Serial killer in Dar!

Hivi matukio haya mawili yanahusisha muuaji mmoja? Kama ni hivyo motive yake hasa ni nini?
 

Amani ya Tanzania ilishakwisha. Sasa hata ule utulivu nao unatoweka.
 
duh,sasa hv adabu itakuwepo kati ya watu wa pikipiki na wenye magari kwa kuhofia kupigwa risasi,by the way sio jambo jema ila ubabe ulikuwa umezidi barabarani. ma-serial killer wengi ni watu walioumizwa kwa hiyo wanaamua kufanya revenge, inabidi tuwe waangalifu sana huko barabarani.
 
Habari uliyoiandika ina walakini ndani yake, haswa kwenye simulizi la namna matukio yalivyotukia.
Pamoja na hayo bado haya matukio yamenihuzunisha na kuendelea kuamini kuwa Jeshi la Polisi bado wanahitaji kujiimarisha zaidi.


LABDA HEBU TAZAMA HAPA ZAIDI...
Moja kati ya matukio makubwa ya kukumbukwa wiki hii siku ya jumatano march 20 2013 likiwa ni tukio la dereva wa gari dogo aina ya Corolla kupigwa risasi kwenye foleni Kinondoni na mtu aliekua kwenye pikipiki.

millardayo.com na Amplifaya ya Clouds Fm zilipata nafasi ya kuongea kwenye Exclusive interview na mtu pekee ambae alikua kwenye gari na marehemu kabla ya kupigwa risasi na kufariki papohapo wakitokea gereji.

Haya ni mambo 7 makuu aliyoyasema.

1. Kwenye eneo la Mkwajuni Kinondoni kulikua na lori aina ya fuso limesimama barabarani alafu wakati huo kulikua na mwarabu mmoja anaendesha pikipiki aliekua amewatangulia hawa jamaa, walikua kwenye upande wa kushoto wa barabara na mwarabu alikua upande wa kulia ambapo muda mfupi baadae mwarabu alijigonga kwenye ubavu wa fuso akarushwa upande wa kushoto alipokuepo Marehemu ambae aliweza kumkwepa na kuipeleka gari nje ya barabara kulikosababisha tairi kupasua.

2. Baada ya hapo walimfata mwarabu na kwenda kuongea nae, kwanza akawashukuru kwa kumkwepa kisha wakaanza kuongea nae kuhusu malipo, yani wa gari dogo walitaka walipwe tairi lao lililopasuka lakini ghafla bila kutarajia mwarabu alitoa nyaya za umeme zinazotoa shoti na akaanza kuwapiga shoti mwilini kwa makusudi hawa watu wawili waliokuwepo kwenye gari dogo.

3. Huyu shuhuda anasema huyu mwarabu anaitwa ‘Abuu’ na hilo jina lilifahamika baada ya watu kadhaa kujitokeza kwenye eneo la ajali na kumsisitiza asifanye fujo wala kuwapiga wenye gari manake wameokoa maisha yake kwa kumkwepa.

4. Baada ya ubishi huku dereva akiuliza sababu zipi zilizofanya apigwe shoti yeye na mwenzake, mwarabu huyu alichukua bastola yake iliyokua chini na kumfyetulia risasi dereva na kufariki palepale kwenye tukio na mwarabu kukimbia na pikipiki yake.

5. Marehemu hafahamiani na mwarabu huyu hata kidogo ambapo pia shuhuda anasema mazungumzo ya mwisho ya marehemu ni kuhusu mpango wa kuoa July au August mwaka huu.

6. Mtuhumiwa huyu ambae inadaiwa alikua amenyoa panki alionekana na chupa kubwa ya kinywaji maarufu chenye kilevi ambacho kinatengenezwa nje ya Tanzania ambacho husifika na wengi kwa ukali wake wa kulewesha muda mfupi tu baada ya kunywa.

7. Marehemu aliezikwa march 21 2013 saa kumi jioni kwenye makaburi ya kinondoni alikua ameajiriwa kama msaidizi nyumbani ambapo miongoni mwa majukumu yake ni kutumwa sehemu mbalimbali kufanya shughuli za mwajiri wake.

8. Polisi wameahidi kuzungumza leo.
 
Ilikua mbaya kama hivi eenh!





 
Hivi matukio haya mawili yanahusisha muuaji mmoja? Kama ni hivyo motive yake hasa ni nini?

Wauaji ni tofauti lakini namna ya utekelezaji wa kusudio la mauaji ni moja.
 
Lile la kinondoni mkwajuni si walisema aliye husika ni singa singa?
 
Mbaya zaidi wanakua wamevaa lile li helmet na mikoti yani hata akifanya tukio kumtambua ni ishu.
Hii style ilitumika sana na majasusi wa mossad kipindi wanawaua wale wanasayansi wa nyuklia wa iran.pikipiki inatumika kwa advantage ya easy gateaway hata kama kuna trafficjam na lile li helmet kuficha sura ya muuaji,
 
Madreva na abairia kwa ujumla ni kuwa makini wakati wanaendesha magari au kusafiri. Vioo vifungwe.
 
Mbaya sana, sijui jeuri alipata wapi

Labda kwa sangoma. Maana kuna maajabu ajabu kibao yamedhihirika wazi na mchana kweupe, ambayo hapo awali yalionekana kwenye TV. Tuendelee kuvumiliana.
 
Tanzania kupoteza uhai ni rahisi sana!!!
 
Madreva na abairia kwa ujumla ni kuwa makini wakati wanaendesha magari au kusafiri. Vioo vifungwe.

Kwa ni vitu vya ncha kali haviwezi kupenya katika vioo? au vioo hivyo vinakua vile visivyopitisha risasi!
 
Lisa Rina, halafu sio Dar tu. kwa kumbu kumbu zangu kulingana na habari na matukio yaliyopita. Kule Zanzibar, yule padri Mushi kama sikosei aliuawa na mtu ama watu waliokuwa na pikipiki. Kisha baada ya muda tena kuna Padri jijini Mwanza akawa anafuatiliwa na mtu aliyekuwa na pikipiki kila sehemu aliyokwenda, ilikuwa bahati yake akaponea chupuchupu. sasa tena huko dar huyu jamaa wa pikipiki kaonekana, Lazima atakuwa anatekeleza mkakati maalumu.
 
Last edited by a moderator:
CCM inatuharibia nchi kwa tamaa zao ya madaraka.

wengine muwe mnanyamaza tu sio lazima kuchangia.huna tofauti na wale wanaoisingizia cdm na mauaji kama ktk maigizo ya lwakatare.watu wanakufa nyie mnaleta mambo ya kipuuzi
 
Madreva na abairia kwa ujumla ni kuwa makini wakati wanaendesha magari au kusafiri. Vioo vifungwe.

labda iwe sio dar.hapo vioo mnafungua kwenye hizo dalax2 but still mnanusishiana vikwapa na mijasho kibao itakuwaje mkifunga vioo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…