Sera ya ujamaa wa ACT - Wazalendo ndio inapelekea watu kujiunga na ACT - Wazalendo

Ubepari una practice uJamaa kwa kiwango kikubwa sana kwani asiye Nacho anahudumiwa na aliye nacho . Unajua tabia Ya binadamu akitoka Kwenye njaa iliyopitiliza akipewa chakula huwa ana tabia Ya kula kupitia uwezo wake hii ni tabia tuliyo nayo waafrika wengi . Wanaopata nafasi Mara nyingi back ground zao ni ufukara tuu sasa ile nafasi walionayo wanatamani wanyakue kila kilicho ndani Ya upeo wa macho yao. Sisi sasa tumekuwa mabepari kuliko mabepari orijino

Ninaona point yako lakini tukubali pia kuwa matatizo yanayojitokeza si ya mfumo wa uchumi bali mapungufu kama efficiency, cost-effectiveness, financial discipline, strategic management and control, planning na social responsibility. Bila kushughulika na hayo tutabaki hapa hapa tulipo!!!

Ningependa ACT atilie mkazo katika niliyotaja hapo juu badala ya mfumo wa kijamaa. Hivi kweli anataka kusema Azimio la Arusha kufilisi mali za watu ilikuwa ni jambo sahihi?? Wachukue shule binafsi ili kutoa elimu kwa umma bure halafu ziwashinde kuendesha?? Kwani hatuwezi kutoa huduma kwa jamii bila kufanya wealth redistribution?? Kwanini watu wote walazimike kuwa na utajiri unaowiana wakati watu wenyewe wana hulka, tabia na uwezo tofauti??
 
Con chama chenye dhamira ya kweli ya kuikomboa Tz yetu!!cha msingi ni kila mtanzania ajue n vp atajikwamua aweke tonge mdomoni!!N mtazamo wangu tuu!!
 
Zitto kaenda kutibiwa India, ndo uzalendo

Au ndo usanii usanii tuu.. Achani utapeli watz wanaona.
 
Haki Ya Mtu Kamwe Haipotei, Hamuwezi Mkavamia Mchana Kweupe Mkapola Chama Cha Limbu, Mkammilisha Aya, Tolah.
 
Ninaona point yako lakini tukubali pia kuwa matatizo yanayojitokeza si ya mfumo wa uchumi bali mapungufu kama efficiency, cost-effectiveness, financial discipline, strategic management and control, planning na social responsibility. Bila kushughulika na hayo tutabaki hapa hapa tulipo!!!

Ningependa ACT atilie mkazo katika niliyotaja hapo juu badala ya mfumo wa kijamaa. Hivi kweli anataka kusema Azimio la Arusha kufilisi mali za watu ilikuwa ni jambo sahihi?? Wachukue shule binafsi ili kutoa elimu kwa umma bure halafu ziwashinde kuendesha?? Kwani hatuwezi kutoa huduma kwa jamii bila kufanya wealth redistribution?? Kwanini watu wote walazimike kuwa na utajiri unaowiana wakati watu wenyewe wana hulka, tabia na uwezo tofauti??
That's true mkuu . Hata mimi huwa nawaza ACT akiibeba ujamaa kama ilivyo hawezi kufanikiwa na atapata upinzani wa Hali ya juu. Nadhani ujamaa anaoumaanisha si wa enzi ziwe kwani mashani hata dunia haiwezi kumkubali . Nadhani ujamaa anaosema ACT ni ule uliobeba elements zile ulizozisema Kwani hata mabepari tu wa sasa watamwanzishia vita. So ACT kwa mtazamo wangu angefanya kazi Ya ziada kuelezea umma modern ujamaa anaosema ni upi tofauti na ule wa kunyang'anyana mali.
 
