Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,391
- 39,484
Habari Leo
Baadhi ya wabunge wa Mkoa wa Tabora wametishia kutounga mkono bajeti za baadhi ya wizara kutokana na kitendo cha serikali kushindwa kutekeleza ahadi zake hasa katika ujenzi wa barabara ya kutoka Itigi, Tabora kwenda Kigoma.
Wa kwanza aliyesema wazi hataunga mkono bajeti za wizara ya Maendeleo ya Miundombinu, Nishati na Madini na Maji na Umwagiliaji ni Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM). Katika mchango wake, Selelii alisema Serikali katika Bajeti ya 2006/7, iliahidi kutengeneza barabara; lakini safari hii barabara hiyo haimo hata kwenye vitabu vya Bajeti ya Serikali.
Alisema, "safari hii hatoki mtu humu ndani hadi nielezwe kwa nini barabara hii haikutengewa fedha wakati serikali ilituahidi." "Mwaka 2006, Spika uliniomba nikae kimya kwa kuwa wewe ni kaka yangu, lakini safari hii sitakubali kukaa kimya maana nimesoma vitabu vya bajeti na kitabu cha matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu sijaona barabara hizi," alisema Selelii.
Alisema kitendo hicho cha serikali kushindwa kuipangia bajeti barabara hiyo ni dharau kwa wananchi wa mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa. "Humu ndani mawaziri wanatukebehi sisi wabunge mawaziri wanatudharau sisi na wananchi wa mikoa hii," alisema.
Alihoji, "hivi hadi tuseme Kinyamwezi na Kisukuma humu bungeni ndipo tutaeleweka? Spika akamjibu "Hapana hizo siyo lugha rasmi." Akaendelea kusema, "inauma sana Spika maana hata kuitaja tu barabara hiyo sikuona, inaonyesha serikali haina habari nayo."
Selelii alisema barabara hiyo ikiwamo ile ya Ipole kwenda Nzega zilishafanyiwa upembuzi yakinifu tangu miaka ya nyuma; lakini serikali imeshindwa kuanza ujenzi. Mbunge huyo alihoji "Hivi sisi tumeikosea nini Serikali hii?
Akamwangalia Spika na kumweleza, "Spika wakubwa wenzako humu ndani wana uwezo wa kwenda katika majimbo yao kwa barabara, lakini wewe huwezi ni lazima ukitoka hapa urudi Dar es Salaam ndipo upande ndege kwenda jimboni kwako. Kwa nini sisi tuwe watu wa kudanganywa tu?
Alisema barabara hizo ni muhimu kwa utalii wa mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa pamoja na shughuli nyingine za uzalishaji mali, hivyo aliomba mwongozo wa Spika kuona Ofisi ya Waziri Mkuu itafanya nini ili hiyo barabara iingizwe kwenye hotuba yake na Spika akamjibu asubiri kwanza majibu ya Serikali.
Akizungumzia usafiri wa treni, Mbunge huyo alisema tangu reli ya kati ilipokodishwa kwa wageni, abiria wa mikoa ya Magharibi wanapangwa kama kuni kutokana na shida ya usafiri iliyopo. Alisema watu wa mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa ni Watanzania wanahitaji usafiri wa uhakika ili kukuza shughuli zao za uchumi.
Hoja hiyo ya Selelii iliungwa mkono pia na Mbunge wa Viti Maalumu, Aziza Sleyum Ally (CCM), ambaye alitaka Waziri Mkuu ampe sababu tano za serikali kutoipangia fedha barabara ya Itigi kwenda Tabora hadi Kigoma.
"Hizi sababu tano mimi na wananchi wetu zitatupa fursa ya kufahamu sababu ya serikali kuisahau barabara hii," alisema Aziza ambaye pia aligusia suala la usafiri wa reli ya kati na kuhoji iweje baada ya kupewa Wahindi tatizo la usafiri wa treni limekuwa kubwa tofauti na hapo awali.
Alisema wasafiri wa treni wanapewa tiketi ambayo haina namba ya kiti hivyo anayewahi ndiye anayekaa. "Yaani hawa wanatufanya kama hapa ni India, hapa sisi ni Watanzania hatukuzoea shida za namna hii." Naye Mbunge wa Singida Kusini, Mohamed Missanga (CCM), alihoji sababu ya serikali kutotunga sera itakayotoa fursa ya miundombinu ya barabara kutengenezwa kwa ubia na sekta binafsi.
Alisema licha ya suala hilo kuafikiwa na serikali, lakini utekelezaji wake unachukua muda mrefu. Missanga alisema licha ya serikali kuwa na kaulimbiu ya kasi mpya, lakini kwa upande wa maamuzi hiyo kasi mpya haionekani kwani kuna mambo mengi likiwamo suala la ujenzi wa daraja la Kigamboni kushindwa kutekelezwa licha ya nia ya ujenzi kuwapo.
Wabunge leo wataendelea kuchangia katika hotuba ya Waziri Mkuu juu ya matumizi ya ofisi yake pamoja na Wizara ya Tamisemi. Kesho serikali itatoa majibu ya hoja zote. Wabunge 105 wameomba kuchangia kwa mdomo, lakini yawezekana ni nusu yao tu watapata fursa hiyo.
