Serikali 3 na gharama zake
Baada ya kuvunjika kwa bunge la katiba juu ya swala la muundo wa serikali, nachukua nafasi hii kutoa majibu ambayo kwa sababu zisizojulikana imeshindikana kabisa kuelezewa tofauti ya gharama baina ya serikali 2 na 3, gharama zipi zitaongozeka kulingana na mapendekezo ya rasimu ya tume ya Warioba.
Na sii lengo langu kujaribu kuukana ukweli kwamba Tanzania ya leo inahitaji serikali 3 isipokuwa kuwataarifu wananchi waelewa jinsi gani muundo wa aina hii una mamlaka gani na unafanyaje kazi zake ktk utekelezaji wa majukumu wanayokabidhiwa kikatiba. Hii inatokana na mimi kuwasoma watu wengi kutofahamu Mamlaka ya tawala wa muundo huu ili serikali hizo ziweze kuwawakilisha wananchi wake haraka na kwa ufasaha zaidi. Hivyo lengo la kuzitaka serikali 3 linaonyesha wazi ni kutaka kutengenisha mambo ya Muungano na yasiyokuwa ya Muungano kutokana na ukweli kwamba hadi sasa Mambo yote ya Muungano ni mambo ya bara sio ya Muungano badala ya kuziunda serikali ili ziwe karibu zaidi na wananchi wake ktk utekelezaji wa mahitaji yao.
Mara zote nimesikia wananchi wakidai kuwepo kwa seikali 2 hakuna tofauti ya gharama na serikali 3 na wakitumia sababu za mapngufu ya utawala uliopo ambao miaka yote baada ya 1984 tulipounda vyama vingi, kumekuwa na mkanganyika wa utawala ambao umewavuruga wananchi wasijue mamlaka ya vyombo vyao yana ukomo gani. Pia imewavuruga viongozi ambao kwa dhana zao wamekuwa wakiongeza mikoa, wilaya na majimbo wakifikiria ndio njia rahisi ya kuwafikia wananchi wakati mamlaka bado yapo chini ya rais wa serikali kuu. Hivyo mitazamo yote hii imelenga zaidi hifadhi ya Utawala (kisiasa) kuliko sababu za ujenzi wa nyenzo za kuijenga nchi na wananchi wake ambao pia kw abahati mbaya wamevutwa katika zizi la Uchama na kupoteza Utaifa wao.
Ngoja niseme ukweli, Ukweli ni kwamba tunapoihitaji serikali ya 3 siyo serikali ya Tanganyika kama wanavyodai wanasiasa wengi ama wana taaluma wapambanaji isipokuwa tunaihitaji serikali ya Muungano ambayo haipo. Ukweli ni kwamba jina la Muungano lipo lakini hatuna seriikali ya Muungano kiutekelezaji toka mwaka 1984, niliwahi kulisema hili na sasa limedhihirishwa ktk kongamano la jana. Imeelezwa katika kongamano la Mwl.Nyerere foundation ya kwamba hata hayo mambo tunayosema kuwa ni ya Muungano ni mambo ya serikali ya bara.
Hivyo mawaziri wote walioko ktk ushirika wa Muungano ni mawaziri wa serikali ya Tanganyika sio ya Muungano. Wajumbe hao walifikia hadi kuhoji ni lini wananchi wamewaona viongozi mawaziri wa Muungano wakitembelea Zanzibar katika maswala ya Muungano?. Kwa hiyo tunazo serikali 2 nazo ni serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika - Hatuna serikali ya Muungano!.. Ukweli ndio huo japo unauma.
Kwa hiyo basi ni muhimu tukubali kwamba tuchukulie hii serikali ya Muungano ni serikali ya bara, bunge lake, mahakama zake zote ni za bara, na ndio maana wapo wananchi wanaohoji kuwepo kwa wabunge wa Zanzibar katika bunge la Muungano kujadili mambo yasokuwa ya Muungano, bila kujua kwamba pale hakuna mambo ya Muungano. Hivyo tunachokililia leo hii ni serikali ya Muungano na sio Tanganyika maana ipo.
Sasa swali linakuja - Tukiunda serikali ya 3 ya Muungano haitakuwa na gharama zake? Hizo ghrama zake ni nani atazihudumia? Na Je, bunge la serikali hii litakuwa na wajumbe wangapi, kutoka wapi na majimbo gani? Mishahara na posho zao zitagharamiwa na nani, watumishi wake watakuwa sehemu zote za Jamhuri au makao makuu tu na kadhalika… Hizi gharama za misafara ya rais ktk mialiko ya Kimataifa, mawaziri wake, mamlaka yake katika mipango ya maendeleo na kadhalika ndiyo maswala muhimu ya kujadili kuliko kuendelea kuidai Tanganyika ambayo ipo.
Je, nchi za wenzetu walokuwa na mfumo kama huu mamlaka ya uendeshaji wa shughuli za serikali zake umejengwa vipi na nini nafasi ya serikali kuu ktk ujenzi wa Mataifa hayo. Nini ukomo wa mamlaka ya serikali za nchi kuendea mamlaka ya serikali kuu juu ya jambo hilo hilo. Ikiwa Nchi yetu inahitaji uwekezaji katika Kilimo, serikali kuu itahusika vipi tofauti na hizo za kila nchi.
Nafikiri hii inatosha kwa leo tutaendelea inapobidi baada ya michango yenu.
