Barbarosa
JF-Expert Member
- Apr 16, 2015
- 22,584
- 27,838
Nimebahatika kutembelea nchi nyingi Dunia hii, zote nchi tajiri na nchi Masikini, kitu mabacho nimejifunza ktk kwa Wananchi wa nchi zote hizo ni kwamba sehemu kubwa ya Binadamu wote ni Wapumbavu na haijalishi ni wa nchi Masikini au nchi tajiri, na kwa kuwa sehemu kubwa ya Binadamu ni Wapumbavu basi wanatoa nafasi ya kudanganywa na kutawaliwa maisha yao yote na kundi dogo la maelite ambao ndiyo wamejimilikisha Mali za walio wengi.
Kwa mfano nchi ya Marekani inasemekana asilimia moja (1%) ya Wananchi anamiliki zaidi ya asilimia 90 (90%) ya uchumi wa nchi hiyo lkn ukiongea na wananchi wa nchi hiyo watakwambia wanaishi in freedom, watakwambia wana demokrasia bora Duniani na cha kushangaza zaidi ukifika uchaguzi wanarundikana kwenda kupiga kura ingawaje inajulikana kwamba Raisi wa Marekani huteuliwa na hiyo 1% wanapewa ahadi kede kede kama vile Obama alivyowadanganya Change lkn mwisho wa siku hakuna alichokifanya!
Sasa anakuja Bush ambaye Baba yake, kaka yake pia alikuwa Raisi na wote walikuwa failure lkn anawapiga porojo kwamba yuko tofauti, anawadanganya hivyo hivyo watajazana tena kupiga kura lkn matokeo hayabadiliki bado 1% inamiliki Uchumi wote!
Ukija kwenye nchi kama Libya siku Gadafi ameuliwa na waLibya wenyewe chini ya NATO Walibya walikuwa wanafanya pati kushangilia. Kumbuka kwamba Libya wakati wa Gadafi wananchi wasiokuwa na kazi walikuwa wanalipwa na Ustawi wa Jamii, huduma zote zilikuwepo na ni Bure, walibya walikuwa wakimaliza Sekondari na kama amepata Chuo nje ya Nchi Serikali inalipa kila kitu, ingawaje Libya ni Jangwa lkn Gadafi alianzisha Mradi mkubwa sana wa Maji na Kilimo, yote hii kwa ajili ya Wananchi wa Libya lkn mwisho wa siku walicheza barabarani alivyouliwa na leo hii hata nchi hawana tena, Rasilimali zao wazungu wananyonya mafuta juu kwa juu wanaondoka wanaenda kuuza, kila kitu kimekufa!
Ukienda Singapore utakutana na Wananchi wanalalamika na kulaani Serikali yao kwamba ni ya kidikteta na haijafanya chochote tangu Uhuru ingawaje serikali hiyo hiyo wanyoilalamikia imeitoa Singapore ktk nchi masikini kwenda kuwa moja kati ya nchi tajiri Duniani, leo hi Singapore ni ya Tano kwa Utajiri Duniani...
Hivyo nilichojifunza ni kwamba sehemu kubwa ya Binadamu na haijalishi wako nchi gani ni Wapumbavu na hawajui hata wanataka nini na huwa kwa kiasi kikubwa wanastahili maisha wanayoishi!
Kwa mfano nchi ya Marekani inasemekana asilimia moja (1%) ya Wananchi anamiliki zaidi ya asilimia 90 (90%) ya uchumi wa nchi hiyo lkn ukiongea na wananchi wa nchi hiyo watakwambia wanaishi in freedom, watakwambia wana demokrasia bora Duniani na cha kushangaza zaidi ukifika uchaguzi wanarundikana kwenda kupiga kura ingawaje inajulikana kwamba Raisi wa Marekani huteuliwa na hiyo 1% wanapewa ahadi kede kede kama vile Obama alivyowadanganya Change lkn mwisho wa siku hakuna alichokifanya!
Sasa anakuja Bush ambaye Baba yake, kaka yake pia alikuwa Raisi na wote walikuwa failure lkn anawapiga porojo kwamba yuko tofauti, anawadanganya hivyo hivyo watajazana tena kupiga kura lkn matokeo hayabadiliki bado 1% inamiliki Uchumi wote!
Ukija kwenye nchi kama Libya siku Gadafi ameuliwa na waLibya wenyewe chini ya NATO Walibya walikuwa wanafanya pati kushangilia. Kumbuka kwamba Libya wakati wa Gadafi wananchi wasiokuwa na kazi walikuwa wanalipwa na Ustawi wa Jamii, huduma zote zilikuwepo na ni Bure, walibya walikuwa wakimaliza Sekondari na kama amepata Chuo nje ya Nchi Serikali inalipa kila kitu, ingawaje Libya ni Jangwa lkn Gadafi alianzisha Mradi mkubwa sana wa Maji na Kilimo, yote hii kwa ajili ya Wananchi wa Libya lkn mwisho wa siku walicheza barabarani alivyouliwa na leo hii hata nchi hawana tena, Rasilimali zao wazungu wananyonya mafuta juu kwa juu wanaondoka wanaenda kuuza, kila kitu kimekufa!
Ukienda Singapore utakutana na Wananchi wanalalamika na kulaani Serikali yao kwamba ni ya kidikteta na haijafanya chochote tangu Uhuru ingawaje serikali hiyo hiyo wanyoilalamikia imeitoa Singapore ktk nchi masikini kwenda kuwa moja kati ya nchi tajiri Duniani, leo hi Singapore ni ya Tano kwa Utajiri Duniani...
Hivyo nilichojifunza ni kwamba sehemu kubwa ya Binadamu na haijalishi wako nchi gani ni Wapumbavu na hawajui hata wanataka nini na huwa kwa kiasi kikubwa wanastahili maisha wanayoishi!