Acha mhemko bad things happen.Mtaani kuna makubwa zaidi ya kutobolewa macho.The thing is sheria ichukue mkondo wake na kuhusu mhanga huyo well ni mbaya kapoteza uwezo wa kuona na inasikitisha sana lakini despite all maisha lazima yaendelee....
Huyu anatoa hukumu halafu anataka tena aende mahakamani!
Kumtoa mtu jicho (jicho kwa jicho) ni hukumu tayari.
Kibaya Zaidi anaitaka serikali ndiyo imuhukumu, anasahau huo ni wajibu wa mahakama.
angeomba serikali izidishe ulinzi (hapo unalizungumzia jeshi la polisi, serikali ya mtaa, halmashauri na jiji)
Then ungeliomba bunge, liangalie sheria zake zinazohusu masuala haya ya uhalifu wa aina au ukubwa huu, kama unaona zina mapungufu lakini... maana ile mahakama haiwezi kuhukumu nje ya kile kinacho ainishwa na sharia/kifungu au kanuni au taratibu husika.
Jifunze kuwa mahakani ni sehemu ya kusimamia haki na sio kuadhibu kwa hisia.
inawezekana hata huyo aliyepelekwa mahakamani kama scorpion akawa kasingiziwa, kumbe watu kwa kumuogopa scorpion au kwa kuwa ana immunity ukaletewa mtu mwingine kumponya yule muharifu, so mahakama inatoa nafasi pia kwa umma (walioathiriwa) na kwa huyo mshtakiwa kuthibitisha kuwa kweli parties zote zimewakilishwa kisheria, then kujua kweli kosa tajwa limetendeka, na nini kimepelekea kosa hilo kutendekea. mwisho hakimu anaringanisha matukio, ushahidi na utetezi ili afikie suluhisho sahihi kwa faida ya wote, mshtaki (aliyepatwa madhara), mshtakiwa na umma.
kuna wakati unaweza kukuta kumbe scorpion ni mwendawazimu, sasa unamnyonga badala ya kumtibu, au na yeye alikuwa analipiza kisasi kwa bwana saidi (haimpi msamaha, lkn ktk mambo ya hisia kumbe halijichukulia sharia mikononi kama wewe) au ni mualifu ambaye motives zake ni za kihalifu tu, na hivyo anahitaji hukumu kama ilivyo andikika.
anyway mi si mwana sharia lakini nadhani tuache mahakama ihukumu kwa kufuata kanuni na taratibu na sio kuridhisha umma, haitowezekana. (mfano mwepesi angalia kesi ya babu seya na jinsi umma ulivyo na different opinions, hiyo ndio hatari ya kufuata hisia)