
Bwiru ni moja ya shule ambazo wanafunzi waliozungumza na gazeti hili waliitaja kuwa imefungwa.
Wakati mkuu huyo wa Sekondari ya Bwiru, akitoa kauli hiyo, kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Abeid Mwinyimsa, akihojiwa na Idhaa ya Kiwahili ya BBC, alikiri kuwa hali ni mbaya kwa shule hizo za Mkoa wa Tabora, kwani wazabuni wamesitisha huduma katika shule hizo na kusababisha shule hizo kufungwa.
Taarifa kama hii ukisoma unaelewa kabisa kwamba baadhi ya Mawaziri hawapo "duniani" hivi hata vyombo vya habari tu hawasomi, kama waziri mwenye mamlaka kwanini asichukue simu akapiga kuwasiliana na shule husika ili kuchukua hatua "eti anasubiri taarifa zije ofisini" Hiyo ndiyo ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya? Najihisi bado tupo enzi ya "Mfagio wa Chuma"
SERIKALI imesema kuwa haina uhakika kama wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Manispaa ya Tabora, wamerudishwa nyumbani baada ya shule kufungwa kutokana na wazabuni kusitisha huduma ya chakula katika shule zao.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza, alipokuwa akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake mwishoni mwa wiki iliyopita, juu ya hatima ya wazabuni waliositisha kutoa huduma ya chakula katika shule za sekondari za serikali pamoja na vyuo vya walimu.
Sina hakika kama wanafunzi wako nyumbani, sina hakika na hilo kwa kuwa sijapata taarifa ya kiofisi mezani kwangu, alisema Mahiza.
Kwa maelezo ya naibu waziri huyo, hatima ya wazabuni hao itajulikana baada ya hazina kutoa pesa hizo, kwa kuwa ni haki yao kulipwa.
Alikiri kuwa, wazabuni hao wanaidai serikali sh bilioni tisa na kuongeza kuwa ni wajibu wa serikali kulipa pesa hizo.
Hivi karibuni iliripotiwa kuwa, shule za Manispaa ya Tabora zilifungwa kutokana na wazabuni kusitisha huduma ya chakula, kwa kuwa hawajalipwa madeni yao na serikali kwa muda mrefu.
Baadhi ya wanafunzi walilalamikia kitendo hicho kwa kusema kuwa, kitawaathiri katika mitihani yao waliyokuwa wanatarajia kuifanya siku za karibuni.
Shule hizo ni Kazima, Milambo, Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora na Shule ya Sekondari ya Wasichana Tabora.
Hata hivyo, mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bwiru iliyoko Mwanza, Elia Kisuu, aliwaondoa hofu wazazi ambao watoto wao wanasoma katika shule hiyo, kwa kuwaeleza kuwa, shule yake haina tatizo la chakula na wala haijafungwa.
Bwiru ni moja ya shule ambazo wanafunzi waliozungumza na gazeti hili waliitaja kuwa imefungwa.
Wakati mkuu huyo wa Sekondari ya Bwiru, akitoa kauli hiyo, kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Abeid Mwinyimsa, akihojiwa na Idhaa ya Kiwahili ya BBC, alikiri kuwa hali ni mbaya kwa shule hizo za Mkoa wa Tabora, kwani wazabuni wamesitisha huduma katika shule hizo na kusababisha shule hizo kufungwa.
Taarifa kama hii ukisoma unaelewa kabisa kwamba baadhi ya Mawaziri hawapo "duniani" hivi hata vyombo vya habari tu hawasomi, kama waziri mwenye mamlaka kwanini asichukue simu akapiga kuwasiliana na shule husika ili kuchukua hatua "eti anasubiri taarifa zije ofisini" Hiyo ndiyo ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya? Najihisi bado tupo enzi ya "Mfagio wa Chuma"