'Selfie' yaondoka na uhai wa msichana huko Urusi

'Selfie' yaondoka na uhai wa msichana huko Urusi

FikraPevu

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2010
Posts
304
Reaction score
236
Tunaishi katika dunia ambayo watu wengi wanapenda kujipiga picha ‘selfie’na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii. Tabia hiyo ya kujipiga selfie inatajwa kuwa ni mapinduzi makubwa ya tasnia ya upigaji picha duniani. Pamoja na uzuri wake kuna matokeo hasi ambayo yanaweza kujitokeza kwa mtu pale anapotumia vibaya teknolojia hiyo.

Moja ya madhara hayo ni vifo kwa mshtuko wa moyo ambavyo hutokana na watu hao kujipiga picha kwenye maeneo hatarishi na muda usiofaa. Baadhi ya watu waliofariki kwa mshtuko wa moyo wakati wakijipiga picha katika maeneo mbalimbali duniani.

Huko Urusi, msichana mdogo aitwae Xenia Ignatyeya alifariki wakati akiwa juu ya jengo refu nchini humo. Taarifa zinaeleza kuwa hakushika vizuri fimbo aliyokuwa imeshikilia simu ambayo alikuwa anatumia kujipiga picha, alikosa mwelekeo na akaanguka chini kutoka kwenye jengo hilo ambalo lina urefu wa futi 820.

Chakushangaza ni kwamba alifariki kabla hajafika chini kwasababu aligusa nyaya za umeme wakati akishuka chini.

Xenia-Ignatyeva.jpg


Kufahamu vifo vinavyotokana na kujipiga selfie soma hapa => Kujipiga picha za ‘selfie’ kunavyoweza kuhatarisha maisha yako
 
Hili tukio si la kwel..alifikaje hapo,..hakuna jinsia ya kike yenye ujasiri wa kupanda hapo,na alipandishwa na nan kwenye hiyo ncha ya jengo.

Unatuwekea photo shop mkuu?
 
Hili tukio si la kwel..alifikaje hapo,..hakuna jinsia ya kike yenye ujasiri wa kupanda hapo,na alipandishwa na nan kwenye hiyo ncha ya jengo.

Unatuwekea photo shop mkuu?
kuna wanawake jasiri acha kabisa
 
Hili tukio si la kwel..alifikaje hapo,..hakuna jinsia ya kike yenye ujasiri wa kupanda hapo,na alipandishwa na nan kwenye hiyo ncha ya jengo.

Unatuwekea photo shop mkuu?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hili tukio si la kwel..alifikaje hapo,..hakuna jinsia ya kike yenye ujasiri wa kupanda hapo,na alipandishwa na nan kwenye hiyo ncha ya jengo.

Unatuwekea photo shop mkuu?
Alipelekwa na ndege
 
Si wajipige K tu jamani wakiwa chumbani au wanaoga ...

Hizi sura hatuna shida nazo.
Acha wafe tu.
 
Angekuwa mbongo hapo angebinua na "kipumulio" kimtindo ili selfie inoge wakati akiendelea kuanguka.
 
Tunaishi katika dunia ambayo watu wengi wanapenda kujipiga picha ‘selfie’na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii. Tabia hiyo ya kujipiga selfie inatajwa kuwa ni mapinduzi makubwa ya tasnia ya upigaji picha duniani. Pamoja na uzuri wake kuna matokeo hasi ambayo yanaweza kujitokeza kwa mtu pale anapotumia vibaya teknolojia hiyo.

Moja ya madhara hayo ni vifo kwa mshtuko wa moyo ambavyo hutokana na watu hao kujipiga picha kwenye maeneo hatarishi na muda usiofaa. Baadhi ya watu waliofariki kwa mshtuko wa moyo wakati wakijipiga picha katika maeneo mbalimbali duniani.

Huko Urusi, msichana mdogo aitwae Xenia Ignatyeya alifariki wakati akiwa juu ya jengo refu nchini humo. Taarifa zinaeleza kuwa hakushika vizuri fimbo aliyokuwa imeshikilia simu ambayo alikuwa anatumia kujipiga picha, alikosa mwelekeo na akaanguka chini kutoka kwenye jengo hilo ambalo lina urefu wa futi 820.

Chakushangaza ni kwamba alifariki kabla hajafika chini kwasababu aligusa nyaya za umeme wakati akishuka chini.

View attachment 733729

Kufahamu vifo vinavyotokana na kujipiga selfie soma hapa => Kujipiga picha za ‘selfie’ kunavyoweza kuhatarisha maisha yako
Hicho kifimbo nakionaga na boss wangu mkienda visit sehemu basi ni kujipiga tu ila kiukweli hakinivutii hata kidogo!
Naamini zaidi katika camera ya yashica na si vinginevyo
 
Back
Top Bottom