HOJA Sera Mpya ya 'Cashless' itafeli, sababu ni hizi

HOJA Sera Mpya ya 'Cashless' itafeli, sababu ni hizi

Hoja ya Mdau inayopendekeza maboresho au mabadiliko ndani ya jamii, inayotakiwa kuangakiwa kwa mapana na Mamlaka husika
Mtu anauza bidhaa analipia kodi anataka kutuma hiyo pesa kwa ajili ya matumizi analipia tena kodi ananunua umeme ambao upo chini ya Serikali na huduma yao analipia kodi tena..
 
Tuishauri serekali tufanyeje?,
*Makato ya miamala ni makubwa mno! (Unatoa 5000 unakatwa 700-800 hii ni ghali mno its should be 250/-) Ukizingatia hizi function ni automatic au autorun once set-up!/
Ikishashusha gharama ilazimishwe tu,manunuzi yote kariakoo yafanywe kwa mfumo wa card,swap au mobile!...
5000 ikatwe 250/-
10,000 ikatwe 500/-
100,000 ikatwe 1500/-
500,000 ikatwe 2000/-
1,000,000 ikatwe 2500/-
sio kwamba hawajui wanajua...issue ni kwamba wakitoa hizo tozo fuko la serikali litashuka watalambaje asali na wakati hawana mbadala mwingine wa kutunisha fuko...zingatia..na sio kwamba hakuna namna nyingine zakutunisha fuko, ila ndo ni miradi ya makumazani wa nchi hii.
 
SIMU ZOTE AMBAZO ZITAKUWA ZINAPOKEA MALIPO MADUKANI ZIWE REGISTERD!....KWA NANNA YA KIPEKEE NAMBA YA SIMU IWEPO KWENYE LESENI!.....(KU-DIVERT MALIPO KATIKA NAMBA NYINGINE ADHABU IWE KUFILISIWA)
Tusio na simu hatuta nunua kitu?
 
Utapaswa kuwa na card,hata kiswaswadu poa tu,
#Maisha ya ulaya ni kadi tu,zingine za gate pass,basi tunakuwa mfukoni na kadi mpaka 7.
Card ya nida wameshindwa kunipa hadi leo, hayo macard mengine labda tuwape miaka 20 kukamilisha
 
Tatizo kubwa la mambo mengi kukwama Africa, viongozi uwa hawajiandai na kitu chochote wanakurupuka tu. Sasa huo mfumo wa cashless huko ulitakiwa uangaliwe hayo makato yapunguzwe ili kumpa mlipaji unafuu au kuyafuta yote na kubaki na fees kidogo ili kuwaencourage watu wengi wautumie huo mfumo cashless.
Kukurupuka ndio asili yetu waafrika uwaga hatuna research yoyote kabla ya kuleta kitu kipya. Sasa kwa hayo makato anaeumia ni mlipaji. WTF.
Inawezekana ikawa kweli kukurupuka ila sifikiri hivyo.

Tatizo la hao walioko kwenye madaraka wanajiona wao ndio final na wananchi ni watumwa wao hawawajali hata kuwaogopa kabisa.

Mfano fikiria, mbunge (spika wa sasa) anaishauri serikali kuongeza tozo kwy line ya simu ikiwa kama mbinu ya kuongeza mapato ya serikali 😂😂😂

Kujua wao ndio wamiliki wa nchi na wananchi, angalia wanavyolipana mishahara na marupurupu kibao na bado kama haitoshi, hawakatwi kodi na nasikia hata kwy hizi transactions za simu wao hawana makato.
 
Hio sera ya Cashless haiwezi kufeli kwa sababu wakubwa 1st world walishaanza kuitumia kitamboo sana nyie huko 3rd world ni mnapewa maelekezo tu mtafuata mtake msitake hio ndio New world order. Mie huku sijashika dollar kama dollar kwa miezi zaidi ya 6, ni mwendo wa cashless tu kila sehemu.
Kumbe Manzese kwa mfuga mbwa wanatumia dollar siku hizi?
 
Tatizo kubwa la mambo mengi kukwama Africa, viongozi uwa hawajiandai na kitu chochote wanakurupuka tu. Sasa huo mfumo wa cashless huko ulitakiwa uangaliwe hayo makato yapunguzwe ili kumpa mlipaji unafuu au kuyafuta yote na kubaki na fees kidogo ili kuwaencourage watu wengi wautumie huo mfumo cashless.
Kukurupuka ndio asili yetu waafrika uwaga hatuna research yoyote kabla ya kuleta kitu kipya. Sasa kwa hayo makato anaeumia ni mlipaji. WTF.
Well said ,yaani nilipie kitu cha elfu 10 then nikatwe 1,500/= wakati mfukoni nina SHUKA LA MMASAI ,kwanini nisilipe tu cash? Waondoe tozo na tukatwe kidogo maana kwenye hiyo fedha tayari serikali ina kodi yake.
 
SIMU ZOTE AMBAZO ZITAKUWA ZINAPOKEA MALIPO MADUKANI ZIWE REGISTERD!....KWA NANNA YA KIPEKEE NAMBA YA SIMU IWEPO KWENYE LESENI!.....(KU-DIVERT MALIPO KATIKA NAMBA NYINGINE ADHABU IWE KUFILISIWA)
Una fikiria kimaskini, serikali yetu pekee ndio inawaza kudhibiti na ku control kila kitu... ni njia ya kufanya watu wako kua watumwa

Watu wakiwa na mifumo rafiki hauhitaji kua na fikra za kikoloni au kiutumwa namna hii
 
maendeleo huambatana na gharama, tusiogope mabadiliko 🐒
Dunia ya sasa inaangazia kurahisisha, kuounguza gharama, kupunguzq mzigo na automatically the population hufata

Kwetu huku ni kutumikisha, kulazimisha wakati mazingira rafiki hayapo.
Kaa kwa dakika kumi uangalie matangazo ya nchi mbali mbali hata ya kitaasisi za serikali, ni lugha za kurahisisha huduma.

Tanzania yetu ni uthibiti, kupiga fine, kutishia
 
Back
Top Bottom