Hatukosei kabisa Mkuu tunaposema Lissu the Great ni hazina kubwa ya Taifa. Mwenyezi Mungu kasikia sala zetu (Wakristo, Waislamu na wale wa dini nyingine) kuhusu mwenzetu mtetezi wa maslahi ya Taifa na wanyonge nchini tulipomuombea kumuomba amponye pamoja na risasi 38 kuingia mwilini mwake. Mwenyezi Mungu ni mkubwa na leo hii ametupa matumaini makubwa kuhusu afya ya Lissu the Great ukilinganisha na siku ile aliyoshambuliwa ambapo wengi tulikuwa na hofu kubwa kama ataweza kumaliza hata masaa 24 akiwa hai. Tuombe.