Baadhi ya wabunge wa Mkoa wa Tabora wametishia kutounga mkono bajeti za baadhi ya wizara kutokana na kitendo cha serikali kushindwa kutekeleza ahadi zake hasa katika ujenzi wa barabara ya kutoka Itigi, Tabora kwenda Kigoma.
Wa kwanza aliyesema wazi hataunga mkono bajeti za wizara ya Maendeleo ya Miundombinu, Nishati na Madini na Maji na Umwagiliaji ni Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM). Katika mchango wake, Selelii alisema Serikali katika Bajeti ya 2006/7, iliahidi kutengeneza barabara; lakini safari hii barabara hiyo haimo hata kwenye vitabu vya Bajeti ya Serikali.
Alisema, "safari hii hatoki mtu humu ndani hadi nielezwe kwa nini barabara hii haikutengewa fedha wakati serikali ilituahidi." "Mwaka 2006, Spika uliniomba nikae kimya kwa kuwa wewe ni kaka yangu, lakini safari hii sitakubali kukaa kimya maana nimesoma vitabu vya bajeti na kitabu cha matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu sijaona barabara hizi," alisema Selelii.
Alisema kitendo hicho cha serikali kushindwa kuipangia bajeti barabara hiyo ni dharau kwa wananchi wa mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa. "Humu ndani mawaziri wanatukebehi sisi wabunge mawaziri wanatudharau sisi na wananchi wa mikoa hii," alisema.
Alihoji, "hivi hadi tuseme Kinyamwezi na Kisukuma humu bungeni ndipo tutaeleweka? Spika akamjibu "Hapana hizo siyo lugha rasmi." Akaendelea kusema, "inauma sana Spika maana hata kuitaja tu barabara hiyo sikuona, inaonyesha serikali haina habari nayo."
Selelii alisema barabara hiyo ikiwamo ile ya Ipole kwenda Nzega zilishafanyiwa upembuzi yakinifu tangu miaka ya nyuma; lakini serikali imeshindwa kuanza ujenzi. Mbunge huyo alihoji "Hivi sisi tumeikosea nini Serikali hii?
Akamwangalia Spika na kumweleza, "Spika wakubwa wenzako humu ndani wana uwezo wa kwenda katika majimbo yao kwa barabara, lakini wewe huwezi ni lazima ukitoka hapa urudi Dar es Salaam ndipo upande ndege kwenda jimboni kwako. Kwa nini sisi tuwe watu wa kudanganywa tu?
Alisema barabara hizo ni muhimu kwa utalii wa mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa pamoja na shughuli nyingine za uzalishaji mali, hivyo aliomba mwongozo wa Spika kuona Ofisi ya Waziri Mkuu itafanya nini ili hiyo barabara iingizwe kwenye hotuba yake na Spika akamjibu asubiri kwanza majibu ya Serikali.
Akizungumzia usafiri wa treni, Mbunge huyo alisema tangu reli ya kati ilipokodishwa kwa wageni, abiria wa mikoa ya Magharibi wanapangwa kama kuni kutokana na shida ya usafiri iliyopo. Alisema watu wa mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa ni Watanzania wanahitaji usafiri wa uhakika ili kukuza shughuli zao za uchumi.
Hoja hiyo ya Selelii iliungwa mkono pia na Mbunge wa Viti Maalumu, Aziza Sleyum Ally (CCM), ambaye alitaka Waziri Mkuu ampe sababu tano za serikali kutoipangia fedha barabara ya Itigi kwenda Tabora hadi Kigoma.
"Hizi sababu tano mimi na wananchi wetu zitatupa fursa ya kufahamu sababu ya serikali kuisahau barabara hii," alisema Aziza ambaye pia aligusia suala la usafiri wa reli ya kati na kuhoji iweje baada ya kupewa Wahindi tatizo la usafiri wa treni limekuwa kubwa tofauti na hapo awali.
Alisema wasafiri wa treni wanapewa tiketi ambayo haina namba ya kiti hivyo anayewahi ndiye anayekaa. "Yaani hawa wanatufanya kama hapa ni India, hapa sisi ni Watanzania hatukuzoea shida za namna hii." Naye Mbunge wa Singida Kusini, Mohamed Missanga (CCM), alihoji sababu ya serikali kutotunga sera itakayotoa fursa ya miundombinu ya barabara kutengenezwa kwa ubia na sekta binafsi.
Alisema licha ya suala hilo kuafikiwa na serikali, lakini utekelezaji wake unachukua muda mrefu. Missanga alisema licha ya serikali kuwa na kaulimbiu ya kasi mpya, lakini kwa upande wa maamuzi hiyo kasi mpya haionekani kwani kuna mambo mengi likiwamo suala la ujenzi wa daraja la Kigamboni kushindwa kutekelezwa licha ya nia ya ujenzi kuwapo.
Wabunge leo wataendelea kuchangia katika hotuba ya Waziri Mkuu juu ya matumizi ya ofisi yake pamoja na Wizara ya Tamisemi. Kesho serikali itatoa majibu ya hoja zote. Wabunge 105 wameomba kuchangia kwa mdomo, lakini yawezekana ni nusu yao tu watapata fursa hiyo.