SEKRETARIETI YA TFF IMEKOSEA KUMUADHIBU HAJI MANARA
Mbali na mambo mengine katika sakata hilo, bado pia kuna mengine ambayo ni pamoja na haya yafuatayo:
(1) Katika Kanuni zote za adhabu za TFF, hakuna hata moja ya kumtoza mtu shilingi milioni 20;
(2) Katika mashtaka yale, mlalamikaji alipaswa awe Wallace Karia mwenyewe na siyo Sekretarieti ya TFF ambayo ndiyo inailipa posho zote Kamati ya Maadili, hivyo lazima itekeleze maelekezo inayoielekeza kama mwajiri.
Hapa kwa tafsiri nyingine, mlalamikaji hakuwa Karia ila Sekretarieti ya TFF ambayo haijasema inahusikaje na ugomvi wa Manara na Karia wala kuwa ina maslahi gani na malumbano hayo, hasa pale ambapo yule anayedaiwa kudhalilishwa hakulalamika.
Mwisho katika hili, kwa vile Kamati ya Maadili inalipwa posho zote za shughuli zake na Sekretarieti ya TFF zikiwemo za kusikiliza mashtaka, hapa maana yake ni kwamba yenyewe ndiyo iliyokuwa mlalamikaji, shahidi wa upande wa mashtaka na hakimu aliyetoa hukumu hiyo;
(3) Karia aliyepaswa awe ndiye shahidi mkuu wa upande wa mashtaka, kisha wengine wote wabaki kuwa mashuhuda, lakini hakuitwa wala kufika ili kutoa ushahidi wake;
(4) Kamati ya Maadili ya TFF haijasema chanzo cha Manara kufanya hivyo wala haijataja mashahidi waliofika mbele yake ili kutoa ushahidi wao dhidi ya Manara.
Hii ni kwa sababu, inawezekana Manara alikuwa anajihami au kujibu mapigo baada ya kuchkozwa, kutukanwa au kudhalilishwa kwanza na Karia; na
(5) Kwa mujibu wa Sheria za TFF, anayefikishwa katika Kamati ya Maadili kwa masuala ya soka ni kiongozi wa kuchaguliwa wa Klabu, Chama cha Soka cha ngazi yoyote, chombo cha Shirikisho la Soka au mwenye nafasi ya kuteuliwa iliyopo kwenye muundo wa Shirikisho la Kandanda Duniani au FIFA.
Nafasi ya "Mhamasishaji" kama aliyonayo Manara haipo katika muundo wa FIFA, hivyo anaweza tu kuwa ni shabiki wa Yanga ambaye hawezi kushtakiwa katika Kamati ya Maadili ya TFF ila mahakamani kama alimdhalilisha Karia.
Alipaswa ashtakiwe Kituo cha Polisi na Karia mwenyewe, kisha apelekwe mahakamani kama mtu binafsi na mlalamikaji akawe shahidi wa Jamhuri kama mtu binafsi na siyo kama Rais wa TFF.
Katika kutekeleza mfumo na muundo wa FIFA, Yanga yenyewe ina Afisa Habari wake, Hassan Bumbuli. Huyo ndiye anaweza kushtakiwa katika Kamati ya Maadili ya TFF.
Kutokana na hali hiyo na hata vinginevyo, swali linalozuka hapa ni je, tangu lini Manara ni kiongozi wa kuchaguliwa au afisa wa kuteuliwa wa Yanga kwa kuzingatia muundo wa FIFA?
Ni cha kujifunza hapa na kukishika kila mshabiki na kukipigia kelele siku zote hadi Manara atakapoachiwa huru ni wajibu ni kwa nini mashabiki au shabiki anaporusha chupa ya maji uwanjani inaazibiwa klabu na si mhusika why Manara ahukumiwe kama yeye wakati anaipigania timu.
Mbali na mambo mengine katika sakata hilo, bado pia kuna mengine ambayo ni pamoja na haya yafuatayo:
(1) Katika Kanuni zote za adhabu za TFF, hakuna hata moja ya kumtoza mtu shilingi milioni 20;
(2) Katika mashtaka yale, mlalamikaji alipaswa awe Wallace Karia mwenyewe na siyo Sekretarieti ya TFF ambayo ndiyo inailipa posho zote Kamati ya Maadili, hivyo lazima itekeleze maelekezo inayoielekeza kama mwajiri.
Hapa kwa tafsiri nyingine, mlalamikaji hakuwa Karia ila Sekretarieti ya TFF ambayo haijasema inahusikaje na ugomvi wa Manara na Karia wala kuwa ina maslahi gani na malumbano hayo, hasa pale ambapo yule anayedaiwa kudhalilishwa hakulalamika.
Mwisho katika hili, kwa vile Kamati ya Maadili inalipwa posho zote za shughuli zake na Sekretarieti ya TFF zikiwemo za kusikiliza mashtaka, hapa maana yake ni kwamba yenyewe ndiyo iliyokuwa mlalamikaji, shahidi wa upande wa mashtaka na hakimu aliyetoa hukumu hiyo;
(3) Karia aliyepaswa awe ndiye shahidi mkuu wa upande wa mashtaka, kisha wengine wote wabaki kuwa mashuhuda, lakini hakuitwa wala kufika ili kutoa ushahidi wake;
(4) Kamati ya Maadili ya TFF haijasema chanzo cha Manara kufanya hivyo wala haijataja mashahidi waliofika mbele yake ili kutoa ushahidi wao dhidi ya Manara.
Hii ni kwa sababu, inawezekana Manara alikuwa anajihami au kujibu mapigo baada ya kuchkozwa, kutukanwa au kudhalilishwa kwanza na Karia; na
(5) Kwa mujibu wa Sheria za TFF, anayefikishwa katika Kamati ya Maadili kwa masuala ya soka ni kiongozi wa kuchaguliwa wa Klabu, Chama cha Soka cha ngazi yoyote, chombo cha Shirikisho la Soka au mwenye nafasi ya kuteuliwa iliyopo kwenye muundo wa Shirikisho la Kandanda Duniani au FIFA.
Nafasi ya "Mhamasishaji" kama aliyonayo Manara haipo katika muundo wa FIFA, hivyo anaweza tu kuwa ni shabiki wa Yanga ambaye hawezi kushtakiwa katika Kamati ya Maadili ya TFF ila mahakamani kama alimdhalilisha Karia.
Alipaswa ashtakiwe Kituo cha Polisi na Karia mwenyewe, kisha apelekwe mahakamani kama mtu binafsi na mlalamikaji akawe shahidi wa Jamhuri kama mtu binafsi na siyo kama Rais wa TFF.
Katika kutekeleza mfumo na muundo wa FIFA, Yanga yenyewe ina Afisa Habari wake, Hassan Bumbuli. Huyo ndiye anaweza kushtakiwa katika Kamati ya Maadili ya TFF.
Kutokana na hali hiyo na hata vinginevyo, swali linalozuka hapa ni je, tangu lini Manara ni kiongozi wa kuchaguliwa au afisa wa kuteuliwa wa Yanga kwa kuzingatia muundo wa FIFA?
Ni cha kujifunza hapa na kukishika kila mshabiki na kukipigia kelele siku zote hadi Manara atakapoachiwa huru ni wajibu ni kwa nini mashabiki au shabiki anaporusha chupa ya maji uwanjani inaazibiwa klabu na si mhusika why Manara ahukumiwe kama yeye wakati anaipigania timu.