Magesa Mwita
UNGANA NAMI KATIKA IMANI YA UJAMAA WA
KIDEMOKRASIA YA ACT-WAZALENDO
SEHEMU YA KWANZA: UTANGULIZI
ACT-Wazalendo imejengwa kwenye IMANI, imani
ya Ujamaa wa Kidemokrasia. Imani tu haitoshi,
bali inahitaji kuenezwa na kutekelezwa na watu,
hapa ndipo unapata team ya Uongozi na
Wanachama wa AC
T-Wazalendo na waumini
wengine wa falsafa ya Ujamaa wa Demokrasia
waliokwishajiunga na watakaojiunga baadaye.
Kwa hiyo dhana ya kujiunga ACT-Wazalendo ni
kumfuata mtu ni dhana ya maadui wasiojua
wanapambana na nini, watapoteza muda na
watakuja kushangaa hata kama mtu huyo hayupo,
upinzani dhidi yao utazidi kushamiri. Msingi mkuu
wa ACT-Wazalendo siyo mtu ni IMANI yetu ya
Ujamaa wa Kidemokrasia.
Tangu tupate uhuru tumekuwa tukifuata mfumo
wa Ujamaa, Pamoja na mazuri yake kama vile
kutokuwa na gap kubwa kati ya masikini na
matajiri, fursa sawa katika kupata huduma za
kijamii kama vile Elimu, Afya, n.k, katika miaka
ya 1980 mfumo huu ulianza kufeli. Sababu ziko
nyingi, nyingine ni ufisadi tu! Lakini kubwa ni la
kiimani, ambalo ni matakwa ya kila mwenye
juhudi kutaka anufaike na matunda ya juhudi
zake bila kuwa na mipaka, namaanisha tama ya
utajirisho au ukwasi kwa kiwango atakacholizika
nacho yeye. Imani ya Ujamaa kwa watu
ikapungua na taratibu tukaanza safari ya
kuelekea kwenye Ubepari. Katika mfumo wa sasa
Ubepari Matajiri wameongezeka
, mafukara
wamekuwa wengi kupindukia, huduma za msingi
zimekuwa za matabaka, kama wewe ni mtu wa
chini mtoto wako hawezi kusoma shule nzuri,
then atakuwa na elimu duni na mwisho wa siku
si rahisi kumudu ushindani katika ajira! Huduma
bora za afya ni kwa wenye fedha. Matajiri
wanamiliki maelfu ya hekari za ardhi kwa
matumizi yao leo na kwa vizazi vyao vya kesho.
Mtoto wa masikini siku za usoni hana chake
katika nchi yake kwa kuwa tu wazazi wake ni
masikini.
Upinzani tuliokuwanao kwa kiwango kikubwa
unafuata mrengo wa kati. Ni ngumu mrengo huu
kuaminika kwa kuwa ni ngumu kujua katika
jambo gani utaegemea kwenye uelekeo wa
Ujamaa na ni katika jambo gani utaegemea
uelekeo wa Ubepari! Lakini practice ya Upinzani
tuliokuwanao inaonyesha dhahiri kuwa
unaegemea zaidi mfumo wa kibepari, kwa
mantiki hiyo basi bado hatuna suluhisho la
matatizo ya kimfumo tuliyonayo sasa, matatizo
ya matajiri kumiliki ardhi yote
. Matatizo ya elimu
bora kwa wachache wenye fedha na hivyo ajira
kubaki za kwao tu. Matatizo ya mwenye fedha
ndiye mwenye haki ya kupata huduma bora za
afya. Matatizo ya mafukara wengi mno
kuongezeka huku wachache wakitumia fursa za
rasilimali zetu sote kujitwalia ukwasi uliopindukia,
n.k. Hapa ndipo IMANI ya Ujamaa wa
Kidemokrasia inapoweza kutusaidia katika
kutatua matatizo haya:
1. ACT-Wazalendo katika Ujamaa wa
Kidemokrasia tunaamini kuwa kila mtu anayohaki
ya kujitajirisha. Lakini ni jukumu la Serikali
kutumia rasilimali zilizopo kuwainua watu wa
tabaka la chini ili kupunguza gap kati ya masikini
na tajiri.
2. ACT-Wazalendo katika Ujamaa wa
Kidemokrasia tunaamini kuwa huduma zote za
msingi serikali ina wajibu wa kuzisimamia na
kutoa fursa sawa kwa raia wote bila kujali tofauti
zao katika vipato au kitu kingine chochote.
Masikini aliye na ugonjwa ana haki ya kupata
matibabu na kuishi sawasawa na tajiri mgonjwa.
Mtoto wa masikini ana haki ya kupata elimu bora
sawasawa na mtoto wa tajiri ili wote waweze
kuwa na fursa za kuchangia katika maendeleo ya
nchi.
3. Utajiri wa nchi au rasilimali nyeti kama madini,
mafuta, gesi, ardhi, n.k lazima zisimamiwe na
serikali kwa manufaa ya wote. Na zaidi zitumike
katika kuwawezesha wanyonge ili wawe na
uwezo wa kushiriki katika uchumi wa nchi
(Uchumi Shirikishi)
Na kadhalika.
Nchi ni lazima iongozwe na uelekeo unaoeleweka
wazi, na katika nchi yetu Ujamaa pamoja na uzuri
wake bado ulikuwa na mapungufu yaliyopelekea
ukashindikana, Ubepari ndio umetufikisha kwenye
matatizo tuliyonayo leo. Ni mtazamo wangu kuwa
IMANI hii ya Ujamaa wa Kidemokrasia ni
suluhisho la matatizo haya ya sasa.

