Sekretarieti ya Ajira na Database

Malunkwi

JF-Expert Member
Jan 19, 2011
339
79
Kwa wale waliofanya written interview ya Nationa Audit Office Sept 2011 waliambiwa kuwa Sekretariet iliamua kuita watu wengi ili iwaweke kwenye Database wale watakaofanya vizuri na litakapotokea hitaji la Auditors & Accountants(Wakaguzi/Wahasibu) serikalini bac watakua wakiitwa wale waliowekwa kwenye database hivyo hakutakua na haja ya kutangaza tena nafasi hizo hadi waliopo ktk Database watakapokwisha. Hivi karibuni watu wamekua wakiitwa kwenda kuchukua barua za Ajira na kwenda kuripoti kazini NAO na baadhi ya Wizara(ushahidi ninao). Sasa wasiwasi wangu ni kwamba kwanini wanaita watu kimyakimya? Na je tutaamini vipi kua hao wanaoitwa walifaulu ktk mchakato mzima wa usaili wkt Sekretarieti haikutoa orodha yao?
Upo uwezekano mkubwa wa kuingizana kwenye ajira za serikali pasipo hata kufuata taratibu hivyo sina imani na Sekretarieti ya Ajira, kwani watoto wa wakulima wataendelea kuchoma nauli zao kutoka mikoani kuja Dar es salaam kufanya usaili ambao nafasi zake tayari watoto wa walio ktk system washaanza kula mishahara.
 
Bado hawa jamaa hawajajipanga vizuri hata ule utaratibu wa kuondoka na matokeo ya written interview na kuwaahidi watu kuwa watapigiwa simu sidhani kama unazuia mianya ya kuweka mtu kwani hata matokeo hayaonyeshwi. Sijui hata shule tungekuwa tunafanya mitihani kisha tunaambiwa kuwa watakaofaulu watapigiwa simu ingekuwaje maana hata matokeo hupewi wala huyaoni ni kwenda kwa imani tu. nadhani kuna haja ya hawa watu kujifunza vitu vingi kuepuka malalamiko kama haya ukizingatia watu wanatumia gharama zao badala ya kusulubu watu kwa shida zao. Ni maoni binafsi
 
huu ni ukweli mtupu. hata mimi nakumbuka hicho kitu kilisemwa na mkubwa kutoka pale tume ya ajira. tena tuliambia na wasimamizi kuwa tunamsubiri huyo mkubwa wao anataka kuongea na sisi KWA BAHATI MBAYA turimsubiri kwa muda mrefu na hatukufanya mtihani paka yeye alivyokuja kuongea hayo maneno alipo toa hizo ahadi ndipo tulipo anza ule mtihani.
Cha ajabu kila kukicha wanatangaza hizo nafasi BILA kujitathimini wenyewe kuwa kuna ahadi waliitoa kwa watu zaidi ya alfu mbili (2000) ambao walikuwa katika huo mtihani.

TANZANIA BWANA'
Viongozi wetu wamejaa na ubabaishaji ndo mana wakitoa ahadi hawazikumbuki coz kila kukicha wao wanatoa ahadi mpya, hivyo ni vigumu katika hali ya kawaida kizikumbuka zote
 
kaka kwani una mda gani unaishi tanzania ucjue ivyo vitu??? zile ni protocal tu kazi zinawenyewe zile mkuu
 
Back
Top Bottom