Baada ya kuvunjika kwa bunge la katiba juu ya swala la muundo wa serikali, nachukua nafasi hii kutoa majibu ambayo kwa sababu zisizojulikana imeshindikana kabisa kuelezewa tofauti ya gharama baina ya serikali 2 na 3, gharama zipi zitaongozeka kulingana na mapendekezo ya rasimu ya tume ya Warioba.
Na sii lengo langu kujaribu kuukana ukweli kwamba Tanzania ya leo inahitaji serikali 3 isipokuwa kuwataarifu wananchi waelewa jinsi gani muundo wa aina hii una mamlaka gani na unafanyaje kazi zake ktk utekelezaji wa majukumu wanayokabidhiwa kikatiba. Hii inatokana na mimi kuwasoma watu wengi kutofahamu Mamlaka ya tawala wa muundo huu ili serikali hizo ziweze kuwawakilisha wananchi wake haraka na kwa ufasaha zaidi. Hivyo lengo la kuzitaka serikali 3 linaonyesha wazi ni kutaka kutengenisha mambo ya Muungano na yasiyokuwa ya Muungano kutokana na ukweli kwamba hadi sasa Mambo yote ya Muungano ni mambo ya bara sio ya Muungano badala ya kuziunda serikali ili ziwe karibu zaidi na wananchi wake ktk utekelezaji wa mahitaji yao.
Mara zote nimesikia wananchi wakidai kuwepo kwa seikali 2 hakuna tofauti ya gharama na serikali 3 na wakitumia sababu za mapngufu ya utawala uliopo ambao miaka yote baada ya 1984 tulipounda vyama vingi, kumekuwa na mkanganyika wa utawala ambao umewavuruga wananchi wasijue mamlaka ya vyombo vyao yana ukomo gani. Pia imewavuruga viongozi ambao kwa dhana zao wamekuwa wakiongeza mikoa, wilaya na majimbo wakifikiria ndio njia rahisi ya kuwafikia wananchi wakati mamlaka bado yapo chini ya rais wa serikali kuu. Hivyo mitazamo yote hii imelenga zaidi hifadhi ya Utawala (kisiasa) kuliko sababu za ujenzi wa nyenzo za kuijenga nchi na wananchi wake ambao pia kw abahati mbaya wamevutwa katika zizi la Uchama na kupoteza Utaifa wao.
Ngoja niseme ukweli, Ukweli ni kwamba tunapoihitaji serikali ya 3 siyo serikali ya Tanganyika kama wanavyodai wanasiasa wengi ama wana taaluma wapambanaji isipokuwa tunaihitaji serikali ya Muungano ambayo haipo. Ukweli ni kwamba jina la Muungano lipo lakini hatuna seriikali ya Muungano kiutekelezaji toka mwaka 1984, niliwahi kulisema hili na sasa limedhihirishwa ktk kongamano la jana. Imeelezwa katika kongamano la Mwl.Nyerere foundation ya kwamba hata hayo mambo tunayosema kuwa ni ya Muungano ni mambo ya serikali ya bara.
Hivyo mawaziri wote walioko ktk ushirika wa Muungano ni mawaziri wa serikali ya Tanganyika sio ya Muungano. Wajumbe hao walifikia hadi kuhoji ni lini wananchi wamewaona viongozi mawaziri wa Muungano wakitembelea Zanzibar katika maswala ya Muungano?. Kwa hiyo tunazo serikali 2 nazo ni serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika - Hatuna serikali ya Muungano!.. Ukweli ndio huo japo unauma.
Kwa hiyo basi ni muhimu tukubali kwamba tuchukulie hii serikali ya Muungano ni serikali ya bara, bunge lake, mahakama zake zote ni za bara, na ndio maana wapo wananchi wanaohoji kuwepo kwa wabunge wa Zanzibar katika bunge la Muungano kujadili mambo yasokuwa ya Muungano, bila kujua kwamba pale hakuna mambo ya Muungano. Hivyo tunachokililia leo hii ni serikali ya Muungano na sio Tanganyika maana ipo.
Sasa swali linakuja - Tukiunda serikali ya 3 ya Muungano haitakuwa na gharama zake? Hizo ghrama zake ni nani atazihudumia? Na Je, bunge la serikali hii litakuwa na wajumbe wangapi, kutoka wapi na majimbo gani? Mishahara na posho zao zitagharamiwa na nani, watumishi wake watakuwa sehemu zote za Jamhuri au makao makuu tu na kadhalika… Hizi gharama za misafara ya rais ktk mialiko ya Kimataifa, mawaziri wake, mamlaka yake katika mipango ya maendeleo na kadhalika ndiyo maswala muhimu ya kujadili kuliko kuendelea kuidai Tanganyika ambayo ipo.
Je, nchi za wenzetu walokuwa na mfumo kama huu mamlaka ya uendeshaji wa shughuli za serikali zake umejengwa vipi na nini nafasi ya serikali kuu ktk ujenzi wa Mataifa hayo. Nini ukomo wa mamlaka ya serikali za nchi kuendea mamlaka ya serikali kuu juu ya jambo hilo hilo. Ikiwa Nchi yetu inahitaji uwekezaji katika Kilimo, serikali kuu itahusika vipi tofauti na hizo za kila nchi.
Nafikiri hii inatosha kwa leo tutaendelea inapobidi baada ya michango yenu.