Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,797
- 71,216
Niwaambie nini kuhusu Tundu Lissu?
Sina la kusema
Kwa ufupi
Nilifungwa jela miaka 30 na viboko 12! Nikiwa kada wa CCM na mjumbe wa mkutano Mkuu wa CCM. Kwa kusema neno moja tu watu tunaozunguka mgodi tuingie ubia na kampuni ya uwekezaji nikiwa mwenyekiti wa kijiji cha Kewanja,( CCM ) na mstaafu wa Jeshi la Wananchi
Amri ya Benjamin mkapa Rais ikaja kwamba huyo anayefundisha watu ashughulikiwe
Nikafungwa miaka 30! Familia yangu haikuwa na uwezo wa kuja Mahakami ila Tundu Lissu akajitolea akawa Wakili wangu bila kumpa cent hata moja. Akanitetea nikashinda kesi
LISSU KWANGU NI ZAIDI YA MTETEZI
AUGUSTINO NESTORY SASSI
KUTOKA NYAMONGO
Senior council 1984- 2010
Mwkt wa Kijiji. 1982-2001
Nimeona mengi namuomba MUNGU AMTETE LISSU
My take;
Kuna watu wamemwita Lissu msaliti na majina kedekede, lakini ona ushuhuda wa huyu Mzee kada wa ccm ulivyo. Alisaidiwa bila kujali yeye ni CCM lakini kama Mtanzania mnyonge. Lakini Kuna watu wanabomolewa Nyumba zao kwa vile tuu hawakuwapa kura.
Je mzalendo ni nani hapo?
Nadhani ni mpango wa Mungu Ku spare maisha ya Lissu ili 2020 aje awapiganie wananchi wote bila kujali haya mavyama