Mi kwa maoni yangu, hoja yenu ni dhaifu kabisa, nimejiuliza swali dogo tu ni kweli matajiri wanamiliki ardhi yote? kwa kosa dogo tu hili najua unaandika usichokijua.Ujamaaaa haupendi utajiri? Mfano akina Alibaba ni wachina, Je si matajiri?Nadhani karudi ukasome vizuri ujamaa wa Mtumishi wa Mungu Mwalimu Nyerere! Alianza na "Utu" nyie mnaanza na umiliki wa mali? Ubepari wenye Utu ndio akina Nyerere waliutaka, baada ya kuona ujamaa unamwelekeo wa kutoswa. Tatizo kubwa la Tanzania sio ujamaa wala ubepari ni Corruption! Rushwa! Rushwa! Kila Mmoja ni msemaji, sheria zipo nzuri, mifumo ya kimaandishi safi sana! Je tunaishi kwa kufuata katiba na sheria? wajapani kwani ni wajamaa? kakamatwe huko endapo umekula rushwa, itakuwaje? Kwa taarifa yako bepari wa kweli halali anachapa kazi na analipa kodi! Kuzidiana kwa kipato sio issue, kwangu ni issue kapate hiyo analipa kodi? uliza kodi kiasi gani inakusanywa? Suala lingiine suala ni Serikali kama mfumo, je upo? umemsikia bwana mkubwa jana anasema hatamaliza yote rais atakayefuata atamaliza akijilinganisha na mzee Nyerere! Hajui Urais ni system, kwamba utawala huenda kwa mujibu wa katiba sheria na kanuni mbalimbali. Yeye anaishi na anaongoza kwa maelekezo kama mkwere. Yeye alipaswa kukamilisha waliyoanzisha maraisi wenzake! Yeye kaja na maagizo na ahadi, fedha inakusanywa inapelekwa kutimiza ahadi zake! Kenya wanacheka kwani Kibaki alisimamia mfumo wa kodi, watu wakaja juu, sasa Kenya wanakimbia mbele sisi tunarudi nyuma.
Kuhusu mtu, ni kweli wala msisingizie watu wanasema ACT wanafuata Mtu, ni ukweli uko wazi. Kama alivyosema ametumwa, kuna wabunge zaidi ya 50, kwani inatofautiana vipi na CCJ, akina mpendazoe walieza kurudisha ujamaa, tumemsikia Sita aliyeanzisha CCJ na Nape, wanasapoti ACT kwamba zina sera inayoeleweka, kimantiki huhitaji kubisha. Mitandao mingi, magazeti mengi yanamwongelea Zitto. Bila zito hakuna ACT, na kwa mantiki nyepesi kapewa cheo. Kwa nini hakuanza kama raia wa kawaida. Tumeona kwa Mrema, alipotoka CCM akaenda NCCR, tulimfuata Mrema. Mrema alipoharibu, mpaka sasa NCCR iliyumba na haina utukufu ule wa Mrema. Kama si kweli, mwambie kesho zito aende TLP, kama itakuwa ACT ile ile. Kwa heri, tuonane mwakani
 
Haki Ya Mtu Kamwe Haipotei, Hamuwezi Mkavamia Mchana Kweupe Mkapola Chama Cha Limbu, Mkammilisha Aya, Tolah.

Kabla hujaendelea kuupotosha umma wa watanzania juu ya Zitto Kabwe na ACT-Wazalendo nakuomba utuondolee utata kwa kujibu haya maswali ili kuweka kumbukumbu sahihi.

