Serikali boresheni vituo vya afya kutokana na yanayoendelea kwenye hospitali binafsi na wateja wa NHIF

Chagga King

JF-Expert Member
Jul 6, 2011
1,826
1,045
Kutokana na umuhimu wa Afya bora katika mustakabali wa maendeleo ya taifa lolote duniani, serikali inahitaji kuhakikisha inaboresha huduma katika hospitali zake.

Hii ifanyike ili kuweka ushindani na sekta za afya binafsi ambazo serikali imekuwa ikizilipa pesa nyingi kwa huduma wanazotoa (mara nyingi) zikikosa uhalisia, na hivyo kupoteza pesa nyingi.

Ikiwa hiyo haitosha, sekta binafsi ni kama zinaihujumu serikali, kwa kusitisha huduma za afya kwa waTanzania wengi wenye mahitaji.

Kumekuwa na wimbi kubwa ktk sekta mbalimbali i.e. biashara (sukari,mafuta) usafirishaji na sasa Afya, kuwa watoa huduma pamoja na kuwa wanapata faida, lakini wamekuwa wakiiwekea migomo baridi serikali ili kuishinikiza serikali iwape uhuru wa kuwanyonya wananchi masikini. mambo ni mengi sana.

Ushauri wangu kwa serikali, isikubali kushinikizwa, kwakuwa ndiyo yenye mamlaka, inayotunga sheria so haiwezi kubanwa na wachache, watoa huduma waliogoma, serikali iwadhibiti, na isiruhusu tabia kama hizi kuendelea, walichofanya hao watoa huduma ni uhalifu wa hali ya juu.

Hongereni kwa kujenga vituo vingi vya afya, sasa boresheni, tutaenda huko, na Mungu atatulinda. Amina.
 
NHIF ina wahuni wengi wanaoshirikiana na baadhi ya hospitali binafsi kuhujumu mfuko.
Ili kufidia hujuma hiyo,wahuni hao hao wanazikata pesa nyingi sana hospitali za umma na baadhi za binafsi hasa zinazomikikiwa,na dini( FBOs) katika kufidia pesa iliyolipwa kwa dili kwa wadau wao wa siri.

Kitendo cha NHIF kusema inakula hasara,ni uongo mkubwa na inabidi uchunguzi ufanyike ili kubaini ukweli wa jambo hili.

Upo ukweli mkubwa wa baadhi ya taasisi binafsi kuhujumu mapato ya mfuko lakini hili haliwezekani pasipo na msaada wa watu wa ndani ya mfuko kusaidia.

Binafsi niliwahi kuwauzia vipimo vya sukari ili wakatoe msaada mahali fulani lakini walitaka tuwaandikie kuwa tumewauzia zaidi ya walivyohitaji ili mhasibu abaki na pesa.Sikukubaliana nao hivyo wakaenda kununua sehemu nyingine.

Wanaohujumu ni hao hao watumishi wa Bima
 
Kwani serikali inanyonywa na wangapi na wanajua wananyonywa wako kimyaaaa wanasikilizia unyonywaji?

Hii vita ya kipumbavu wanaoumia ni wananchi.

wewe ulie nyumbani safiiii unaona fresh tu lakini piga hesabu waliohospital muda huu private wenye magonjwa makubwa wanaohitaji huduma na uangalizi wa katibu wa kitabibu ambazo serikali imeshindwa kufanya kwa ufanisi kupitia vituo vyao Halafu kesho anapigwe stop.
 
Back
Top Bottom