1.Walituambia kuwa chama cha wananchi CUF
ni tawi la ccm,wakaenda mbali kwa kuwaita
kuwa ni chama cha Mashoga ghafla wakasahau
matusi yao na wakaanza mashirikiano
Mapya,Je ile tuhuma iliishia wapi?
2.Chadema walituaminisha kuwa Chama cha
NCCR mageuzi kimejaa Usalama wa
Taifa,wakaenda mbali wakamkejeli Mbatia, tena
ndani ya Bunge kuwa,yupo Upinzani huku
akiitumikia ccm,ghafla tu Mbatia ni Mshirika
namba Mbili wa Ukawa bila watanzania
kuelezwa kama zile tuhuma zilikuwa za kweli
au za kutunga kwa nia ya kuwalaghai watu.
3.Chadema kwenye Ilani yake 2010
walituambia kuwa tukiwachagua hawatachukua
posho kama hatua mojawapo ya kuonyesha
kwa vitendo kuchukizwa na matumizi mabaya
ya serikali.Je Kwanini wamekiuka Ilani yao?
4.Chadema Mwaka 2011 walikataa kushirikiana
na vyama vya Upinzani ili kuunda kambi ya
Upinzani yenye sauti na nguvu,wakatuambia
kuwa Vyama vyote ni mawakala wa ccm
isipokuwa Chadema,hivyo kushirikiana nao ni
kurudisha nyuma harakati za ukombozi,ghafla
tu baraza kivuli la mawaziri likavunjwa na wale
vibaraka wa ccm wakaingizwa kwenye kambi
ya upinzani bila sisi wafuasi kuambiwa ni lini
ukibaraka wao umeisha mpaka wakaaminiwa.
5.Tuliambiwa kuwa David Kafulila ni mtu hatari
kwa ustawi wa Upinzani hasa
Chadema,tukaambiwa ni Sisimizi ambae hana
umuhimu wowote ndani ya Chadema ,ghafla tu
Sisimizi kageuka tembo,Mtu hatari kageuka
Shujaa na sasa ananadiwa na viongozi wa
Chadema kuwa ukawa imepata tuzo,Je ni lini
kafulila alianza kuaminiwa ?
6.Tuliambiwa tena kuwa ,Serikali kutumia
mashangingi huku Zahanati hazina dawa ni
kiwango cha juu cha Ubinafsi,Mbowe akalikataa
Shangingi la Kiongozi wa Upinzani....ghafla
nimemuona Bukoba akiwa na Shangingi lenye
maandishi KUB. Je ndio lilelile alilolikataa
hadharani au ni lingine?
7.Mbowe alituahidi kwenda mahakamani,na
kudai kuwa wanasheria wake wanaandaa
mashtaka dhidi ya Zitto Kabwe baada ya Zitto
kumtuhumu kuwa alipokea fedha toka kwa
makada wa ccm na kuwa alicheza dili ns
Kinana kuhusu deni analodaiwa na NSSF.Je
taratibu za ufunguaji kesi ziliishia wapi ?
8. Chadema Mwaka 2011 ilitangazia Umma
kutomtambua Rais Kikwete kwakuwa
alishindwa na Slaa,ghafla wanatangaza kuomba
mashauriano na Rais waliemkataa,wakafika
Ikulu kujadiliana juu ya maswala mbalimbali ya
Kitaifa,wakanywa Juice na kupiga picha,Je ni
lini Chadema ilianza kumtambua Rais na
kwanini sisi wananchi hatukuelezwa kuwa
kuanzia sasa Kikwete ni Rais?
Sina nia ya kuibua Marumbano yasiyotujenga
bali nataka mtu mwenye uelewa mkubwa kuliko
mimi anaondoe Uvulivuli ili nami nijitambue.
Naomba nijibiwe hayo ili nami niwe Kamanda
nitakaeitetea Chadema popote.
Hayo Majawabu yakipatikana,ndio utakuwa
mwisho wa Chama cha ACT-Wazalendo maana
umma utaiamini Chadema na hivyo kuiunga
mkono.
Kama Maswali yakikosa Majibu basi Chadema
itakosa uhalali wa kutuhumu ACT-Wazalendo na
viongozi wake na hivyo wananchi wataendelea
kujiunga na ACT-Wazalendo kwa kuamini kuwa
maneno yoyote yanayotolewa na Chadema ni
Ulaghai.
Karibuni kwa majibu Makamanda ili nasi tupate
chakuwaambia wananchi ili waipuuze ACT-
Wazalendo.
 
Back
Top Bottom